• No results found

Uhalisiajabu katika riwaya ya babu alipofufuka (2001) ya S.A mohamed na bina-adamu! (2002) yA K.W Wamitila

N/A
N/A
Protected

Academic year: 2020

Share "Uhalisiajabu katika riwaya ya babu alipofufuka (2001) ya S.A mohamed na bina-adamu! (2002) yA K.W Wamitila"

Copied!
131
0
0

Loading.... (view fulltext now)

Full text

(1)

UHALISIAlABU

KATIKA RIWAVA VA BABU ALIPOFUFUKA

(2001)

VA S.A MOHAMED NA BINA-ADAMU! (2002)

VA K.W

WAMITILA

NA:

JACINTA KAGENDO

~GAJU

IDARA VA KISWAHILI NA LUGHA ZA KIAFRIKA

CHUO KIKUU CHA KENVATTA

Tasnifu hii imetolewa iIi kutosheleza baadhi ya mahitaji ya Shahada

ya Uzamili katika Chuo Kikuu cha Kenyatta

AGOSn

2004

Magaju, Jacinta, Uhalisiajabu katika riwaya ya 'Babu

1111111111111111111111111111111111111111111111111111111 OS/277415

(2)

IKIRARI

Tasnifu hii ni kazi yangu binafsi na haijatolewa kwa mahitaji ya shahada katika Chuo Kikuu

kingine.

JACINTA KAGENDO MAGAJU

Tasnifu hii imetolewa kutahiniwa kwa idhini yetu kama wasimamizi wa kazi hii katika Chuo

hiki.

&

-

(

DKT. R.M. WAFULA

Na

,

(3)

G-O---TABARUKU

Naitabaruku kazi hii kwa mume wangu mpenzi Franklin Magaju. Mbali na kunihimiza kila nilipohisi kulemewa na kuwa nami kwa kila hatua, ulinifaa kwa hali na mali. Binti zangu wapendwa Doreen Kinya na Emily Mukami hawawezi kusahaulika kwa uvumilivu wao si

haba nilipokuwa nikisoma. Mwisho ni kwa kitindamimba changu David Mwenda. Asante

(4)

IV YAlIYOMO Mada Ikirari Tabaruku Yaliyomo ...•...•..••....•...

Shukrani

••••••••••••••••••••

"

'

r •••••••••••••••••••••••••••••••••

c •••••••••••••••••••••••••••

Ikisiri ...

1.II' 11.1 ••II ••••••• II•••• II. I" II. II ••••• 1.11.11. II. II•••••••••••••••• 11.11 ••1 ••1 ••

SURA YA KWANZA

1.0

Utangulizi ...II. II. II. II •••• II. II. II ••••••• 11.11. II. II •••• I••••• II •••• II' II

1.1

Usasa, Usasaleo, Uhalisiajabu ...•..

1.2

Mada ya Ut:afiti II. II••••••• I •• 11 ••1 •••••••••••••• 1 ••1.11 ••1.1 ••

1

.

3

Yaliyoandikwa kuhusu Mada ...•... II. II. II •••• II •••• II. II •••••

1.4

Maswala la U'tafiti ..II •••• II' II. II. II' II •••• II. 11.11. II. II ••••••• II' II' II

1.5

Malengo Ya Utafiti

1.6

Sababu ya kuchagua Mada ...••...••.••...•

1

.

7

Upeo wa Utafiti

1.8

Misingi ya Nadharia ...•...•••.•...•.••

1.9

Mbinu

za

Utafiti .

1.1

0

Kiishilio .,...•...

SURA YA PILI

2.0

Utangulizi ...•....••••...•.•••...••...••...

2.1

Vipindi vya uandishi wa S.A. Mohamed .

2.

1

.

1

Kipindi cha Uhalisia hakiki .

(5)

2.1.2

2.1.3

2.1.4

2.2

2.2.1

2.2.2

2.3

Kipindi cha Uhalisia wa Kijamaa .

Hatua za mwanzo za Uhalisiajabu .

Kipindi cha Uhalisiajabu ...••...

Vipindi vya uandishi wa K.W Wamitila .

Hatua za mwanzo za Uhalisiajabu .

Kipindi cha Uhalisiajabu .

Kiishilio I •••••••••••••• 11 •••••••• 1 ••••••• I" II••••••••••••••••••••

SURA YATATU

3.0

3.1

3.1.1

3.1.2

3.1.3

3

.

2

3.3

3

.

4

3.5

3

.

6

3.7

3

.

8

Utangulizi

Muhtasari wa Riwaya ya 8abu Alipofufuka .

Sehemu ya Kwanza ..

II. 11.11 ••••••• II. II. II •••• II' II. II ••••• I. II' II. II

Sehemu ya Pili II. II. II. II' •••••••••••• II •••• II. 11.11. II •••• II. II.

Sehemu ya Tatu ..II •••• II. I•••••••• II' II' II. II •••••••••• II. 1 ••• 1. II' II ••

Matukio ya Kiajabuajabu .

Ndoto na Uhalisia ..II. II. II. II •••• II. 11.11. II. II. I•• II. II ••••••• II' II. II

Uduara wa Wakati

Uvunjaji wa Mipaka ya Mahali

Mtindo wa Riwaya

·Visaasili ••••••••••••••••••••••••••..•••• ,» •••••••••••••••••••••....•••..•••••

(6)

vt

SURAVA NNE

4.0

Utangulizi 11 •••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••

4.1

Muhtasari wa Riwaya ya Bina-Adamu! .

4.1.1

Sehemu ya Kwanza ..II' II' II. II •••• 11.11. II. II. II. II. II ••••••• II ••••

4.1.2

Sehemu ya Pili ..11.11. II' II. II. 11.11. II. 11.11.11.11. II. II. II•••••••••••

4.1.3

Sehemu ya Tatu

Matukio ya Kiajabuajabu

4.2

4.3

Ndoto na Uhalisia ..II. II. II. II. II. II' •••••• II •••• II' 11.11 ••••• 1 •••• II ••

4.4

Uduara wa Wakati

4.5

Uvunjaji wa Mipaka ..II. II. II. II. II •••• II. II. II •••• II. II ••••••• II. II ••••

4.6

Visaasili .~ •••••••••••••••••••••••••••••••••••••••• a •••• a •••••••••••••••••••••

4.7

Kiishilio ..II•••••••••• II••••••••••••••• 10:1.II. II. 11••1.II. 11.11 •••• I ••I" II••

SURAVA TANO

5.0

Hitimisho ...11 ••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••

5.1

Matokeo ya Utafiti .

5.2

Matatizo ...t.I•••••••••••••••

5.3

Mchango ...•...

5.4

Mapendekezo .

(

MAREJElEO •••••••••••••••••••••••••••••••••••••••• ,.••••••••••••••••• 1 •••••••••••••••• I ••••

(7)

SHUKRANI

Kwanza natoa shukrani kwa Mungu Muumba kwa kunijalia afya na uwezo wa kuifanya kazi

hii. Namshukuru Dkt. Richard Wafula ambaye mbali na kuwa msimamizi wangu, alinishauri

na kunitia moyo katika kila hatua ya utafiti huu. Natoa shukrani kwa Dkt. catherine Ndungo

kama msimamizi wangu kwa kunishauri na kuniongoza katika kazi hii.

Nawashukuru wahadhiri wote wa Idara ya Kiswahili na Lugha za Kiafrika wa Chuo Kikuu

cha Kenyatta kwa motisha walionitia wakati nilipokuwa nikitafiti.

Shukrani zangu zimwendee Profesa Kimani Njogu aliyenitia mshawasha wa kushughulikia

swala la utafiti huu. Dkt. Kyalo Wamitila hawezi kusahaulika. Namshukuru kwa kunifaa kwa

vitabu namajalada yaliyoshadidia pakubwa usomaji wangu wakati nikitafiti.

Nawashukuru wengine wote waliochangia kwa njia moja au nyingine katika ufanisi wa

(8)

\111

IKISIRI

Utafiti huu umeshughulikia swala la uhalisiajabu katika riwaya teule za fasihi ya Kiswahili.

Riwaya zilizohakikiwa ni Babu Alipofufuka (2001) ya S.A. Mohamed na Bina-Adamu!

(2002) yaK.W. Wamitila. Nadharia iliyoongoza utafiti huu ni kitengo kimoja cha mwelekeo

wa usasaleo. Hii ni nadharia ya uhalisiajabu. Katika nadharia ya uhalisiajabu, matukio

yanasawiriwa kiajabuajabu, ni ya kuogofya na kutisha. Matukio haya huashiria hali halisi ya

maisha katika jamii. Uhalisiajabu ni mtindo wa riwaya wa hivi majuzi unaopiku njia za

kimapokeo za uandishi wa fasihi ya Kiswahili na usawiri wa jamii. Kimapokeo, riwaya

inapaswa kujengeka katika misingi ya uhalisia.

Tasnifu hii ina jumla ya sura tano. Sura ya kwanza ni utangulizi wa utafiti. Hapa ndipo

tumeshughulikia mada ya utafiti, malengo ya utafiti, sababu za kuchagua mada na

yaliyoandikwa kuhusu hii mada. Aidha, tumejadili upeo wa utafiti huu na misingi ya

nadharia iliyouongoza. Mwisho, mbinu za utafiti zimeelezwa.

Sura ya pili imejadili maisha ya waandishi S.A. Mohamed na K.W.Wamitila. Tumeonyesha

vipindi mbalimbali vya uandishi wao. Uchunguzi huu umedhamiria kuonyesha mitindo

waliyoitumia tangu waanze kuandika na pia kuonyesha ni kwenye kipindi gani cha uandishi

waliingilia uandishi wa kihalisiajabu na kwa nini walifanya hivyo.

Sura ya tatu na nne zinachunguza jinsi riwaya za Babu Alipofufuka na Bina-Adamu!

zimetumia uhalisiajabu katika kuwasilisha ujumbe. Tumeonyesha mihimili ya nadharia ya

uhalisiajabu waliyoitumia. Mihimili hii ni pamoja na matukio ya kiajabuajabu, ndoto na

uhalisia, uduara wa wakati, visaasili, uvunjwaji wa mipaka ya mahali na upekee wa mtindo

wa riwaya ya kihalisiajabu. ,;~

Sura ya tano imehusika na kulinganisha na kulinganua riwaya zote mbili kwa mujibu wa

mada husika. Aidha, matokeo ya utafiti, matatizo yaliyokabiliwa katika utafiti na

(9)

Kutokana na utafiti huu, imebainika wazi kwamba Mohamed na Wamitila wanatumia

uhalisiajabu kimakusudi.Mihimili mikuu ya uhalisiajabu imo katika kazi zao. La maana zaidi

ni kwamba wanatumia uhalisiajabu kama mkakati unaowawezesha kujadili maswala

yanayousibu ujirani wetu. S.A. Mohamed anatumia mkakati huu kumulika rnatatizo ya

kiuchumina ya kijamii yanayowakabili Waafrika kutokana na utawala finyu wa viongozi

wao. K.W.Wamitila anatumia mtindo huo huo kuupiga vita utandaradhi na ubepari wa

kimataifa. Pamoja na kuonyesha matatizo yanayoyakabiliwa na Waafrika, Mohamed na

Wamitilawana imani kwamba matatizo ya Waafrika yanaweza kutatuliwa si kwa kutafuta

tiba hukonje katika mataifa ya Kimagharibi, bali kwa kuyatafuta humuhumu barani Afrika

(10)

SURAVA KWANZA

1.0 Utangulizi

Katika sura hii tumeshughulikia mada ya utafiti. Tumetambulisha mada yetu ambayo ni

kuchunguza jinsi uhalisiajabu unavyojitokeza katika riwaya za S.A Mohamed Babu

Alipofufuka(2001) na K.W Wamitila Bina-Adamu! (2002). Maswala na malengo ya utafiti

yameshughulikiwa pia. Tumejadili yale yaliyoandikwa kuhusu mada yetu. Hizi ni kazi

mbalimbali za kihakiki kuhusu uhalisiajabu katika uandishi wa sehemu mbalimbali

ulimwenguni kwa jumla, barani Afrika, kwenye fasihi ya Kiswahili na hatimaye na muhimu

zaidi katika riwaya zetu mbili. Aidha, yaliyoandikwa kuhusu nadharia ya uhalisiajabu

tunayoitumia katika uhakiki wetu yamepitiwa.

Tumefafanua sababu za kuchagua mada tunayoishughulikia na pia kuelezea upeo wa

utafiti wetu. Nadharia tunayoitumia imeelezewa na hatimaye mbinu za kukusanya,

kuchanganua na kuwasilisha data zimefafanuliwa.

1.1 Uhalisia, Usasaleo na Uhalisiajabu

Uhalisia ni mojawapo wa matapo maarufu katika ulimwengu wa fasihi na lenye athari

kubwasana. Kwanza uhalisia huashiria tapa la kipindi maalum cha kihistoria katika fasihi

ya Ulaya na pili huelezea aina ya mtazamo au tapa la kifasihi ambapo kazi za kifasihi

zinachukuliwa kama zinazohifadhi au kuakisi sifa za kimsingi zinazohusishwa na uhalisi.

Kazi zinazoangaliwa kama za kihalisia zinatarajiwa kuwa akisio la hali halisi ya maisha

katika jamiii inayohusika (Wamitila 2002: 114).

Uandishi huu ndio uliopokelewa katika baadhi ya nchi za Kiafrika ukawa uhalisia na uhalisia

wa kijarnaa. Uliingia katika riwaya ya Kiswahili katika kazi za waandishi kama vile

(11)

Shaft kwenye Kasri va Mwinvi Fuad (1978) na Kuli (1979) na Mohamed S. Mohamed

kwenye Kiu (1972) na Nvota va Rehema (1976) miongoni mwa nyingine.

Usasaleo ni dhana inayotumiwa kuelezea mielekeo ya kitamaduni na kisanaa

mavonusishwa

kwa kiasi kikubwa na karne ya ishirini. Kimsingi, dhana hii hutumiwa

../

kuelezea au kuzitambulisha sifa mpya za dhamira, tanzu, dhana na mitindo ya kifasihi

inayohusishwa zaidi na miongo ya kwanza ya karne ya ishirini. Wakati unaohusishwa zaidi

na mkabala huu ni Vita Vikuu vya Pili vya Ulimwengu. Ni muhimu ikumbukwe kwamba

Vita Vikuu hivi vilisababisha uvunjifu mkubwa wa maendeleo na utamaduni wa kimagharibi.

Katika hali hii palihitajika njia, mbinu na hata miundo tofauti ya kuangazia na kuelezea

uvunjifu huo (Wamitila 2002: 123-124).

Harrow (2002:3) anasema kwamba fasihi ya Kiafrika katika karne ya ishirini imekua na

kutoka katika ushairi wa asili wa hapo awali wa kinegritudi (swala la ujitambuzi wa

Mwafrika) hadi kufikia riwaya za kisasa za hivi majuzi za uhalisiajabu. Waandishi wa riwaya

na mashairi walipoendelea kushuhudia mambo ya kipekee katika maisha yao na jamii zao,

mikakati mipya ya uandishi ilianza kujitokeza. Swala hili la mabadiliko liIijitokeza katika

shughuli za waandishi waliokabiliwa na migogoro ya jamii zao na wanaokusudia kuanzisha

utaratibu rnova wa kijamii na kitamaduni. Hapo awali waandishi wengi wa Kiafrika

wa uhalisia katika uandishi wao kwani ndio uliokuwa

ume oelewa na kukita mizizi.

Uhalisia huu ulitokana na mapokeo ya Kimagharjbi. Kizazi cha kwanza cha waandishi wa

Kiafrika kilisomea katika vyuo vya kimagharibi au vyuo vilivyoazima mitaala kutoka kwa vyuo vikuu vya kimagharibi. Hivi ndivyo waandishi kama Chinua Achebe, Ngugi wa

Thiong'o, Wole Soyinka na Ayi Kwei Armah waliandika kazi zao kama vile A Grain of Wheat,

(12)

3

Uhalisiauna misingi yake katika maendeleo na ustaarabu wa jamii za Kimagharibi. Uhalisia

ulifika kilele chake katika kipindi cha mapinduzi ya viwanda na maendeleo mengine ya

kisayansi.Hivyo basi, uhalisia kama ulivyopokelewa hapo awali barani Afrika ni kielelezo

cha mitazamo na mielekeo liliyothaminiwa na jamii za Kimagharibi. Uhalisia ndio uliowapa

wazungu mantiki na motisha wa kutawala wananchi wa maeneo mengineyo. Waafrika

"waliazima" uhalisia kam~ ambavyo walivyoazima mambo mengine ya Kimagharibi.

Inaelekea kwamba uhalisia wa kifasihi kama amali zingine zilizoazimwa kutoka kwa jamii za

kimagharibi haujaleta maendeleo bora katika mitazamo ya Waafrika. Hii ndiyo sababu

ambayo imewafanya baadhi ya waandishi wa Kiafrika kuanza kuandika kwa kutumia mbinu

zingine za usanii. Waandishi wa Kiswahili hawajaachwa nyuma katika shughuli hii. Katika

karne ya ishirini na miaka ya mwanzo ya karne ya ishirini na rnoja, kumeibuka baadhi ya

riwaya za Kiswahili ambazo zinadhihirisha vipengele vya uandishi wa usasaleo. Usasaleo

haukuibuka katika ombwe tupu. Kwa hakika usasaleo ni njia ya kuufinyanga ukweli wa

maisha kwa njia tofauti na vile ilivyozoeleka. Wasanii wanaoutumia hawautumii tu kwa ajili

ya kuutumia bali kwa lengo la kuangazia hali zao katika jamii wanamoishi

(Gromov 2002:3-4).

Uhalisiajabu ni mojawapo wa mikondo tofa utitofa uti ya usasaleo kama vile udenguzi wa

lugha, nadharia baada ukoloni na baadhi ya nadharia za kifeministi. Kutokana na kusoma

kwangu kwa riwaya ya Babu Alipofufuka (2001) na Bina-Adamu! (2002), nimegundua

kwamba riwaya hizi zina mwelekeo wa uandishi wa kihalisiajabu.

Katika mojawapo ya makala kuhusu maendeleo ya hivi karibuni ya riwaya ya Kiswahili Said

A.Mohamed katika Gromov (2002: 12) anasema:

Miongo ya mwisho ya karne ya ishirini ni kipindi mwafaka cha maendeleo ya

(13)

mbawa zao zimekatwa huku mashetani wakitembea wapendavyo na kuingia popote bila kikwazo chochote. Tunaishi katika ulimwengu ambao binadamu

amepokwa kwa kila njia kwa maslahi ya kiuchumi. Ni ulimwengu ambao hakuna aliye na uhakika kuhusu sio kesho tu bali hata leo, ambao watu hawakumbuki jana ... Ni ulimwengu ambao mambo ambayo hayangefikirika katika mwongo uliopita yanadhaniwa kuwa ya kawaida ... Ndio maana waandishi wengi wa Kiswahili wanashughulikia maswala ya kilimwengu kwenye kazi zao.

Wanafanya hivyo kwa mtazamo wa kisasa slo kwa kutoa maelezo ya matatizo ya ulimwengu wa leo, bali kwa kwanza kujaribu kuchunguza ukosefu wa mantiki wa matukio ya ulimwengu wa leo. IIi kuweza kutekeleza jukumu hili,waandishi wanatumia uhalisiajabu, uhalisiafifi na usasaleo - mitindo iliyoanzishwa katika fasihi ya Kiswahili katika miaka ya sabini.(Tafsiri yetu)

Riwaya za Babu Alipofufuka (2001) na Bina-Adamu! (2002) ni mifano ya uandishi huu.

Kwa kuzikabili riwaya hizi kama za kiuhalisiajabu, tumeweza kuzielewa vizuri zaidi na

kujua ni misingi gani au vichocheo vipi viliwasukuma waandishi hawa hata wakaanza

kutumia mbinu hii. Pamoja na haya, tumeweza kutambua sababu zilizowafanya kuasi

mbinu za awali kama vile uhalisia na uhalisia wa kijamaa.

1.2 Mada ya utafiti

Utafiti huu unakusudia kuchunguza jinsi vipengele vya uhalisiajabu vinavyodhihirika katika

riwaya ya Said Ahmed Mohamed Babu Alipofufuka (2001) na ya K.W. Wamitila

Bina-Adamu! (2002). Aidha, utafiti huu utabainisha jinsi uhalisiajabu unavyoshughulikia kadhia

zinazohusu maisha halisi ya watu wanaozungumziwa katika riwaya za Kiswahili teule.

Kutokana na jambo hili, tutaonyesha ni kwa nini uhalisiajabu ni njia mwafaka zaidi ya

(14)

5

1.3 Yaliyoandikwa kuhusu mada

Alexander (1990: 127) anasema kwamba uhalisiajabu ni kielelezo cha jinsi nadharia ya

usasaleo inavyotulazimu kufikiria upya juu ya dhana za kimapokeo kuhusu riwaya ya

uhalisia ya karne za kumi na nane na kumi na tisa. Aidha, uhalisiajabu umetulazimu

kuwazia ufaafu wa baadhi ya mitindo ya uandishi kwa mada tofauti tofauti. Baadhi ya

maendeleoya kuslsirnua katika mwisho wa karne ya ishirini ni kuwa kumeibuka waandishi

wanaotalii uhusiano kati ya historia na masimulizi ya ubunifu. Waandishi wa riwaya wa

Marekani Kusini Gabriel Garcia Marquez, Isabel Allende na Vargas Llosa kati ya wengineo

wameibusha na kutumia visaasili vya kitaifa katika kazi zao. Visaasili vya kitaifa ni visa

vinavyojaribu kuelezea mustakabali wa taifa lote kwa ujumla.

Drouart (1993) anasema kwamba tangu miaka ya 1950 na 1960, dhana ya uhalisiajabu

imehusishwa sana na uandishi wa kibunifu katika Marekani Kusini. Katika miaka ya 1940

huko Marekani Kusini, uhalisia wa kimaajabu ulikuwa njia ya kudhihirisha fikra za kikweli za

Wamarekani kusini na kuunda mtindo mpya wa kipekee na huru wa fasihi. Hata hivyo, ni

muhimu sana kujua kuna to fauti kati ya uhalisiajabu katika sanaa ya uchoraji na

uhalisiajabu katika sanaa ya uandishi hususan fasihi.

Roh (1925) alitumia neno uhalisiajabu katika mukhtadha wa ulimwengu wa sanaa

kuelezea aina fulani maalum ya kudhihirisha usiri ulioko kwenye maisha ya kila siku bila

kuupigia maswali yoyote uhalisia huo. Pamoja na hayo, uhalisiajabu katika kazi ya sanaa

hushughulika na kazi zinazoambatana na zisizoambatana na ujumi wa uhalisia.

Kulingana na Ousbv (2002) riwaya mashuhuri zaidi ya kiuhalisiajabu ni ile ya Gabriel Garcia

Marquez One Hundred Years of Solitude (1980). Riwaya hii ilichangia kutuzwa kwa

(15)

Riwaya zingine za Marquez zingine zinazoafiki utanzu huu ni pamoja na Chronicle of

Death Foretold (1983) na Love in the Time of Cholera (1985). Marquez aliathiriwa sana

katika uandishi wake na mitazamo na hali ya maisha ya umma uliokuwa mchanganyiko wa

Waafrika,Wahindi katika sehemu aliyozaliwa huko Colombia ya Marekani Kusini.

Chanady(1985) katika Rio (1999) anasema kwamba uhalisiajabu unahusu matukio yasiyo

ya kawaida, ya kiujiza au chochote kile kilicho kinyume cha uhalisia wa kawaida. La

muhimu zaidi ni kwamba matukio yanayotendeka katika uhalisiajabu hayawezi kujitenga na

uhalisia.

Floyd·Merrel anaelezea kwamba uhalisiajabu unatokana na hali mbili za ulimwengu

zinazopingana. Uhalisiajabu una misingi yake katika uhalisia au ulimwengu ambao

mwandishi anaujua, na pia humwezesha mwandishi kuuona uhalisia ambao kwa kawaida

hatuufahamu.

Okah (2002:94) akizihakiki kazi za Okri (1991) anatuelezea kwamba katika uhalisiajabu

uhalisia na ndoto havitofautishwi. Anaeleza kwamba:

Kwa kuingilia uwanja wa uhalisiajabu, Okri anatoa maelezo ya maisha nchini Nigeria. Maisha ya uhalisi na ya ndoto hayatofautishwi katika nchi hii ya Abiku. Maisha nchini Nigeria ni kama ya ndoto na yasio na mantiki. Kipengele hiki cha kifantasia kinafaa sana kufafanulia hall mbaya ya mambo katika taifa hili.

(Tafsiri yetu)

Gromov (2002:3-4) anaelezea usasa leo kuwa njia ya kuufinyanga ukweli wa maisha kwa

njia tofauti na vile ilivyozowewa. Yaani, wasanii wanaoutumia hawautumii tu kwa ajili ya kuutumia bali kwa lengo la kuangazia hali za jamii wanamoishi. Kulingana na Gromov

(2002), uhalisiajabu ni kitengo cha usasaleo ambacho kimefanikiwa kuzungumzia maswala

(16)

7

Mbatiah (2002:60) anaeleza kwamba uhalisiajabu ni istilahi inayotumiwa kuelezea mkondo

wa uandishi ambapo mazingira, matendo na matukio ya kifantasia husawiriwa kwa kuiga

mtindo wa uhalisia. Uhalisiajabu hufanya hivyo kwa kuyaeleza matukio kwa njia ya moja

kwa moja kana kwamba ni mambo ya kawaida. Wasanii wanaoutumia mtindo huu

hudhamiria kuonyesha kuwa ingawa mambo yanayoshughulikiwa ni ya kiajabuajabu,

hutokea katika maisha ya kawaida ya jamii inayohusika. Uhalisia wa kimaajabu huusishwa

zaidi na nchi zinazoendelea kutoka bara la Afrika, Marekani ya Kusini na Bara Hindi.

Wamitila (2003:274) naye anasema dhana ya uhalisiajabu huhusishwa na waandishi wa

Marekani ya Kusini au hata nchi zinazoitwa ulimwengu wa tatu. Sifa yake kuu ni

kuyaelezeamatukio ya kifantansia au ya kiajabu au kichawi kwa namna ya moja kwa moja

na kwa namna inayoyafanya yaonekane ya kawaida tu. Sababu hasa ya matumizi ya

mtindo huu ni kuonyesha kuwa matukio ya aina hii hupatikana katika maisha ya kawaida

katika jamii zinazohusika. Waandishi wanaoandika katika misingi hii hushikilia kuwa

mtazamo wao wa uhalisia unawakilisha msimamo wa jamii zao. Mpaka uliopo kati ya

mambo yanayoweza kupatikana katika ulimwengu halisi na yasiyowezekana kuwepo katika

ulimwengu huo huwa mdogo sana.

Hadi kufikia miaka ya 1960, fasihi ya Marekani kusini ilikuwa haitiliwi maanani na wasomi.

Kuibuka kwa riwaya ya kisasa katika miaka ya 1950 na 1960 kulibadillisha hali hii pakubwa.

Aidha, kuibuka kwa riwaya za kubuni

za

usasaleo kuliibadili hali iliyokuwepo hata zaidi

(Williams 1995: 1). Gabriel Marquez kama mwanzilishi wa uandishi wa kisasaleo anafikiriwa

na wasomaji wengi wa kimagharibi kuwa mwandishi wa kifantasia. Kinyume na madai

haya, yeye mwenyewe amedai mara nyingi kuwa ni mhalisia ambaye anajaribu kuelezea

(17)

Kwa mfano, kwa mujibu wa Williams (1995), katika riwaya ya One Hundred Years of

Solitude (1980), Marquez anaelezea kuhusu wafanya kazi wa Macondo ambao wanaandaa

mgomo. Baadaye uvumi unaenezwa kwamba serikali imewaua mamia ya wafanyakazi.

Kisa hiki kimetajwa kuwa cha kifantasia kuliko vingine kwa sababu tukio la kihistoria

linapuuziliwa mbali na kuwasilishwa kama uvumi tu.

Wanahistoria na wasomi

warnekubaliana

kwamba hadithi hiyo ina ukweli wa kihistoria na

yenye ukweli kuliko zingine. Hii ni kwa sababu inarejelea mauaji ya wafanyakazi wa

mashamba ya ndizi katika sehemu iliyojulikana kama Cienaga nchini Colombia mnamo

mwaka wa 1928. Ni wazi basi kwamba riwaya hii ya Marquez ni yenye ukweli

unaoshahabiana na matukio halisi ya kihistoria (Williams 1995:6).

Williams (1995:5) akimnukuu Fuentes ambaye ni mwandishi wa kihalisiajabu, anasema

kwamba wanahistoria wa Marekani Kusini wamebadili vile ukweli umekuwa ukitazamwa.

Ukweli ulikuwa ukipuuzwa. Kwa sababu hiyo, riwaya za usasa na usasaleo za Marekani

Kusini zimetoa hali tofauti ya ukweli. Fuentes anadai kwamba ni jukumu la waandishi wa

C

riwaya wa Marekani Kusini kuuelezea 'ukweli (kivyao) wanavyouelewa'.

Katika miaka ya 1960, Julio Cortazar na carlos Fuentes walipigia swali jitihada za falsafa za

kimagharibi katika kutafuta ukweli uliofanana, lakini ulioko katika mazingira tofauti. Yaani

kulingana na wamagharibi, ukweli ni bia. Fuentes na Cortazar wanasema kwamba jitihada

ya utafutaji wa 'ukweli' kila wakati ni ya Kimagharibi na yenye kupendelea mitazamo ya

Kimagharibi.

Nchini Chile, Allende ndiye mwandishi aliyeandika kazi zake za kwanza kwa kuiga mtindo

wa uhalisiajabu

ulioturniwa

hapo awali na Marquez. Alitumia mtindo huu kuandika riwaya

(18)

9

kisiasa. Kama mtangulizi wake, anatumia uhalisiajabu kuyaangazia maswali ya nchi yake

yakiwemo siasa (Encarta Encyclopedia 2002).

Nchini Cuba kazi za Alejo Carpentier zina mchango mkubwa kwa uandishi wa kisasa.

Katika kazi zake The Kingdom of this World (1949) na The Lost Steps (1979), Carpentier

anatumia mtindo wa usasa kuelezea historia na utamaduni wa Cuba kibunifu. Waandishi

wengine kutoka Cuba waliotumia uhalisiajabu ni kama vile Miguel Angel Astrurias na Juan

Rulfo.

Mwandishi mwingine anayetumia uhalisiajabu katika kazi yake ni Mario Llosa Vargos

kutoka Peru. Riwaya moja aliyoandika kwa mtindo wa uhalisiajabu ni The Time of The Hero

(1963) inayozungumzia maisha yalivyokuwa katika chuo kimoja alichohudhuria nchi yake

ilipokuwa ikiongozwa na makadeti ikilinganishwa na uhuru uliokuwa nje ya chuo hicho.

Riwaya nyingine maarufu aliyoiandika Llosa ni Green House (1969) inayolinganisha maisha

ya jangwa la Peru na maisha katika mazingira ya kimji ya Piura (Wamitila 2002).

Salman Rushdie ni mwandishi wa riwaya wa Kiingereza, mzaliwa wa India ambaye

ametumia mtindo wa uhalisiajabu katika riwaya zake. Riwaya ya Midnight's Children

inahusu rnaendeteo.va kisiasa nchini mwake India katika miongo iliyofuata kupata uhuru

kwa nchi hiyo kutoka kwa Waingereza (Alexander 1990: 127, 138-139).

Riwaya nyingine aliyoiandika katika mtindo huu ni ile iliyojaa ubishi mwingi ya SataniC

Verses (1988). Alexander (1990) akinukuu maneno y"aRushdie alipokuwa akihojiwa kuhusu

riwaya hii Rushdie alisema:

(19)

Kwa hivyo tunaona kuwa Rushdie anapendekeza kwamba watu katika nchi yake

wasijifunge kwa kila waambiwalo kuwa ndilo kila siku bali watazame na kuona linalowafaa

wao wenyewe.

Katika bara la Afrika, wengi wa waandishi waliotumia uhalisiajabu ni wa kutoka Afrika

Magharibi. Waandishi hawa nji kama Cheney-Coker wa Sierra Leone, Okri wa Nigeria na

Kojo Laing wa Ghana (Cooper, 1998: 1).

Oka (2002:90) akiielezea riwaya ya Okri ya The Famished Road (1991) iliyomwezesha

kutuzwa tuzo ya "Booker" (1991), anasema kwamba Okri anakagua kwa upekuzi maisha

ya wananchi wa Nigeria. Anatueleza kwa undani historia ya nchi ya Nigeria kuanzia wakati

wa ukoloni hadi wakati wa uhuru na maajilio ya utawala wa kijeshi. Kuzaliwa na kufa kwa

mhusika Azaro mara tano kunasimamia miongo mitano ya utawala nchini Nigeria. Miongo

hiyo mitano ni: utawala wa kikoloni, jamhuri ya kwanza, utawala wa kijeshi, jamhuri ya pili

na hatimaye utawala wa kijeshi tena. Oka (2002:90) anasema kuwa hadithi ya uhalisiajabu

ya Azaro ni kielelezo cha hali ya umaskini na siasa za nchi ya Nigeria.

Okri anasema kwamba:

Uandishi wangu ulikuwa zao la hasira, umaskini ulionizunguka na mwelekeo mbaya wa serikali kwa mateso ya wananchi. Ulikuwa wakati wa ufisadi mwingi nchini Nigeria. Kuwa mamlakani na uongozini na kuwa na nguvu kisiasa kulimaanisha kujinyakulia pesa kwako na jamii (kabila) lako (Okri 1990:viii).

Katika fasihi ya Kiswahili, kuna waandishi watangulizi wa uwanja huu wa uandishi.

Miongoni mwao ni Topan katika tamthilia ya Aliyeonja Pepo (1973) na Hussein katika

tamthilia ya Mashetani (1971). Hawa watunzi wanakaribia kutumia mbinu ya uhalisiajabu.

Hata hivyo, ingawa waliweza kubuni hali za kiajabuajabu, walifanya hivyo kwa kuchota

(20)

11

dhanaza miungu, mashetani pepo na mengineo zimekuwepo. Hata kama hadithi zao ni

zenye uajabu, walijua kwamba kuna ujumbe fiche humo ndani.

Aliyeonja Pepo ni hadithi kuhusu jinsi maisha yanavyoendelea baada tu ya mtu kufa.

(Topan 1970:3). Hata hivyo, kiini ni kuhusu mhusika mmoja aitwaye Juma Hamisi

anayeuawa na malaika wa kifo (Ziraili) kimakosa kupitia ajali ambapo Juma anapigwa

dafrau na punda badala y~tmtu anayestahili kufa anayeitwa John Houghton. Mushkili

unatokea kwa sababu Juma Hamisi anayetoka Bagamoyo ashazikwa na ameingia peponi

mahalikuliko na furaha nyingi. Basi inamlazimu Ziraili kumrudisha duniani tena kwa kipindi

cha mwaka mmoja ndipo atakapokufa.

Hii ni kwa sababu kila mtu ana wakati wake wa kufa na huo ulikuwa wakati wa John

Houghton wa kufa. John alikuwa afe kama matokeo ya gari lake kupambana na farasi saa

nne ya usiku. (Topan 1970:6) Hatimaye inambidi Juma Hamisi hata baada ya kuonja

utamuwa peponi kurudi duniani na kungoja wakati wake. Tatizo ni kwamba kwa sababu

huko duniani watu wake washamzika, Juma hawezi kurudi katika nafsi yake tena bali

atarudi katika nafsi ya paka wa rangi ya kijivujivu na madoa ya chui (Topan 1970:20).

Kwa mujibu wa maelezo ya Kruisheer (1997), tamthilia hii inaweza kusimamia hali

ilivyokuwa nchini Tanzania katika miaka ya sabini wakati ambapo mfumo wa ujamaa

ulikuwa ukitekelezwa. Topan anaelezea hali ya nchi ya Tanzania katika miaka ya baada ya

uhuru kwa kutumia mtindo fiche.

Anwani ya Aliyeonja Pepo ni falsafa ya Ujamaa. Bamkubwa ni Nyerere (kwa sababu ndiye

rnkubwa/rnkuu) wa wafanya kazi na aliyeanzisha falsafa ya ujamaa), sera ya miaka saba

inalinganishwa na sera ya miaka tano inayoongoza nchi, malaika - Ziraili, Jiburili, Munkari

(21)

na Sirafili ni wawakilishi na watumishi wa serikali, (Kruisheer katika Kiswhaili 59, 1997, uk.

10). Peponi ni afisi za serikali, duniani ni vijiji vya ujamaa.

JumaHamisi anapojulishwa kwamba arudi duniani kwa mwili wa John Houghton anasema

kwamba yeye ana roho ya kiujamaa na maisha ya kibepari ya Uropa, yeye hawezi

kuyafikiria. Kwa mfano analalamika kwamba yeye hawezi kamwe kuishi maisha ya

kuwanyonya binadamu wenzake. (Topan 1971: 19) Anasema yeye ni Muislamu na hawezi

kufanya kazi ya kuuza bia na kukaa na mbwa kama John Houghton. Hapa tunamwona

Topan akilinganisha mfumo wa Ujamaa wa Ubepari kama inavyojidhihirisha katika sura

mbalimbali.

Katika tahakiki yao ya tamthilia ya Mashetani, Kimani na Chimerah (1999:200-201)

wanatujulisha kwamba Juma na Kitaru wameamua kucheza mchezo wa Shetani na

Binadamu ili waielewe barabara hali yao ya sasa ya kiuchumi, kisiasa na kijamii kwa jumla.

Mchezo huu unachezwa katika jukwaa karibu na mbuyu (maskani ya mashetani

inavyoaminiwa na Waswahili).

Ni uigizaji unaomfunulia msomaji, mtazamaji na msikilizaji mahusiano yaliyopo baina ya

viongozi na waongozwa, uhuru na ukoloni mamboleo, ukoloni mkongwe,

unyanyaswajijugandamiswaji wa Waafrika na mabwana wazungu na vilevile mabwana

Waafrika wenye madaraka sasa na hata wale waliokuwa na madaraka hapo mbeleni kabla

ya kupokonywa.

Shetani amesawiriwa kama kiumbe mwenye nguvu na uwezo wa kufanya mambo yasiyo ya

kawaida kama vile kujibadilisha nafsi. Shetani anasema anaweza kujigeuza ndege, kuwa

upepo na pia kuweza kurukia tawi (Hussein 1971:2).

Vilevile tamthilia za Mashetani inaashiria uhalisiajabu pale ambapo sehemu ya pili ya

(22)

13

Aidha, Kitaru anatuelezea kuhusu sifa nyingine ya uhalisiajabu anapomwambia Juma kuwa

hajui kama alikuwa amelala au alikuwa anaota na kwa kweli mtu huona ukweli zaidi

kwenyendoto kuliko katika maisha ya kweli. Hiki ni kipengele muhimu sana cha nadharia

hii.Anasema:

Juma: Ndoto gani ulikuwa unaota? Unaikumbuka?

Kitaru: (kimya) Hata sijui kama ilikuwa ndoto au ni fikira tu.

Juma: Juu ya?

Kitaru: Wewe, mimi. (Anacheka) Ajabu katika maisha ya ndoto, mtu anaona ukweli

zaidi kuliko katika maisha ya ukweli.Tena siyo ndoto tu, na katika mchezo vilevile.

Kitaru: Kwa mfano, nimekujua wewe, nimejua mimi zaidi katika ... mchezo...

C

hapana, katika ndoto? Ajabu siwezi kusema ile ilikuwa ndoto, mchezo au ukweli

(Hussein 1971:47).

Kezilahabi ni mwandishi na mwanafasihi mwingine mashuhuri anayetumia mtindo wa

usasaleo katika kazi zake.Riwaya zake maarufu Nagona (1990) na Mzingile 1991) zimezua

mijadala mirefu kati ya wasomi mbalimbali.

Mbatiah (1997) anasema kwamba kimsingi riwaya za Kezilahabi zinahusu maisha ya

Tanzania na mandhari yake ni kisiwa cha Ukerewe. Anaendelea kusema kwamba katika

Nagona na Mzingile, mwandishi anamgurisha msomaji kutoka mazingira ya kilimwengu

aliyoyazoea na kumpeleka kwenye ulimwengu wa kindoto baina ya kifo na uhai, kuwa

macho na kuwa ndotoni.

Kwa kufanya hivyo, anamshirikisha msomaji katika safari ya kifikra ya kutalii ulimwengu ili

kuujua ukweli wake. Safari hii inapindua kabisa mtazamo wa kawaida wa ulimwengu na

(23)

Wamitila (1991) anasema kwamba riwaya za Kezilahabi za awali zilihisu ulimwengu wa

kimaumbile au jinsi ulivyo, kama tuujuavyo na kama tuionavyo. Hata hivyo, Wamitila

anazionariwaya za Nagona na Mzingile kuwa za kimetafizikia - yaani zilizopita ufahamu

wetu wa ulimwengu kama ulivyo. Mwandishi anaendelea kueleza kwamba ingawa haina

haja kujichosha kwa kujiuliza kwa nini Kezilahabi akajiingiza katika udhanifu au utopia,

yeye (Wamitila) anaona kwamba picha yoyote ya kimaumbile inayopuuza utopia si picha

kamilifu. Kwa mujibu wa Wamitila (1991), tunahitaji udhanifu iIi kuwa na uhalisia. Uhalisia

wenyewe huhusisha udhanifu. Anapendekeza kwamba riwaya hizi zichunguzwe upya labda

kwa mtazamo wa kifalsafa (1991:66).

Mbali na mshabaha wa waandishi Topan (1970) na Hussein (1971) katika misingi ya

uhalisiajabu, ni muhimu kutaja kwamba uandishi wao una tofauti kubwa na ule wa

Mohamed (2001) na Wamitlla (2002). Sababu hii ni ya kifalsafa. Ingawa watangulizi wa

uhalisiajabu waliweza kubuni hali za kiajabuajabu, walifanya vile kwa kuchota kutoka kwa

malighafi ya utamaduni wa Kiafrika ambapo tunajua tangu kale dhana za miungu,

mashetani, pepo na zinginezo zimekuwepo.

Waandishi Mohamed (2001) na Wamitila (2002) wanatumia uhalisiajabu kuandika

kimakusudi kwa sababu ya kutaka kuyaangalia maswala ya kijamii kiajabu na kwa njia ya

kipekee. Topan, Hussein na Kezilahabi wanaweza kufahamika vizuri kwa kutumia nadharia

nyinginezo.Mohamed na Wamitila katika kazizao za hivi karib,uni wanafahamika vizuri zaidi

kwa kuzingatia uhalisiajabu Tunachunguza ni kwa kiasi gani Mohamed na Waamitila

wamefaulu au kutofaulu kutumia mtindo huu. katika katika Babu Alipofufuka (2001) na

(24)

15

Fani na miundo ya mengi ya mashairi haya imeathiriwa sana na yale ambayo yamekuwa yakijiri katika jamii zetu tokea wakati huo (yaani 1987 alipoanza

kukiandika kitabu hicho) na hasa hiihali ninayoiita mimi

'uhalisiamazingaombwe', hali ya ndoto si ndoto, ukweli si ukweli.

Kutokana na maneno haya, inabainika kuwa huyu mwandishi mwenyewe anajua kuwa

amebadili mtindo wake wa kuandika kazi za sanaa za hivi karibuni. Babu Alioofufuka (2001)

inapatikana katika mkabala huu ambapo mtindo mpya umetumiwa kuzungumzia maudhui

mapya.

Waandishi wa fasihi ya Kiswahili wametumia uhalisiajabu kama vile wenzao katika maeneo

mengine ya ulimwengu kama vile Marekani kusini, Afrika ya Magharibi na kwingineko ili

kuyapigia mbizi maswala muhimu yanayowakabili wao na jamii zao. Hii ni njia mpya na ya

kipekee ambayo waandishi Mohamed na Wamitila wanaamini kuwa tofauti na zile zingine

zinazoonekena kugonga mwamba katika kuyaangazia na kuyasuluhisha matatizo ya mataifa

ya Kiafrika.Hii ni kwa sababu

uhahslajabu

una mkuruba zaidi na jamii zinazoshughulikiwa.

1.4 Maswala ya utafiti

Katika kuzihakiki riwaya za Babu Alipofufuka (2001) na Bina-Adamu! (2002), tunazikabidhi

muktadha wake ambao ni kuzichunguza kwa mtazamo wa kiuhalisiajabu. Kwa hivyo ili

kuweza kushughulikia mada yetu ifaavyo, utafiti huu umeongozwa na maswali yafuatayo:

1. Je, uhalisiajabu unajitokeza vipi katika riwaya za Babu Alipofufuka na

Bina-Adamu!?

2. Ni kwa namna gani uhalisiajabu unaashiria na kuzungumzia uhalisia wa kimapokeo

katika katika riwaya hizi?

(25)

1.5 Malengo ya utafiti

Utafiti huu unalenga:

1. Kuchunguza ni vipi uhalisiajabu unajitokeza katika riwaya za Babu Alipofufuka na

Bina-Adamu!

?

2. Kubainisha ni vipi uhalisiajabu unavyoashiria uhalisia wa kimapokeo katika riwaya ya

Kiswahili. 'I

3. Kuonyesha ni vipi muktadha wa uhalisiajabu unatuwezesha kuzieleza zaidi riwaya za

Babu Alipofufuka (2000) na Bina-Adamu!

4. Kuchangia nadharia ya uhakiki wa fasihi ya Kiswahili.

1.6 Sababu za kuchagua Mada

Sababu kuu ya kuchagua mada hii ni kwamba kuna uandishi mpya katika fasihi ya Kiswahili

ambayo yanahitaji usomaji mpya. Uandishi huu umejitokeza katika riwaya za Babu

Alipofufuka (2001) na Bina-Adamu! (2002). Pengine kutungwa kwa riwaya hizi kunaashiria

kuzuka kwa mikakati ya kipekee ya kushughulikia matatizo yanayoukabili ujirani wetu.

Jambo hili linapaswa kukaguliwa.

Utafiti huu pia umechangia uhakiki wa fasihi ya Kiswahili kwa kumzingatia mwandishi

Mohamed ambaye ni mwanariwaya mkongwe na Wamitila ambaye ni mwandishi riwaya

chipukizi kwa kuchunguza kazi zao zinazofanana. Uandishi wa Mohamed na Wamitila

katika Babu Alipofufuka na Bina-Adamu! ni uasi dhidi ya jinsi ambavyo waandishi wengi

wamekuwa wakiandika kwa miongo mingi. Utafiti huu unachunguza ni kwa nini waandishi

hawa wawili wameamua kutumia mtindo huu katika kazi zao. Aidha, riwaya hizi mbili

(26)

17

Kwa hivyo, tutakuwa tukiziba pengo katika uhakiki wa fasihi ya Kiswahili. Hatimaye,

uhalisiajabu ni uandishi wenye changamoto kubwa ambapo utunzi na uhakiki hukutanika.

Yaani, ni mtindo wa kuandika na vilevile mtindo wa kuhakiki. Hii ni kwa sababu wale

waandishi wanaoandika ni hao hao wanaozungumzia kazi zao au nyinginezo

zinazoshabihiana na zao. Tumetalii na kuona ni kwa kiasi gani mambo haya yanaingiliana

na ni kwa nini Mohamed na Wamitila wameamua kutumia mtindo wa uandishi wa namna

hii.

1.7 Upeo/Mipaka ya utafiti

Uchunguzi huu umejikita katika riwaya za Kiswahili tu ambapo tumechunguza riwaya ya

Mohamed Babu Alipofufuka (2001) na ya Wamitila Bina-Adamu! (2002). Waandishi hawa

wameandika riwaya zingine lakini hizi mbili zinatosheleza mahitaji ya utafiti huu kwa

sababu kutokana na mapitio tuliyoyafanya, riwaya hizi mbili zimeonyesha mwelekeo wa

uhalisiajabu. Inawezekana kuwa na riwaya zingine, tamthilia au mashairi yanayoweza

kuhakikiwa kwa kutumia mihimili ya uhalisiajabu. Hata hivyo hatujajihusisha na hayo kwa

sababu riwaya hizi mbili zina ushahidi wa kutosha kuthibitisha madai yetu.

1.8 Misingi ya Nadharia

Nadharia tunayoamini inaafiki utafiti huu ni ya uhalisiajabu. Zamora (1995) anatueleza

kwambanadharia hii iliasisiwa mwaka wa 1925

na-

Mjerumani aliyejulikana kama Franz Roh

aliyekuwa mhakiki wa sanaa.

Franz Roh alitumia istilahi uhalisiajabu katika muktadha wa sanaa kuelezea na kuonyesha

jinsi ya kusawiri aina fulani ya uujiza uliomo kwenye uhalisi uliozoelewa na unaotokana na

(27)

Akielezeauhalisiajabu Mbatiah (2002:60) anasema kwamba:

Istilahi hii inatumiwa kuelezea mkondo wa uandishi ambapo mazingira, matendo na matukio ya kifantasia husawiriwa kwa kuiga mtindo wa uhalisia. Yaani, kwa kuyaeleza kwa njia ya moja kwa moja kana kwamba ni mambo ya kawaida. Wasanii wanaoutumia mtindo huu hudhamiria kuonyesha kuwa ingawa mambo yanayoshughulikiwa ni ya kiajabuajabu, hutokea katika maisha ya kawaida ya jamii

inayohusika. Uhalisia wa kimaajabu huusishwa zaidi na nchi zinazoendelea kutoka bara la Afrika, Marekani ya Kusini na Asia.

Wamitila (2003:274) naye anaeleza kuwa:

Dhana hii ya uhalisiajabu huhusishwa na waandishi wa Marekani ya Kusini au hata nchi inazoitwa ulimwengu wa tatu. Sifa yake kuu ni kuyaelezea matukio ya kifantansia au ya kiajabu au kichawi kwa namna ya moja kwa moja kwa namna

inayoyafanya yaonekane ya kawaida tu. Sababu hasa ya matumizi ya mtindo huu ni kuonyesha kuwa matukio ya aina hii hupatikana katika maisha ya kawaida katika jamii zinazohusika. Waandishi wanaoandika katika misingi hii hushikilia kuwa mtazamo wao wa uhalisia unawakilisha msimamo wa jamii zao. Mpaka uliopo kati ya mambo yanayoweza kupatikana katika ulimwengu halisi na yasiyowezekana

huwa mdogo sana.

Kutokana na maelezo ya Mbatiah (2002) na Wamitila (2003), uhalisiajabu ni namna fulani

ya kueleza uhalisia uliotuzunguka. Waandishi wametumia mtindo huu makusudi kwa kujua

kwamba ni njia mwafaka ya kuyapigia mbizi maswala muhimu katika jamii. Tukiichunguza

mihimili ya nadharia ya uhalisiajabu inatosheleza uhakiki wa kazi yetu. Kwa kuzingatia

mihimili muhimu ya nadharia hii tutaweza kuzielewa riwaya tunazozihakiki na hatimaye

kufanikisha malengo yetu.

Amaryll katika Michelle (1993) anatueleza kuwa uhalrslajabu una sifa na mitazamo miwili

inayokinzana lakini pia inayokubaliana. Mtazamo mmoja ni ule wenye msingi wa uhalisi

ilhali wa pili una msingi wake katika imani kuwa uajabu ni kiungo muhimu cha ulimwengu

wa kila siku. Kwa hivyo kiini cha uhalisiajabu katika fasihi huwa ni msisitizo wa ushirikiano

(28)

19

Ingawa kuna matukio ya kiajabu katika kazi zinazozingatia uhalisiajabu, yanaunganishwa

na ulimwengu 'halisi' na matukio haya yana misingi yake katika uhalisi wa kijamii, uhalisi

wa kihistoria na kisiasa.

Cooper(1998: 16) ameshughulika kwa kina na uandishi wa kiuhalisiajabu hasa kwa kutilia

maananiwaandishi wa kutoka Afrika Magharibi. Anaelezea kuwa sababu za kiuchumi,

kijamii na kisiasa ndizo zinazowachochea waandishi kutumia mtindo huu katika kazi zao.

Akiwarejelea Jameson na Anderson, Cooper (1998) anasema kwamba kuna uhusiano kati

yamaendeleo ya kibepari na kuibuka kwa uhalisiajabu.

Jambo linalodhihirika kutokana na maelezo ya wasomi tuliowarejelea ni kwamba

uhalisiajabu haujajitenga na hali halisi ya jamii zetu, bali kwa kweli umeibuka kutokana na

hali mbalimbali za hizo jamii.

Kwamuhtasari, ifuatayo ndiyo mihimili ya nadharia ya uhalisiajabu:

(i) Matokeo ya kiajabuajabu yanayoonekana ya kawaida. Pia huwa na hali za

kushangaza, kuduwaza na kuogofya.

(ii) Uhalisi na ndoto vinachanganyika. Hakuna mipaka ya uhalisi na utohalisi katika

uhalisiajabu. Labda wakati mtu anapoota ndipo yupo uhalisini na wakati yupo

uhalisini ndipo tumo ndotoni.

(iii) Mipaka ya kijamii, kitaifa na kimataifa huvunjwa. Maanake ni kuwa

wanauhalisiajabu wanajadili mambo yanayohusu ulimwengu kwa jumla bila

kujiweka katika mazingira finyu kama vile.jamii, nchi au bara moja.

(iv) Wakati na mahali vina uhusiano wa kiduara badala ya kistari. Inamaanisha

kwamba jambo linaloweza kufanyika wakati mmoja (ambalo linaweza kuwa si la

(29)

(v) Uhahalisiajabu umefungamana na sanaajadi kama vile visaasili na hadithi. Kisaasili ni hadithi zinazoeleza asili ya watu na matukio fulani.

(vi) Matukio hayafuatani kimantiki kama ilivyo kawaida. Mtindo wa baadhi ya tanzu za fasihi simulizi hutumika. Jambo hili hufanywa kwa kumpeleka msomaji kwenye safari ya hali na matukio ya kikweli na yanayowezekana. Aidha, wasanii hutumia mbinu ya ukumbukaji, mbinu rejeshi, mtiririko wa urazini na ujenzi wa wahusika wenye nafsi mbili.

(vii) Mazingira' ni sehemu muhimu sana katika aina hii ya fasihi. Wanyama, majitu, misitu mikubwa yenye giza totoro, wanyama hatari na mazimwi hurejelewa.

Vilevile mimea, mito, maziwa na bahari huchukua nafasi muhimu katika uandishi wa uhalisiajabu.

(viii) Uhalisiajabu unapinga uhusiano wa kadhia zinazotendeka katika maisha ya mtu kiutengano. Hali mbalimbali kama vile uhalisi na ndoto, kifo na uhai, usasa na

uzamani, shamba na mjini, ugeni na wenyeji tamaduni huonekana zikiingiliana (Danow

1995:74,

Cooper

1998,

Zamora

1995,

Drouart

1993

& Encarta Encyclopedia 2002).

(30)

21

1.9 Mbinu za utafiti

Utafiti wetu umejikita maktabani. Sababu ya kwanza ya kufanya hivi ni kuwa huko ndipo

tumepata vitabu vinavyohusiana na riwaya za Babu Alipofufuka (2001) na Bina-Adamu!

(2002).

Vilevile, katika maktaba tumepata vitabu vya kusoma kuhusiana na nadharia ya

uhalisiajabu tunayoitumia katika uhakiki wa kazi yetu. Aidha tumepata vitabu, majarida na

makala mengine yaliyochangia kazi hii.Tumesoma vitabu vingine vya waandishi Mohamed

na Wamitila ili kuweza kuelewa falsafa zao kuhusu uandishi wa kazi zao. Aghalabu

mazingiraanamoishi mwandishi, uhusiano wake na jamii, juhudi na mafanikio yake huathiri

mtazamo wake kuhusu maisha. Jambo hili linaweza kujulikana kwa kusoma kazi nyingine

za mwandishi. Hatimaye, tumeshawahoji waandishi wa riwaya hizi mbili. Jambo hili

limetusaidia pale inapowezekana na kuhitajika.

IIi kupata data ya kutumia katika utafiti huu, tumesoma riwaya mbili tunazozihakiki kwa

lengo la kuchunguza jinsi uhalisiajabu unavyosawiriwa.

Pili,tumesoma vitabu vinavyohusu nadharia tunayoitumia ili kuielewa na vilevile kuifaharnu

mihimili yake mahsusi. Hii ni muhimu kwa sababu vipengele hivyo ndivyo tunavyotumia

kutuongoza katika uchunguzi wetu na kutuwezesha kuelewa msingi wa kuudhibiti utafiti

huu. Kazizilizohakikiwa kwa kutumia nadharia hii pia zimesomwa ili kutupa mwanga zaidi

kwenye uhakiki wetu.

Mambo haya yote yamefanywa ili tupate data ya kutuwezesha kujibu maswali yetu na

hatimaye kufanikisha lengo letu. Baada ya kusoma riwaya zetu mbili tumepata data

ambayo imejenga uchunguzi wetu. Data ambayo tumekusanya baada ya kusoma nadharia

nayo piaimetumiwa katika ufafanuzi wa uhakiki wetu.

(31)

Hivi ni vipengele vile tunavyohisi vitafaa zaidi katika uhakiki wa kazi hii. Baada ya kusoma

riwaya zetu tunazihakiki kwa mujibu wa nadharia ya uhalisiajabu na kwa kufuata mihimili

ya uhalisiajabu tutaweza kuchunguza ikiwa vigezo hivyo vinabainika katika riwaya za Babu

Alipofufuka (2001) na Bina-Adamu! (2002). Zaidi ya hayo, tumeshirikisha maoni ya

wataalamu katika taaluma hii hasa kuhusiana na mada na nadharia ya utafiti.

1.10 Kiishilio

Katika sura ya kwanza tumetambulisha utafiti wetu unahusu nini. Mada ya utafiti

imeelezwa. Tumeelezea yale yaliyoandikwa kuhusu mada yetu ya utafiti. Maswala na

malengo ya utafiti yamegusiwa na tumetoa sababu za kuchagua mada husika. Hatimaye,

upeo wa utafiti, nadharia ya iliyotumiwa katika utafiti imefafanuliwa na pia mbinu za utafiti

zimeelezewa. Katika sura ya pili, tutashughulikia maisha ya Mohamed na Wamitila na kazi

ambazo wameziandika. Tutachunguza maendeleo ya mawazo yao katika uandishi wao

tangu waanze kuandika hadi wanapofikia kiwango cha kuandika kwa kutumia mbinu ya

uhalisiajabu. Sababu hasa ya kufanya hivi ni kuweza kupata mwanga zaidi wa kutuwezesha

kuelewa riwaya zao tunazozihakiki za Babu Alipofufuka (2001) na Bina-Adamu! (2002).

(32)

23

SURAVA PILI

2.0 Utangulizi

Katika sura ya kwanza tuliitambulisha mada ya utafiti huu ambayo ni kuchunguza jinsi

uhalisiajabu unavyojitokeza katika riwaya za Mohamed Babu Alipofufuka (2001) na

Wamitila Bina-Adamu! (2002). Maswala na malengo ya utafiti pia yalishughulikiwa.

Tumejadili yale yaliyoandikwa kuhusu mada yetu. Sababu za kuchagua mada

tunayoishughulikia zimefafanuliwa na upeo wa utafiti wetu kuelezewa. Nadharia

tunayoitumia imeelezewa na hatimaye mbinu za utafiti zimefafanuliwa.

Kama ilivyotajwa katika kiishilio cha sura ya kwanza, katika sura hii tutashughulikia historia

ya uandishi ya waandishi Mohamed na Wamitila. Katika kufanya hivyo tutaweza kuelewa

wamekuwa wakiandika kwa kutumia mitindo gani hapo awali na ni kwa nini

wameshughulikia kazi zao mahsusi tunazohakiki kwa kutumia mtindo wa uhalisiajabu.

2.1 Vipindi vya Uandishi wa Said Ahmed Mohamed

5.A.Mohamed alizaliwa Unguja (Zanzibar) mwaka wa 1947. Alipata elimu yake ya msingi na

shule ya sekondari visiwani Zanzibar.Baadaye mwaka wa 1974 alijiunga na Chuo Kikuucha

Dar-es-Salaam kusomea shahada ya B.A (Elimu) na kisha kusomea Isimu katika kiwango

cha M.A katika chuo hicho hichb. Baadaye alisomea shahada yake ya Ph.D nchini

Ujerumani. Ni mhadhiri aliyefundisha visiwani Zanzibar, Vyuo Vikuu vya Nairobi na Moi

nchini Kenya na Chuo Kikuu cha Osaka nchini Japani. Kwa sasa, ni mhadhiri katika Chuo

Kikuu cha Bayreuth nchini Ujerumani anakofundisha fasihi ya Kiafrika.

5.A. Mohamed alianza kuandika alipokuwa katika shule ya msingi mnamo miaka ya 1960.

Alitunga mashairi yaliyosomwa siku za wazee na mengine kutangazwa katika idhaa

(33)

Katika miaka hiyo hiyo ya 1960, idhaa ya Kiswahili ya BBC ilianzisha mashindano ya

uandishiwa hadithi fupi za Kiswahili.Alishiriki katika mashindano hayo. Moja kati ya hadithi

alizoandika ni 'Msiba wa Pamoja' katika Hekaya za Kuburudisha. Katika miaka ya 1970

alianza kuandika vitabu vya misemo. Vitabu hivi ni kama vile Vito vya Hekima, Methali na

Misemoya Mshangao na Milio na Tashbihi. Baadaye alianza kuandika riwaya. Riwaya yake

ya kwanza ilikuwa Asali Chungu (1978). Riwaya nyingine alizoandika ni Utengano (1980),

Dunia Mti Mkavu (1980), Kiza katika Nuru (1988), Tata za Asumini (1990), na Babu

Alipofufuka (2001).

S.A.Mohamed ni mwandishi wa mashairi

~a

tamthilia pia. Diwani za mashairi alizotunga ni Sikate Tamaa (1980), Kina cha Maisha (1984) na Jicho La Ndani (2001). Nazo tamthilia

alizotunga ni Pungwa (1988) Kivuli Kinaishi (1990), Amezidi (1995) na Kitumbua Kimeingia

Mchanga (2001).

Uandishi wa S.A. Mohamed unaweza kugawanywa katika vikundi vinne.

2.1.1 Kipindi cha uhalisia hakiki

Huu,ni uhalisia ambao huhusisha uchunguzi wa kihakiki wa hali ya kijamii, matatizo

yanayoikabili jamii hiyo na madhara yake. Uhakiki huu hata hivyo hautoi suluhisho ya

matatizo hayo mbalimbali. Uhalisia ya kihakiki unaelekea kuchukua msimamo wa ubaki

fulani wa kuendelezwa kwa hali kama ilivyo. Kwa mujibu Wamitila (2003:274), huu ndio

mojawapo ya upungufu wa uhakiki huu.

Katika kipindi hiki cha uandishi wa S.A.Mohamed kaziambazo zinaweza kuratibiwa hapa ni

kama vile Asali Chungu (1978) na Utengano (1980).

Kipindi hiki cha uandishi kinahusisha uandishi unaoshambulia maovu ya kijamii bila

(34)

25

nzuri.Hata hivyo katika hii hii jamii hutokea watu ambao huharibu utaratibu ama kwa

kukiuka maadili ya kidini na kutatiza hali nzuri inayotarajiwa katika jamii husika. S.A.

Mohamed alipokuwa akiandika kwa mtindo wa uhalisia hakiki, alikuwa akiihurumia jamii

yake. Anaihakiki jamii kwa kuzingatia jinsi jamii ya Kiislamu inavyopaswa kuongozwa kwa

sababu kuna sheria ambazo waumini hupaswa kutii na matarajio wanayopaswa kutimiza.

Hata hivyo baadhi ya wahusika ni wanafiki na hawafuati utaratibu wa jamii uliozoewa.

Uandishi wa aina hii unaweza kuchukuliwa kama mahubiri ili kuirudisha jamii kwenye

mwelekeo unaofaa. Kwa mfano katika riwaya ya Asali Chungu (1980), Zuberi anasawiriwa

kama mzee aliye na tabia ya kupenda kushiriki kimapenzi na wasichana wa umri wa binti

zake inwenyewe. Ni watu kama hawa ambao Mohamed anaodhamiria kuasa.

Upungufu wa mtindo huu wa uandishi ni kwamba utatuzi wa matatizo yaliyowakabili

wanyonge hutegemea huruma ya wenye nguvu. Ina maana kwamba anayenyanyaswa

asipohurumiwa na mnyanyasaji hali yake ya maisha haitabadilika. Wanajamii wanategemea

majaaliwa. Mtindo huu wa uandishi hauleti mapinduzi ya msingi. Jambo hili linafafanuliwa

zaidi na mwandishi wa Kirusi Maxim Gorky.

Maxim Gorky ni mmoja wa wale waliopinga mtazamo wa uhalisia hakiki na kuunga mkono

nadharia ya uhalisia wa kijamaa. Alielezea upungufu wa nadharia ya uhalisi wa kihakiki kwa

kusema:

Uhalisia hakiki ni muhimu tu kwa kadri unavyoangazia kujimudu kwa zamani na harakati za rnwanajarnu kuparnbana dhidi ya hali dhalili ...Uhalisia wa kijamaa kwa upande mwingine hupambanua kwamba maisha ni vitendo na uzalishaji ambao lengo lake ni maendeleo bila kizuizi cha uwezo wa binadamu dhidi ya nguvu za mazingira (Khaemba 1990: 14).

Mwandishi anasisitiza kwamba ingawa uhalisia hakiki,ulionyesha matatizo na uozo wa jamii

na kumulika maisha na matatizo ya mtu binafsi pamoja na mafunzo ya imani za kidini na

. .'

sheria dhalimu za nchi, haukuonyesha jinsi ya kujinasua na hali hii. Pengine hapo ndipo

(35)

-S.A.Mohamed alionakwamba wahusika wake walibaki pale pale wakiwa wamekubali nafasi

yao. Labda haya ndiyo yaliyomfanya mwandishi kubadilisha mtazamo wake na njia yake ya

uandishi.Lengo la Mohamed la kufanya hivyo likawa la kuwaumba wahusika wachochole

lakini waliokuwa na nia na ari ya kuzibadilisha hali zao kwa kupigana na utabaka na

unyanyasaji. Wahusika walio na uwezo wa kuiangalia hali yao ya maisha kama

iliyosababishwa na historia wala sio majaliwa.

2.1.2 Kioindi cha uhalisia wa kijamaa

Kwa mujibu wa Suchkov katika Khaemba (1999), nadharia ya uhalisia wa kijamaa ilizuka

pale wanajamii walipong'amua kwamba rnahttaji ya jamii yanatawaliwa na mahitaji ya

kiuchumi na wala si fikra za watu ama majaaliwa. Uhalisia wa kijamaa uliiona jamii jinsi

ilivyo na ukaonyesha mikinzano iliyomo na chanzo chake. Nadharia hii inapendekeza

namna ya kutatua matatizo ya kijamii ili kuunda jamii mpya iliyokuwa bora zaidi na ikawa

sharti kanuni za nadharia hii zizingatiwe na waandishi na wahakiki.

Baada ya kongamano la waandishi uliofanyika mnamo 1934 nchini Sovieti ya za~ani,

uhalisia wa kijamaa ulipendekezwa kuwa msingi wa fasihi ya Kisovieti. Ilipendekezwa kuwa

mwandishi wa fasihi katika Usovieti anapaswa kusema ukweli juu ya jamii bila kuficha

chochote. Katika kazi za fasihi, pia kulihitajika kuonyesha kipindi mahsusi cha kihistoria.

Lukacs (1963:91) anasisitiza umuhimu wa jambo hili kwa kuliona katika misingi ya uhalisia:

Tofauti ya uhalisia hakiki na ule wa kijarnaa umo katika mitaala iliyobobea kiitikadi.

Muhimu ni pendekezo kuwa sanaa ya kijamaa ni sanaa ya kitaifa kwa kuwa

huangazia mazingira mahsusi ya kihistoria ambamo jamii fulani imepitia (Khaemba

1999:16).

Tunaweza kusema kwamba hiki ndicho kipindi cha pili katika uandishi wa S.A.Mohamed.

Mtazamo huu hujaribu kusisitiza uwasilishi wa uhalisia unaotilia mkazo mkubwa maendeleo

(36)

27

Kaziambazo S.A.Mohamed aliandika wakati huu ni kama vile Dunia Mti Mkavu (1980),

Utengano(1980), Kiza katika Nuru (1988) na Tata za Asumini (1990).

Katikakipindi hikimwandishi anachagua kimakusudi itikadi ya kijamaa kuuelekeza uandishi

wake. Katika kufanya hivyo anadhamiria kuwa itikadi ya kijamaa inaweza kumsaidia

,

kutatua matatizo ya kijamii

"

ha

kiuchumi. Mwandishi anonyesha katika uandishi wake kuwa

matatizo yajamii yanatokana na mitafaruku ya kiuchumi, kitabaka na unyonyaji. Suluhu ya

matatizohaya ni mapinduzi yatakayoleta usawa kati ya wanajamii.

Kamunde (1983) katika tasnifu yake anashughulikia unyonge wa kiuchumi uliomo katika

tabaka la chini katika jamii. Aidha anajadili kiburi cha watukufu katika riwaya za Asali

Chungu (1978), Utengano (1980) na Dunia Mti Mkavu (1980). Kamunde anakusudia

kuwajadili wahusika mbalimbali na jinsi wanavyodhihirisha unyonge wa kiuchumi, kisiasa

na kijamii.Kutokana na uhakiki huu, uhalisia wa kijamaa unadhihirika zaidi katika riwaya ya

Dunia Mti Mkavu (1980). Katika riwaya hii, wahusika wanajaribu kuboresha hali yao ya

maishakwa kufuata mwelekeo wa uhalisia wa kijamaa.

Jambo hili linashadidiwa katika uhakiki wa Alamin Mazrui (1984) anapojadili n~mna

maudhui ya mapinduzi yanavyojitokeza katika riwaya ya Dunia Mti Mkavu kwa kutumia

nadharia ya Kimarx. Kimani Njogu (1997) anatumia nadharia ya uhalisia wa kijamaa

kujadili maudhui katika riwaya za visiwani hususan zilizotungwa na Shafi A. Shafi,

Mohamed S. Mohamed na S.A. Mohamed. Uhakiki wa Njogu unajadili utabaka, migogoro

inayotokea katika haya matabaka, chanzo cha migogoro, na kulipuka kwa mapinduzi

(37)

2.1.3 Hatua za mwanzo za uhalisiajabu

Kazi zilizoshughulikiwa na S.A. Mohamed katika kipindi hiki cha uhalisiajabu ni kama vile

Pungwa (198 ), Kivuli Kinaishi (1990 ) na Amezidi (1995).

Pungwa ni tamthilia inayohusu migogoro iliyopo baina ya ubepari na ufanyikazi.

\

Tamthilia ya Kivuli Kinaishlt(1990) inaonyesha misingi ya imla na jinsi inavyoendelezwa.

Mwandishi anasema kwamba mashiko ya uongozi wa kiimla ni ufisadi, uwongo,

ukandamizaji na upungufu wa nafsi ya mtu (Wafula 1999: 148).

Dalili za uhalisiajabu zinaonekana katika tabia ya Kirembe hasa anapofuma uongozi wake

katika miujiza, uajabu na sihiri. Tunaambiwa kwamba Bi. Kirembwe anajilinganisha na

mmoja kati ya miungu wa Rorna. Kwa kufanya hivi, anajipa uwezo na sifa za kuishi daima

dawamu. Hiki ni kielelezo cha jinsi baadhi ya viongozi wanavyohusudu nguvu za kisiasa na

kiuchumi hivi kwamba wanatamani hata kuwa miungu ili wasife na kuacha uongozi.

Wafula (1999) anasema kwamba kuzaliwa\wa Kirembwe kumefumwa katika miujiza.

Kirembwe anadai kwamba alizaliwa na tete za utawala. Miviga yote inayofanywa baada ya

kuzaliwa kwake ni dhihirisho la wajibu huu wa kirnalkia:

Nikafikishwa mafusho ... uvumba ... ubani ... mvuje; kitunguu saumu na ma]am mlangamia. Wakanifundisha mizungu. Mimi malikia wa wachawi Kirembwe niliyerembekezwa. Kirembe mnywa kinywaji cha uzima kilichoremwekewa wengu la mamba na mafuvu yawafu... Kinywaji chenye sumu isiyotupata wazee. Nani atakaye ubishi? Nani? (Mohamed 1990:42).

Maelezo haya yanapaswa kuwasadikisha Wanaginingi kwamba Bi.Kirembwe ni malkia wao

kutokana na majaliwa wasiyokuwa na uwezo juu yake. Uwezo wake unafanana na uwezo

wa kiungu tuuonao katika mhusika shetani katika tamthilia ya Mashetani (1971).

Wafula (1999: 162) anasema kwamba 'kivuli' ni tamathali inayoashiria upinzani dhidi ya

(38)

29

Madai haya yanatukumbusha jinsi S.A.Mohamed anavyomtumia mhusika Babu katika

riwaya ya Babu Alipofufuka ili kumjulisha K kwamba amefufuka na pia kumkumbusha

wajibu wake katika jamii yake ambao alikuwa ameusahau. Babu anamwambia K kwamba

ni lazima aamini kwamba wafu huweza kufufuka. Bi Kirembwe anaweza kumithilishwa na K

wa Babu Alipofufuka kama tunavyoona kwenye dondoo hii:

Bi Kirembwe: Sauti:

Bi. Kirembwe: Sauti:

Bi. Kirembwe: Sauti

Bi. Kirembwe Sauti:

Nini ni nini hicho? (kaemewa zaidi) Sauti .

Haya sa ... sau ... sauti ya nini tena? Sauti ya Kivuli

Kivuli gani? Kivuli kinachoishi!

Kivuli gani hicho, kivuli kisichokufa/

Kivuli kinachoishi, kivuli kisichoweza kufa ... kivuli cha ukweli na haki ... (Mohamed 1990:127).

S.A.Mohamed ametumia ngano, visakale na maono ambavyo ni vipengele vya uhalisiajabu.

Kwa mfano katika onyesho la kwanza tunasawiriwa Bi. Kizee akiwatambia watoto hekaya.

Kipengele cha kufungamanisha vipengee vya kijadi vya sanaa za maonyesha na mbinu za

kileo za kuigizia tarntluua .. Mohamed anaithamini ngano ya Wanaginingi kwa vile

anatufundisha sisi wa kizazi hiki kuhusu hali yetu ya maisha na jinsi ya kuirekebisha ikiwa

imeenda kombo au jinsi ya kuyaboresha maisha kwa kuyarahisisha na kuyafurahia.

Tamthilia ya Amezidi (1995) ni kazi nyingine ya S.A. Mohamed inayodhihirisha hatua za

mwanzo za uandishi wa kihalisiajabu. Huu ni mchezo wa mawazoni unaotazama matatizo

ya kijamii na ya kiuchumi katika nchi nyingi za Kiafrika za hivi leo. Hii ni sifa mojawapo ya

uhalisiajabu. Katika tamthilia hii, pia tunaona matukio ya kiajabu kama vile wahusika

wanaokufa kwa kipindupindu kwa sababu ya kula nyama ya msaada iliyooza. Ame na Zidi

(39)

walinayokuwa nayo. Wanaishi katika kasri la mawazoni, kupiga simu zisizokuwepo na

kulaliavitanda vipana visivyokuwepo.

Kimani na Chimerah (1999:75) wanasema kwamba wahusika wa kibwege si wa kihalisia

wanaoweza kutambulika na kuonekana katika mazingira yetu, bali wamebuniwa akilini

mwa mwandishi ili kuendeleza mawazo yake. Udhahania wao unatufanya tuwacheke, na

katika kuwacheka tunajicheka sisi wenyewe.

Vipengele vingine vinavyoonyesha dalili za uhalisiajabu katika tamthilia ya Amezidi ni kule

kuwa na mhusika mmoja anayechukua sura za watu mbalimbali, vicheko vinavyotumiwa

na mwandishi kuonyesha ukengeushi na vicheko visivyojulikana mahali vinatoka.

Kwa mujibu wa Wafula (1999:83), mtindo wa uandishi wa Amezidi unasawiri tarehe mpya

katika utunzi wa tamthilia ya Kiswahili. Nakubaliana naye kuhusu kauli yake na kuongeza

kwamba tarehe hii mpya haiko katika tamthiia ya Kiswahili tu bali pia kwenye riwaya ya

Kiswahili. Mohamed amethibitisha haya katika utunzi wa Pungwa, Kivuli kinaishi, Amezidi

na kwa kinaganaga zaidi katika Babu Alipofufuka.

Wamitila (2002:273) anaelezea kwamba katika miaka ya hivi karibuni mtazamo wa uhalisia

umeelekea kushambuliwa kwa sababu ya ubunifu wake. Ubunifu huu unahusiana na

majaribio ya kifasihi, kupinga kwake kwa sifa kama za kifantansia, bulinizi za kisayansi

ambazo kwa kiasi kikubwa ni sehemu ya uhalisi wa siku hizi na ugumu uliopo wa kuielezea

dhana yenyewe. Inaelekea kwamba waandishi kama S.A. Mohamed na K.W. Wamitila ni

(40)

31

2.1.4 Kipindi cha uhalisiajabu

Hikindicho kimekuwa kipindi cha hivi karibuni na pia kilele cha uandishi wa S.A. Mohamed.

Katikadibaji ya Jicho la Ndani (2001) S.A. Mohamed mwenyewe anasema:

Fani na miundo ya mengi ya mashairi haya imeathiriwa sana na yale ambayo

yamekuwa yakijiri katika jamii zetu tokea wakati huo (yaani 1987 alipoanza

kukiandika kitabu hicho) na hasahii hali ninayoiita mimi

'uhalisiamazingaombwe' hali ya ndoto si ndoto, ukweli si ukweli.

Madaihaya ya mwandishi huyu yanadhihirisha kwamba anajua yeye mwenyewe amebadili

mtindo wake wa utunzi. Anasema hali ni ile anayoiita "uhalisiamazingaombwe" yaani hali

ambayo ndoto si ndoto ukweli si ukweli. Hiki ni kigezo cha uhalisiajabu kwa sababu katika

mtindo huu ukweli na ndoto ni kama kitu kimoja. katika Mohamed katika Gromov

(2003:12) anasema kwamba, miongo ya mwisho ya karne ya ishirini ni kipindi mwafaka

cha maendeleo ya riwaya. Hii ni kwa sababu katika kipindi cha mwanzo wa utandaradhi

tumeshuhudia uporomokaji wa maadili ya kibinadamu. Mwandishi anasema kwamba

tunaishi katika ulimwengu ambao binadamu amepokwa kwa kila njia kwa maslahi ya

kiuchumi.Ni ulimwengu ambapo hakuna aliye na uhakika kuhusu sio kesho tu balihata leo.

ulimwengu ambao watu hawakumbuki jana na ulimwengu ambao mambo ambayo

hayangefikirika mwongo uliopita yanachukuliwa kama ya kawaida.

Hii ndio sababu inayowafanya waandishi wengi wa Kiswahili kushughulikia maswala ya

kilimwengu katika kazi zao wakitumia mtazamo wa kihalisiajabu kuelezea matatizo ya

ulimwengu wa leo na pia kujaribu kuchunquza ukosefu wa mantiki wa matukio ya

ulimwengu wa leo. IIi kuweza kutekeleza jukumu hili, waandishi wanatumia uhalisiajabu,

uhalisiafifi na usasaleo.

(41)

Riwaya ya Babu Alipofufuka (2001) ni kielelezo mwafaka cha uandishi wa uhalisiajabu.

Kwenye kazi hii mwandishi ametumia mtindo ambao huhusisha matukio ya ajabuajabu

ambayo hufikiriwa kama ya kawaida tu. Katika uadishi huu pia, mpangilio tuliouzoea katika

mitindo mingine ya kuwa na mwanzo, kiini cha kazi ya fasihi na hitimisho, haufuatwi bali

hadithi inaweza kuanzia mwisho ikafuatia sehemu ya katikati na kuishia na sehemu

inayopaswakuwa ya kwanza. Mipaka ya kitaifa na kimataifa huondolewa na mwandishi na

mhusikaanaweza kutoka nchi au hata bara moja na kuzuru lingine. Aidha, dhana ya wakati

katikauhalisiajabu ni ya duara wala si kistari kama ilivyozoeleka.

Kwa kutumia mtindo huu kama tulivyoeleza hapo juu, waandishi wanaoutumia wanaamini

kwamba wataweza kufanikiwa zaidi kuwasilisha ujumbe wao kuliko vile ingekuwa

wangalitumia mitindo ya kimapokeo.

2.2 Vipindi vya Uandishi wa K.W. Wamitila

Wamitila ni mwandishi, mwalimu, msomi na mhakiki wa fasihi ya Kiswahili. Katika maisha

yake ya awali alikulia Arusha nchini Tanzania. Alisomea shahada ya B.A na M.A katika Chuo

Kikuu cha Nairobi. Baadaye alisomea shahada yake ya Ph.D katika Chuo Kikuu cha

Bayreuth nchini Ujerumani. Wamitila amechapisha makala na tahakiki za fasihi ya Kiswahili

katika majarida mengi ya kitaaluma barani Afrika, Ulaya, Asia na Marekani. Ameandika

tamthilia, riwaya fupi, riwaya na mashairi. Baadhi ya vitabu vyake vilivyochapishwa ni

Wingu la Kupita (1999), Nguvu ya Sala (1999), Bina-Adamu! (2002), Pango (2003) na

Musaleo (2004). Baadhi ya kazi za Wamitila ambazo hazijachapishwa ni tamthilia ya Sumu

(42)

33

Kwa mujibu wa mazungumzo niliyokuwa nayo na mwandishi mnamo tarehe 25/6/2004,

imani yake ni kwamba maisha ya binadamu huthibitiwa na hali ya urazini na kutokuwa na

urazini ya binadamu. Jambo ambalo mwandishi ana vita nalo ni jinsi nchi za Kimagharibi

zinadhibiti na kujinufaisha na dhana kama vile utandaradhi. Hii ni kwa sababu Waafrika

ndio wanaoumia wakati ulimwengu mzima unajulikana kama 'kijiji'. Dhana kama vile

,

utandaradhi na ullrnwenqukuwa kijiji kimoja ni kwa manufaa ya Wamagharibi tu. Riwaya

yake ya Bina-Adamu inadhihirisha hayo waziwazi.

2.2.1 Hatua ya mwanzo ya uhalisiajabu

Wamitila (2002: 118) anasema kwamba kazi za kihalisiajabu zinavunja muundo wa ~

u;

a::

~ kikawaida wa utanzu kama njia ya kuzuka na istiara ya miundo ya mifumo ya kisiasa,

z

~ ~

~ kiuchumi na kitamaduni ya ulimwengu. Sababu ya kufanya hivi ni ili kufanikiwa katika

7-~

kuchunguza kile ambacho kinaitwa "ung'amuzi wa kisiasa". Kwa mfano, msomaji wa riwaya

ya Babu Alioofufuka anapaswa kuigundua siasa ya ulimwengu inayozihusu nchi za Kiafrika

na hasa nchi ya Tanzania.

Riwaya ya Wamitila Zimwi wa Leo (2002) inaonyesha kwamba, tangu mwanzo, uandishi

wake umekuwa na dalili za uhalisiajabu. Hii ni hadithi kuhusu zimwi moja ambalo linatoka

mahali kusikojulikana na kuwatokea watu waliokuwa wakiishi kwa amani na upendo.

Watu hawa ni wenye safi na wanapoona kuwa zimwi linakitamani chakula wanachokila

wanalikaribisha kwa mikono miwili.Tatizo ni kwamba zimwi hili halionekani kushiba. Inabidi

watu hawa wafanye kazi kwa bidii sana ili kuweza kutosheleza mahitaji ya zimwi hili. Kwa

upande wake zimwi, linawaona watu wanaoweza kulisaidia kujifaidi. Liliwaza:

(43)

Zimwi hili linawaza sana jinsi linavyoweza kuwashawishi hawa watu kulifanyia kazi.

Hatimaye linajiwa na wazo kwamba likiwapa Wantu nguo nyingi na zawadi watashirikiana

nala.

Zimwi hili linaendelea kutumia kutojua na wema wa watu wa jamii hii na kuanzisha mambo

mengi ambayo Wantu (kama walivyoitwa) waliyakubali bila kung'amua hatari iliyokuwepo.

Kwa kifupi, Wamitila (2002) anaeleza kifumbo jinsi wazungu walivyoingia Afrika. Waafrika

kwa moyo safi na bila kuwa na tuhuma yoyote, walivyowakaribisha. Wazungu walitumia

werna huo kuchukua mashamba ya Waafrika na hatimaye kuwatumikisha katika nchi yao

wenyewe. Mwandishi anatupitisha kwenye vipindi mbalimbali kuanzia pale zimwi linapofika

Afrika. Kwa sababu ya ile tabia yake ya 'kukaba' chakula tu bila kujali kilitoka wapi pamoja

na hila zake, Wantu walianza kuliita 'Kabaila' (Wamitila 2002: 15).

Baadaye yule Kabaila (halikuitwa zimwi tena) anabadilishiwa jina na Wantu. Hii ni kwa

sababu baada ya kuanzisha viwanda, anajipatia pesa zaidi kutokana na kodi anayowatoza

Wantu huku wao wakiendelea kuteseka tu. Aidha, kabaila anawafunza mchezo wa kamari

ili Wantu 'wajipatie pesa nyingi' lakini Kabaila ndiye anashinda karibu mara zote. Wantu

wanapoona tabia hii ya 'kubeba' na 'kuparia' Wantu wanaanza kumwita kabaila 'Bepari'.

Jambo moja linalostaajabisha kuhusu mchezo wa kamari ni kwamba kila anayeucheza na

kushinda, anabadilika kwa sura na tabia. Kiumbo, anaanza kuota mikono na vinywa vingi

kama Bepari. Kitabia anaanza kuwachukia wenzake polepole. Hawa ni wale waitwao

(44)

35

Wamitilaanasema:

Wantu waliopata pesa hawakuwa watu tena bali vizimwi vilivyokuwa na mikono

kama Bepari.Vizimwi hivyo vilikuwa tayari kuvitumia vikono vyao kuua kama Bepari

ili vipate pesa (Wamitila 2002:29).

Bepari linakuwa halifanyi kazi ila kukaa tu na kula. Hali hii inalifanya linoneane na

linashindwa na kazi yake ya awali ya kupitapita ili kuona kama Wantu wanafanya kazi.

Linawatumia vizimwi na vibepari vinavyofanana nave riale kwa ya pili kufanya hivyo. Hawa

ni vibaraka wazungu-weusi waliotumia na wazungu kufanikisha lengo lao.

Kwa sababu ya kule kutooga na kunoneana kwa Bepari, linaanza kutokwa na harufu mbaya

sana kama ya beberu. Harufu hii inatanda kila mahali kama upepo wa msimu wa rnvua.

Tangu siku hiyo Bepari linapewa jina jingine. Wantu wanaliita Beberu. Mwandishi anasema:

Hata baada ya kuondoka, mnuko ulibakia ukienea. Waliokwenda viwandani

walikumbana na mnuko wa Beberu. Hata pesa zenyewe zilikuwa na mnuko huo. Kila kitu kilikuwa kinanuka beberu (Wamitila 2002:33).

Mwandishi anataka kutujulisha kwarnba hata baada ya wakoloni kuondoka, alama zake

bado zipo. Hii ni kwa njia ya wazungu weusi/wakoloni mamboleo waliobaki. Aidha, athari

ya ukoloni bado ipo kupitia jinsi nchi nyingi za Kiafrika zimeendelea kutegemea nchi za

Kimagharibi kwa misaada ya pesa, mikopo, madawa na hata vyakula.

2.2.2 Kioindi cha uhalisiajabu

Wamitila (2002) katika Bertoncini (2004:1) anasema:

Nimeamua kuandika riwaya hii (Bina-Adamu!) hivi ili kuweza kuzungumzia suala

ambalo nahisi nisingeweza kulizungumzia kwa njia ya kawaida (kwa riwaya za

References

Related documents

Utafiti huu umebainisha kuwa dhana ya uhai na kifo cha mwanadamu katika riwaya za Euphrase KezilahabiNagona na M z ingile ni kama safari inayoashiria maisha mapya na mazuri..

Utafiti ulishughulikia maudhui ya ndoa na dini katika riwaya teule za Paradi s o , (Habwe 2005) na Kala Tufaha (Omar,2007) na kubainisha athari ya kidini, utamaduni na

Upekee: Jinsi vipengele fulani vya kazi za fasihi vinavyotofautina kwa mfano mandhari katika hadithi fupi mbalimbali kuwa tofauti ... Mwingilianomatini: Mkabala unaoshikilia kuwa

mwanamke upya kama mwenye nguvu katika unyonge wake , no mwen y e.. hekima.Haya yote yanasadifu nadharia tete ya mtafiti

Utafiti huu ulifanywa katika lugha tofauti ambayo ni ile ya Kiigembe na ulihusu makosa ya kifonolojia kwa wanafunzi wa shule za upili wanaojifunza lugha ya Kiswahili.... Utafiti

Utafiti huu ulinuia kuonyesha jinsi mbazi za kibiblia zilivyotumika katika ukuzaji wa maudhui na mtindo katika fasihi andishi ya Kiswahili.. 2 Swala

N i jambo la kushangaza sana kuwa kwa kulingana na fasihi katika Kiingereza ya wakati huu am bay oilikuwa na kazi nyingi za nathari zilizohusu juhudi za mapambano ya

Mtafiti alichochewa na hali kwamba hata kama waandishi wa v itendawili walifanya kazi kubwa kuhusu kuvikusanya, kuviainisha, kueleza sifa na dhima ya v y o, swala la matumizi ya