• No results found

Athari ya mbinu rejeshi katika hadithi fupi za Kiswahili

N/A
N/A
Protected

Academic year: 2020

Share "Athari ya mbinu rejeshi katika hadithi fupi za Kiswahili"

Copied!
104
0
0

Loading.... (view fulltext now)

Full text

(1)

~·300'"D

I

ATHARJ YA MBINU REJESHI KATIKA HADITHI FUPI ZA KISW AIDLI.

NA

LUCIA MULl MUSILI

TASNIFU HII lMETOLEWA ILl KUTOSHELEZA BAADHI YA MARITAJI YA SHAHADA YA UZAMILI KATlKA CHUO KIKUU CRA KENYATTA.

NOVEMBA 2015

(2)

---~-IKIRARI

Tasnifu hii ni kazi yangu mwenyewe na haijatolewa kwa mahitaji ya shahada katika chuo kikuu chochote.

LUCIA MULl MUSILl NAMBARl YA USAJlU: C50/CE22593111

Sahihi ~... Tarehe

yJ.u.l~.\..~

.

Tasnifu hii imetolewa kwa idhini yetu kama wasimamizi wa Chuo Kikuu cha Kenyatta.

DKT. JOSEPH N MAITARIA.

Idara ya Kiswahili na Lugha za Kiafirika

Tareheu¥i~E~

DKT. EDWIN W. MASINDE.

=-_-...::Lugha za Kiafirika

Tarehe

·

+/tj/~t£.

u

Sahihi .

(3)

TABARUKU

Naitabaruki kazi hii kwa Bwana yangu mpendwa Francis Musili Maithya, watoto wangu Ann, Margaret, Grace, Elizabeth, Everlyn, Mary, Kelvin na Victor. Mwisho naitabaruki kazi hii kwa marehemu mama yangu Josphine King'elu Nzumbu ambaye alikuwa akinipa moyo wa kuendelea na masomo. Mungu ailaze roho yake mahali perna peponi.

(4)

SHUKRANI

Natoa shukrani zangu kwa Mwenyezi Mungu ambaye amenipa uhai mpaka nikafika kiwango cha kumalizia kazi hii. Shukrani zangu pia ziwaendee wasimamizi wangu Daktari J.M Maitaria na Daktari Edwin Masinde kwa kuniongoza katika kila sura ya tasnifu hii. Waliweza kunisaidia kwa nakala nilizohitaji aidha kunip~ mwongozo wa uandishi. Sitasahau kuwashukuru wahadhiri wote katika idara ya Kiswahili na Lugha za Kiafrika. Waliweza kunipa msingi wa elimu ndio nikaweza kufika kiwango hiki. Natoa shukrani za dhati kwa Bwana yangu mpendwa Francis Musili Maithya kwa kugharamia masomo yangu. Baba yangu Daniel Nzumbu apokee shukrani kwa kuwa msingi imara wa elimu yangu kuanzia masomo ya kiwango cha msingi hadi cha upili. Watoto wangu wote nawashukuru kwa kunivumilia wakati nilikuwa katika chuo nikiendelea na masomo yangu. Kuna mambo ambayo sikuyatimiza kama mzazi wao . Mwisho natoa shurkrani zangu kwa wandani wangu katika chuo ambao bila wao kazihii haingekamilika .Tuliweza kusaidiana bega kwa bega. Baadhi ya marafiki hawa ni Sarah, Sophie, Charity, Munyao, Florence, Gecere miongoni mwa wengine.

iv

(5)

IKISIRI

Utafiti huu ulishughulikia athari ya mbinu rejeshi katika hadithi fupi za Kiswahili. Diwani zilizoshughulikiwa ni za miaka ya elfu mbili nazo ni Mwendawazimu na Hadithi Nyingine (2000) na Kunani Merikani na Hadithi Nyingine (2011). Utafiti huu umeongozwa na nadharia ya eilmumtindo. Nadharia hii ilimfaa mtafiti katika utafiti huu maana diwani hizi ambazo zimeteuliwa zimesheheni matumizi ya mtindo wa mbinu rejeshi. Utafiti huu umegawanywa katika sura nne. Sura ya kwanza ilitupa mwelekeo wa utafiti wetu. Katika sura hii tumejadili swala la utafiti, malengo ya utafiti na sababu za kuchangua mada. Pia katika sura hii tumejadili misingi ya nadharia, upeo wa mipaka na yalioandikwa kuhusu mada. Mwisho mbinu za utafiti, uteuzi wa sampuli, ukusanyaji wa data uchanganuzi wa data na uwasilishaji wa data zimeangaziwa, Sura ya pili nayo imejadili matumizi ya mbinu rejeshi katika diwani ya Mwendawazimu na hadithi Nyingine. Katika sura hii mtafiti amebainisha matumizi ya mbinu rejeshi katika diwani hii na athari ya mtindo huu. Sura ya tatu imezingatia matumizi ya mbinu rejeshi na athari yake katika diwani ya Kunani Merikani na Hadithi Nyingine. Sura ya nne ambayo ni hitimisho imekuwa muhtasari, matatizo na mapendekezo ya mtafiti. Utafiti huu unanuia kuwafaidi wahakiki wengine, wasomi na waandishi wa kazi za fasihi. Pia utafiti huu utawasaidia wahadhiri na wanafunzi wa vyuo vikuu katika kuhakiki kazi zao.

(6)

ABSTRACT

The study was to investigate effects of flashback in Kiswahili short stories. The study aimed at aspects of flashback in Kiswahili short stories. The researcher dealt with two selected Kiswahili short story books of different editors. Selected books were Mwendawazimu na Hadithi Nyingine (2000) edited by Mwenda Mbatiah and Kunani Merikani na Hadithi Nyingine(2011) edited Iribemwangi. The researcher employed stylistic theory. The theory explained the study well since the short story books selected were rich in flashbacks. This thesis comprises of four chapters. Chapter one discussed the introduction and background to the study, statement of the problem, objectives, research questions, the theories used, the scope of the study and literature review. Lastly it discussed about the methods of the research. Chapter two dealt with the history of short stories and development up to date. Chapter three discussed about the effects of flashback in Mwendawazimu na Hadithi Nyingine and Kunani Merikani na Hadithi Nyingine. The researcher tried to show flashbacks used in these books and how they bring effect to characters. Chapter three discussed about flashback in Mwendawazimu na Hadithi Nyingine and Kunani Merekani na Hadithi Nyingine and how they affect settings. Different flashbacks were also analysed.Chapter four gave the summary of the research, the findings of the research, the problem encountered and the proposals for the future study. This research intends to benefit other researchers, learners and literature writers. It will also go a long way in assisting lecturers

(7)

MAELEZO YAISTILAHI MUHIMU

Dhamira: Kiini chajambo au habari iliyosimuliwa ama kuandikwa.

Hadithi Fupi: Hii ni hadithi ambayo inashughulikia suala fulani kwa muhtasari na huwa aghalabu na mhusika mmoja anayejitokeza ingawa hakuzwi kama ilivyo katika novela au riwaya.

Matini: Kifungu cha maandishi au taarifa inayojisimamia katika kueleza dhana

Mbinu rejeshi: Ni mbinu anayoitumia mwandishi kuyaeleza matukio yaliyotokea wakati wa nyuma ya wakati wa hadithi

Msuko: Ni mpangilio wa matukio yanayopatikana katika hadithi na huhusisha matendo ya nguli najinsi yanavyoathiri wahusika wengine.

Nadharia: Ni maelezo au mwongozo uliopagwa ili kusaidia kueleza, kutatua au kutekeleza jambo.

(8)

YALIYOMO IKIRARI ii TABARUKU iii SHUKRANI iv IKISIRI v ABSTRACT vi

MAELEZO Y A ISTILAHI MUHIMU vii

Y ALIYOMO viii

SURA YA KWANZA : 1

1.0UTANGULIZI 1

1.4 Sababu Za Kuchangua Mada 4

1.6 Yaliyoandikwa Kuhusu Mada 15

1.7.1 Muundo Wa Utafiti 22

1.7.2 Mahali Pa Utafiti 22

1.7.3 Uteuzi Wa Sampuli 22

1.7.4 Ukusanyaji Wa Data 24

1.7.5 Uchanganuzi Wa Data 24

1.7.6 Uwasiiishaji WaMatokeo 25

1.8 HITIMISHO 25

ATHARI YA MBINU REJESHI KATlKA UWASILSHAJl WA MAUDHUI 26

2.0 UTANGULIZI 26

2.1 Mchango Wa Mbinu Rejeshi Katika Usawiri Wa Wahusika Na Uwasilishaji Wa

Maudhui 26

2.1.1 Mwendawazirnu-Rose Shake 28

2.1.2 Kunani Merikani - Iribemwangi 30

2.k1 Korti Ya Kishenzi - David Maillu 35

2.1.4 Siri- Stephen Munyasi 39

2.1.5 Walicheka Kicheko - John Habwe 42

2.1.6 Mbio Za Sakafuni - O. Ong'utu 44

2.1.7 Mboni La Jicho -Kyallo Wamitilla 47

2.1.8 Kwa Nini - Hassan Ali 51

2.2 Hitimisho 55

SURA YA TATU 56

ATHARI YA MANDHARI NA UWASILlSHAJl WA MAUDHU 56

3.1.1 Kunani Merkani -Iribemwangi 57

3.1. 2 Mwendawazimu - Rose Shake 60

3.1.3 Mja Mja- Rabbecca Nandwa 62

(9)

3.1.4 Mtego Wa Panya - Hamisi Babusa 66

3.1.5 Mboni Ya Jicho - Kyalo Wamitila 69

3.1.6 Mapenzi Chungu - Betty Kiruja 71

3.1.7 Jitu La Kisasa-R. M Wafula 74

3.1.9 Maji Aliyavulia Nguo!- Assumpta Mulila-Matei 80

3.2Hitimisho 83

SURA YA NNE 85

HITIMISHO 85

4.0 Utangulizi 85~

4.1 Muhtasari , 85~

4.2 Matokeo Ya Utafiti 871

Umuhimu Wa Matokeo Ya Utafiti 90

Changamoto Zilizoathiri Utafiti 90

Mapendekezo

21

Marejeleo 92

ix

(10)

SURA YA KWANZA

1.0 UTANGULIZI

Hadithi ni mfululizo wa matukio kwa kuzingatia mfuatano au mpangilio

wa kiwakati. Hadithi ni kipengele muhimu sana katika utanzu wa fasihi.

Katika kufafanua hadithi fupi tuliyoisoma inatulazimu kuyachukua matukio

yaliyomo na kuyapanga kiwakati. (Wamitila, 2002). Katika hadithi fupi za

Kiswahili, hoja kuu ni kuwasilisha ujumbe kwa kutumia vipengele

mbalimbali vya kimtindo. Kipengele kilichoshughulikwa ni mbinu rejeshi

na athari yake katika hadithi fupi za Kiswahili. Mbinu rejeshi ni kipengele

cha mtindo kinachotumiwa na mtunzi wa kazi ya kisanaa kwa kurejerea

mambo yaliyokwisha kusimuliwa awali kupitia mpangilio wa matukio ya

kazi au uzungumzi nafsia wa wahusika.

Katika utafiti huu kazi za wahariri wawili tofauti zimeangaziwa. Mwenda

Mbatiah amehariri diwani yaMwendawazimu na Hadithi Nyingine (2000) naye Iribemwangi amehariri diwani ya Kunani Merikani na Hadithi Nyingine (2011). Hata hivyo Kuna kazi zingine za fasihi ambazo waandishi

hawa wamehariri. Kwa mfano Iribemwangi amehariri diwani ya Alidhani Kapata na Hadithi Nyingine (2007). Naye Mwenda Mbatiah, amehariri kitabu

cha Kurudi Nyumbani na Hadithi Nyingine (2007) miongoni mwa kazi zingine.

(11)

Diwani za Mwendawazimu na Hadithi Nyingine na Kunani Merikani na

Hadithi Nyingine ni kazi za fasihi ambazo hazijafanyiwa utafiti

tukiangazia kipengele cha mbinu rejeshi katika hadithi fupi za Kiswahili. Hivyo kulikuwa na haja ya kushughulikia kazi hizi kwa upana.

Hata hivyo, uhakiki umefanywa kuhusu hadithi fupi za kiswahili kwa jumla. Uhakiki ambao umefanywa unalenga wahusika, ,mtindo, mandhari

na usimulizi. Utafiti wetu umekuwa tofauti kwa sababu umejikita katika kuchunguza athari ya mbinu rejeshi katika kazi mbili teule za wahariri tofauti ambao ni Mwenda Mbatiah na Iribemwangi.

1.1Swala la utafiti

Mbinu rejeshi ni kipengele muhimu sana cha mtindo katika kazi ya fasihi. Fasihi ni sanaa ambayo huitaji lugha ili kuyasimulia maisha ya wanajamii kwa jumla. Hivyo matumizi ya lugha katika kazi ya fasihi huwa moja kwa moja na wakati mwingine matumizi haya huwa fiche. Kuna mitindo mbalimbali ambayo mtunzi wa kazi ya fasihi anaweza kutumia ili kuwasilisha ujumbe. Mtindo wa mbinu rejeshi ni mojawapo wa mbinu zinazotumiwa na watunzi wa kazi ya fasihi. Hivyo basi utafiti

huu umeshughulikia athari ya mbinu rejeshi katika hadithi fupi za Kiswahili.

Utafiti huu umechunguza athari ya mtindo wa mbinu rejeshi katika kazi

(12)

mbili za fasihi ambazo zimehaririwa na wahariri wawili tofauti. Diwani

ya Mwendawazimu na Hadithi Nyingine na Diwani ya Kunani Merikani

na Hadithi Nyingine. Mtindo wa mbinu rejeshi ambao umetumiwa na

wahariri hawa wawili ulichunguzwa. Ujumbe ambao uliweza kuwasilishwa na

mtindo huu uliangaziwa pia. Aidha, utafiti huu umebainisha na kuchanganua

mbinu rejeshi kwa lengo la kuonyesha iwapo imefanikisha malengo ya

mtunzi kisanaa. Vilevile mtindo huu umeonyesha kama malengo ya mtafiti

yamefanikishwa.

Kwa vile kuna pengo katika mtindo wa mbinu rejeshi ambao unatumiwa

na watunzi wa kazi ya fasihi, katika utafiti huu tuliweza kuangazia huu

mtindo na kujua athari yake katika hadithi fupi za kiswahili hivyo basi

kujaza pengo hila kupitia utafiti wetu.

1.2 Maswali ya utafiti

Utafiti huu umeongozwa na maswali yafuatayo:

1. Ni aina zipi za mbinu rejeshi zinazopatikana katika diwani teule za

Kiswahili?

2. Mbinu rejeshi imeathiri vipi msuko wa maudhui katika diwani teule

za Kiswahili?

3. Mbinu rejeshi imetumiwa vipi kuwasawiri wahusika katika diwani teule

za Kiswahili?

(13)

1.3 Malengo ya utafiti

Utafiti huu uliongozwa na malengo yafuatayo.

1. Kubainisha aina mbalimbali za mbinu rejeshi zinazopatikana katika

diwani teule za Kiswahili.

2. Kuonyesha vile mbinu rejeshi imeathiri msuko wa maudhui katika diwani za teule za kiswahili.

3. Kuonyesha vile mbinu rejeshi imewasawiri wahusika katika diwani teule

za Kiswahili.

1.4 Sababu za kuchangua mada

Sababu ya mtafiti kushughulikia mada hii ilitokana na hoja nne kuu.

Kwanza swala hili halijashughulikiwa kwa upana na watafiti wengine hivyo

kuna pengo ambalo linahitaji kujazwa. Ingawa mtafiti alihusika na mtindo

mmoja tu wa mbinu rejeshi katika hadithi fupi za Kiswahili, mtindo huu

umeonyesha vile una uwezo wa kuendeleza kazi ya fasihi kwa wasomi na

wasanii mbalimbali tukiangazia hadithi fupi za Kiswahili. Pili utafiti huu

umechunguza kazi za wahariri wawili na kuangalia kama wametumia mtindo

wa mbinu rejeshi katika vitabu vya hadithi fupi za Kiswahili. Diwani hizi

ni Mwendawazimu na Hadithi Nyingine (2000) na Kunani Merikani na

Hadithi Nyingine (2011). Tatu ni maoni yetu kuwa utafiti huu utawasaidia

wahakiki wa kazi za fasihi kwa kuchunguza mitindo inayotumiwa na

waandishi wa hadithi fupi za kiswahili. Nne utafiti huu utakuwa na

(14)

manufaa kwa wasomi na wapenzi wa lugha ya Kiswahili kwa jumla.

1.5Upeowa Mipaka ya Utafiti

Utafiti huu umeshughulikia diwani mbili za hadithi fupi ambazo ni

Mwendawazimu na Hadithi Nyingine ya Mwenda Mbatiah na Kunani

Merikani na Hadithi Nyingine ya Iribemwangi. Kazi hizi mbili zimeteuliwa

kwa sababu data inayopatikana katika diwani hizi ilitarajiwa kutosheleza

mahitaji ya utafiti huu. Kuna kazi nyingi za kisanii ambazo zimeandikwa

na watunzi wengi kama vile riwaya, tamthilia, ushairi na hadithi fupi.

Diwani hizi mbili zimeteuliwa kwa sababu ya ufaranguzi wa kimtindo

uliotumika humu wa kutumia mtindo wa mbinu rejeshi.

1.5.1 Nadharia ya Elimumtindo

Nadharia ni maelezo ya jambo kufungamana na vigezo vilivyowekwa au

vinavyozalika kutokana na majarimbio ya jambo hilo. Swala la utafiti ndilo

linalomwongoza mtafiti kutumia nadharia ifaayo.

Nadharia hii iliweza kutekeleza swala la mtafiti vyema. Mtafiti alichunguza

athari ya mbinu rejeshi katika diwani mbili za hadithi fupi za Kiswahili.

Matumizi ya mbinu rejeshi yamechanganuliwa kwa kuzingatia mihimili ya

nadharia ya elimumtindo.

Mwasisi wa nadharia hii rn Buffon (1930) ambaye kwa mawazo yake alidai

(15)

kuwa mtindo ni mtu mwenyewe kumaanisha jinsi mtu anavyotumia lugha

kupitisha ujumbe wake. Mawazo yake ni kuwa kazi ya fasihi hudumu kupitia

mtindo wake na mtindo huo ni mtu mwenyewe. Hivyo mtindo huweza

kumtambulisha mtunzi wa kazi yoyote ya fasihi. Aidha mtindo ndio kifaa cha

pekee ambacho mtunzi ana uwezo wa kukimiliki hivyo akasema kuwa

tunaweza kusema huu ni mtindo wa mtunzi fulani. Kwa mfano tunaposema mtindo wa M.S Mohamed, inamaanisha kuwa ametumia lugha yake. M.S

Mohamed ametumia jazada na sitiari katika utunzi wake kwa upana naye

Shafi Adam Shafi ameengemea kwa upande wa wepesi wa lugha na

tamadhali katika kazi zake (Wamitila, 2003). Watunzi hawa wametumia vipengele tofauti vya mtindo ili kuwasilisha ujumbe wao.

Crystal na Davy (1969) wametoa maoni kuhusu mtindo. Wanaeleza mtindo

kwa kutumia njia nne kuu. Kwanza wanasema mtindo ni tabia ya mtu kupitia

matumizi yake ya lugha. Hapa wana maana kuwa namna mtu anavyotumia

lugha kuwasilisha ujumbe wake. Crystal na Davy wanaendelea kudai kuwa

mtindo ni tabia ya mtu binafsi kuhusu matumizi yake ya lugha. Matumizi haya

ya lugha huweza kudhihirisha hulka ya mtunzi. Mfano mzuri ni mtindo wa watunzi mbalimbali kama vile Shakespheare na Jacob Joyce. Tunaposema

mtindo wa Shakespheare tunamaanisha jinsi mtunzi ametumia lugha yake.

Vilevile tunaposema mtindo wa Jacob Joyce tuna maana kuwa mtunzi huyu

ametumia lugha yake. Pili wahakiki hawa wanaeleza mtindo kama namna

6

(16)

kikundi cha watu wanavyotumia lugha katika kipindi fulani, yaani tabia za

matumizi ya lugha ambazo zinashughulikiwa na jamii fulani. Kwa mfano

mtindo wa mashairi ya kina Augustan au mtindo wa mashairi ya kishujaa ya

kingereza. Aidha wanasema kuwa mtindo ni tabia ya kueleza mambo kama

vile matumizi mwafaka ya lugha katika mazingira. Mwisho wanasema kuwa

mtindo umekuwa ukihusishwa na fasihi kama sifa bora na yenye maandishi

yenye mapambo.

Naye Leech (1969) anatilia mkazo kuwa nadharia ya mtindo inalenga

matumizi ya lugha ambayo ndio huibua dhamira za mwandishi. Kipengele muhimu alichokizungumzia ni lugha ambayo inamsadia mwandishi kutoa

dhamira yake kwa wasomaji au wasikilizaji.

Naye Epstein (1978) anasema mtindo ni mapambo yanayojitokeza katika kazi

nzuri. Epstein anadai kuwa mtindo ni elementi ya lazima katika mawasiliano

ya binadamu. Tabia ya binadamu huonekana kupitia mtindo wake kwa njia

tofauti hivyo basi mtindo wa mtu ndio unaweza kumtofautisha binadamu

na wengine. Mhakiki huyu anayaunga maoni ya Buffon kwa kudai kuwa

mtindo ni mtu.

Naye Diyann (1976:81) anasema kuwa mtindo ni jinsi mwandishi anavyopanga

maneno na sentensi katika kazi yake. Aidha, anasema mtindo ndicho

kitambulisho ambacho kina uwezo wa kumtambulisha mtunzi kupitia

maandishi yake ya kipekee.

(17)

Scot (1925) ametoa mawazo yake kuhusu mbinu rejeshi. Hiki ni kipengele

cha mtindo ambacho hutumiwa na waandishi wa kazi ya fasihi. Maoni yake ni

kuwa mwandishi hutumia mbinu rjeshi kwa sababu kadhaa. Kwanza huwa

anataka kuwasilisha kina cha ujumbe katika kazi ya fasihi. Vilevile mtunzi

huonyesha kazi zilizopendwa ambazo zimetiliwa chuku au zinazosisimua.

Aidha anasema kuwa mbinu rejeshi huibua taharuki kwa kuzingatia vipengele

vya hadithi fupi kama vile wahusika. Amesisitiza kuwa mbinu rejeshi huweza

kumsawiri mhusika kwa kuangalia tabia yake.

Kimani Njogu na Dorothy (1996) wanasema mtindo ni namna mwandishi

au msimulizi anavyounda kazi yake. Wahakiki hawa wamedai kuwa

mtindo ni mazoea ya msanii vile yanajitokeza katika kazi yake. Maoni

yao ni kuwa mtindo waweza kujitokeza katika kazi kadhaa za mwandishi

mmoja au kazi za wasanii wa kipindi kimoja cha historia. Hivyo basi

wakasema mtindo hujitokeza katika fani na maudhui. Haya yanapatikana

katika tamathali za usemi, taswira, ujengaji wa wahusika, mandhari au

uteuzi wa msanii. Mwisho wanasisitiza kwamba mtindo si mali ya msanii

fulani peke yake. Mtindo anaoutumia msanii mmoja waweza kutumiwa na

msanii mwingine.

Kimani na Chimera (1999) wanasema kuwa mtindo ni ufundi wa kupanga

kupangua. Vilevile wanaeleza kuwa mtindo ni ujuzi wa kujieleza. Maoni

yao ni kuwa mtindo huwa na vipengele vyake kama vile jazada, taashira,

(18)

tashbihi, tasfida, taswira, taharuki, mbinu rejeshi na viangaza mbele.

Wahakiki hawa wamesisitiza kuwa mtindo hutumiwa kupeleka mbele

maudhui na dhamira pamoja na kusanifu kazi nzima ili ufasaha ujitokee.

Kwa mujibu wao mtindo ndio unaomtofautisha fanani na mwingine hivyo

basi wakasema ni mseto wa fani na maudhui. Maoni yao kuwa, mbinu

rejeshi ni mtindo wa kisanaa ambao unatumiwa na rntunzi kwa kurudia

mambo yaliyokwisha simuliwa awali kupitia mpangilio wa matukio ya

kazi au uzungumzi nafsia wa wahusika. Wanasema kwamba mbinu hii ni

kinyume cha mbinu ya kiangaza mbele ambayo badala ya kubashiria

yaliyotokea baadaye, hurejelea mambo yaliyopita.

Naye Wamitila (2002) anasema kwamba mbinu rejeshi hutokea pale

ambapo matukio hutokea kabla ya sasa hadithi inapowasilishwa.

Saundra na Richard (2004) wanasema mtindo ni matokeo ya vile mtunzi

huchangua na kupanga maneno na sentensi. Mawazo yake ni kuwa watu huchangua maneno mbalimbali ili kuwasilisha ujumbe wao na kila mtu ana

mtindo wake mwenyewe. Hivyo kila mtu hutumia mtindo wake kuwasilisha

ujumbe wake kulingana na hali. Mtindo wa mbinu rejeshi ni kipengele cha

lugha ambacho kinaaminika kuwa kinaibua mawasiliano katika hadithi. Hata

hivyo maoni ya wahakiki hawa ni kuwa ikiwa mtu ana ujumbe unaofaa wakati

fulani, na msikilizaji awe amefutwa na ujumbe huo yale atakayewasilisha

huenda yakapotea ikiwa mtindo wake haufai.

(19)

Leech (2008) anadai kuwa mtindo ni matumizi ya lugha kulingana na

mabandiliko ya hali. Kwa mfano, hali ya sehemu za isimu zinazohusiana na maandishi ambayo yana vigezo vyenye utaratibu. Leech amesisitiza kuwa

kuna uwezekano wa kutofautisha elimu mtindo ya jumla na elimu mtindo ya

fasihi. Tofauti iliopo mitindo hii ni kupitia maandishi. Maoni ya Leech ni

kuwa mtindo unaweza kujulikana kupitia mwandishi na vile alinuia kueleza

wazo lake kupitia maandishi yake. Hivyo, mtindo ni jinsi lugha inavyotumiwa

tukiangazia vigezo vya lugha. Anaeleza umuhimu wa mtindo katika kazi ya

fasihi. Kwanza mtindo husaidia wasomi na wasanii kuwa na uwezo wa kukumbali kazi ya fasihi. Pili husaidia kufunza vikundi vidogo na kuwa na

uwezo wa kufikia kiwango cha elimu vizuri. Tatu mtindo husaidia kupata ujuzi

wa isimu unaojitajika katikajamii. Mwisho husaidiajamii kuwa na uwezo wa

kupata ujumbe wowote katika maeneo mengine.

Wamitila (2003:191-192) anasema kwamba mtindo nijumla ya mbinu au sifa

zinazomwezesha mwandishi kuwasilisha ujumbe wake. Anasema kuwa

mtindo huelezajinsi mwandishi anavyounda kazi yake. Mawazo ya Wamitila

ni kuwa mwandishi anapotumia mtindo fulani anajitambulisha kwa wasomi

na wanaweza kutambua kazi ya mtunzi fulani kupitia kuisoma tu. Anaendelea

kusema kwamba mtindo unaweza kujitokeza kwenye kazi kadhaa za

mwandishi mmoja au pia kwa waandishi wa sehemu fulani au kipindi cha

kihistoria. Wamitila anasisitiza ya kwamba fani peke yake haitoshi

(20)

kumtambulisha msanii hivyo basi akasema kuwa mtindo huweza kujitokeza

kwenye fani na maudhui ya mwandishi fulani. IIi tuweze kuangalia mtindo

ambao ameutmia mtunzi, alisema ya kwamba ni vyema kuzingatia vielekezi

mbalimbali. Vielekezi hivi ni kama; matumizi ya lugha, mpangilio wa matukio,

taswira, tamathali za usemi, ujezi au usawiri wa wahusika, mandhari mpangilio

wa matukio, uteuzi wa msamiati miongoni mwa vielekezi vingine. Wamitila

amezungumzia muundowa kazi ya asihi ambapo tunatoa kauli ya mwandishi

kutumia wahusika changamano, kutmia lugha nyepesi, ana tamathali nzito na

usimulizi wa kuvutia.

Leech (2008) anadai kuwa mtindo ni matumizi ya lugha kulingana na

mabandiliko ya hali. Kwa mfano hali ya sehemu za isimu zinazohusiana

na maandishi ambayo yana vigezo vyenye utaratibu.

Wafula na Njogu (2007:97) wametoa mawazo yao kuhusu nadharia ya mtindo.

Maoni yao ni kuwa mtindo huelezwa kwa kuainishwa na madhumuni ya

msanii. Madhumuni wanayaeleza kama dhamira hivyo basi wakasema

mtindo ni jinsi dhamira zinavyowasilishwa. Kauli hii inachukuliwa kuwa

wazo huota katika fikra za mwanasanaa au msemaji yeyote wa kifasihi.

Wadhifa wa mwanasanaa ni kuainisha na kutumia lugha inayofaa kulieleza

wazo hilo. Wanamtindo huchukua lugha kama vazi la fikra. Maoni ya

wahakiki hawa ni kwamba fikra hizi zilielea angani bila umbo au muundo

wowote. Ilibidi fikra hizi zivishwe nguo yaani zielezwe kimaneno ili zipate

(21)

sura maalum. Imani hii ilichukuliwa kwamba kuna maudhui na mtindo na

kwamba maudhui yanapasa kuwasilishwa katika mtindo unaofikiana nayo.

Senkoro (2011) anasema mtindo katika kazi ya fasihi ni ile namna ambayo

msanii hutunga kazi hiyo na kuipa sura ambayo kifani na maudhui huainisha

kanuni au kaida zilizofuatwa kama ni za mapokeo au za kipekee.

Charles na Mary, (2005) wametoa mchango wao kuhusu mbinu rejeshi na

kusema kuwa ni sehemu ya kazi ya fasihi ambayo inaleta mfuatano wa

matukio. Iii kuwe na uhusiano wa hayo matukio kutoka mwanzo wa kazi ya

fasihi, waandishi hutumia mbinu rejeshi kuonyesha kile kilimpa motisha

mhusika au kurudia tukio fulani lililopita kuhusu mhusika.

Wamitila, (2008:153-157) anazungumzia mtindo wa anakroni au urejeshi

ambapo mkondo asilia wa matukio umekiukwa. Anaeleza aina mbili za

anakroni yaani mbinu rejeshi na mbinu elekezi. Wamitila anasema kwamba

mbinu hizi mbili zinaweza kupimwa kwa kuangalia mfiko wa upana wake.

Mhakiki huyu wa fasihi anasema kuwa mbinu rejeshi hutokea pale ambapo

matukio yaliyotokea kabla sasa ya hadithi yanapowasilsihwa. Wamitla

anasema kuwa kuna aina mbalimbali za mbinu rejeshi.

Nazo ni;

1. Mbinu rejeshi ya ukamilishaji: Hapa ni pale mtunzi hutumia mbinu

rejeshi kurejelea. maelezo au tukio ili kukamilisha au kulijaza pengo

(22)

fulani katika usimulizi na ambalo msomaji wa kazi inayohusika anahisi

anaposoma maelezo au tukio linalorejelewa.

2. Mbinu rejeshi ya nje: Hii ni mbinu ambapo urejeshi unaotokea

unapatikana nje ya pale matini au hadithi kiwakati inayohusika

inapoanzia.

3. Mbinu rejeshi ya urudiaji: Hapa tukio linalorejelewa huweza kuwa nt

tukio lililosimuliwa kabla na kwa hivyo linarudiwa.

4. Mbinu rejeshi ya kibinafsi: Hii ni mbinu ambayo inamhusu mhusika

kibinafsi. Mbinu rejeshi ya aina hii hutokea pale ambapo maelezo ya

ndoto au kumbukumbu zinazomhusu mhusika binafsi zinarejelewa.

Hapa kazi za fasihi zenye mielekeo ya kisaikolojia uangaziwa.

5. Mbinu rejeshi ya ndani: Hapa urejeshi unaohusika haupo nje ya wakati

unaondokezwa na mwanzo wa matini au kazi ya fasihi inayohusika.

6. Mbinu rejeshi mseto: Hii ni aina ya mbinu rejeshi ambapo wakati

unaohusika unaanza kabla ya hadithi yenyewe lakini unaelekea kwenye

wakati wa hadithi kuingia kwenye hadithi kuu yenyewe.

7. Mbinu rejeshi ya muktadha wa karibu: Mbinu rejeshi hii urejelea

mhusika, au unaozunguka mhusika au tukio fulani.

8. Mbinu rejeshi muktadha mpana: Mbinu hii inatokea wakati kile

kinarejelewa kiko nje ya ulimwengu wa mhusika au tukio fulani.

9. Mbinu rejeshi ndani ya mbinu rejeshi: Urejeshi wa aina hii unafuata

misingi sawa na mchezo ndani ya mchezo. Katika mbinu rejeshi

(23)

iliyopo kuu, panakuwako na rnbinu nyingine ndani yake, inaweza

ikawa mbinu rejeshi moja au zikawa mbinu rejeshi kadha na kwa

njia hii kuunda aina ya ngazi katika kiwango cha usimulizi.

10. Mbinu rejeshi za kikufu: Dhana hii hutumika kuelezea hali katika

matini au kazi ya kifasihi. Huwa kuna matumizi ya mbinu rejeshi

kadha ambazo zinaunganishwa kwa namna ya kuunda mkufu fulani. Hali hii hutokea pale ambapo hadithi inarejelea tukio fulani kisha tukio

hilo nalo likarejelea matukio mengine kadha.

Wanamtindo wanasisitiza umuhimu wa lugha kama chombo kinachosaidia

katika kuelewa ujumbe au maudhui kwa hivyo kama hakuna lugha hakuna

fasihi. Wanaeleza kuwa vipengele vya isimu hutumika katika kueleza namna

ambavyo lugha hutumika katika kazi ya fasihi. Mbinu rejeshi kipengele cha

mtindo kinachutumiwa na watunzi wa kazi ya fasihi. Kipengele hiki ndicho

muhimu sana katika utafiti huu maana ndicho kitakachotumika kuongoza

utafiti wetu.

Nadharia ya elimumtindo ilitusaidia kuchuguza athari ya mbinu rejeshi katika

hadithi fupi za Kiswahili. Kwa mujibu wa nadharia hii, tuliangazia mtindo wa

mbinu rejeshi na vile mwandishi anaweza kujenga ufanisi wa kazi yake

akitumia lugha tukiangazia kipengele cha mbinu rejeshi.

Kutokana na maoni ya wataalamu hawa, tumeweza kubainisha mihimili ya

kimtindo tukirejelea kipengele cha mbinu rejeshi. Mihimili minne iliweza

(24)

kubainishwa kama ifuatayo:

1. Matumizi ya mbinu rejeshi huonyesha kile kilimpa mhusika motisha katika hadithi. Muhimili huu ulitusaidia kuangalia kilichomsukuma

mhandishi kutunga kazi yake namna alivyoitunga.

2. Mbinu rejeshi hurudia tukio fulani lililopita kuhusu mhusika. Muhimili

huu ulitusaidia kuchunguza matukio yaliyorudiwa pamoja na athari

yake katika kuendeleza hadithi fupi.

3. Mbinu rejeshi huibua taharuki kwa kuzingatia vipengele vya hadithi

fupi. Muhimili huu ulitusaindia kuangalia athari ya taharuki katika

uwasilishaji ujumbe katika hadithi fupi

4. Matumizi ya mbinu rejeshi uwasilisha dhamira ya mtunzi katika

hadithi. Muhimili huu ulitusaindia kuangalia dhamira ya mtunzi

ilivyowasilishwa pamoja na athari yake.

1.6 Yaliyoandikwa Kuhusu Mada

Baadhi ya wahakiki ambao wameshughulikia tafiti za hadithi fupi na

kuonyesha maswala mbalimbali yanayojitokeza katika hadithi fupi za kiswahili

ni wafuatao.

King'ala, (1985) anadai kuwa mwandishi huwezeshwa na matumizi ya lugha

kuwasilisha mawazo yake kwa msomaji wake. Anasema kuwa matumizi ya

lugha ya mwandishi yaweza kuwa yanavutia au yakawa dufu, ambayo

hayawatii moyo wasomaji. Rata yote hutengemea ufundi wa mwandishi katika

(25)

kutumia lugha. Hivyo ni matumizi ya lugha ambayo hufanya ujumbe wa

mwandishi ueleweke vyema au usieleweke na msomaji. Utafiti wa King'ala ni tofauti na wetu. Ameangazia matumizi ya lugha kwa jumla na vile yanaweza

kuwavutia wsomaji au yakawa hayawavuti wasomaji. Utafiti wetu umeangazia

kipengele cha mbinu rejeshi na vile kimeweza kuibua athari kwa msomaji,

mhusika na mandhari katika hadithi fupi za Kiswahili.

Mwachofi (1987:57) katika tamthilia ya Mama Ee ametumia mbinu rejeshi

ndani ya mbinu rejeshi. Mwachofi anatoa sifa za wahusika akizingatia mandhari yao. Mtunzi ameshugulikia mbinu rejeshi kwa kuwahusisha

wahusika katika kazi yake. Utafiti wetu uliangalia kwa kina jinsi wahusika

wanaathiriwa na mtindo wa mbinu rejeshi.

Naye Burhani (1987) katika riwaya ya Mwisho wa Kosa amezingatia matumizi

ya mbinu rejeshi katika sura ya kwanza. Hapa mtunzi anarejelea kuwasili kwa

Monica na tabia yake. Msilimulizi ametumia mbinu rejeshi ya ukamilishaji

kwa kuonyesha kuwasili kwa Monica na kueleza tabia yake kama mhusika

aliyedhoofika kitabia. Monica ameathiriwa na mandhari ya nchi za ughaibuni.

Aidha utafiti wetu uliangalia vile mandhari yanamuathiri muhusika katika

hadithi fupi.

Kwa mujibu wa Walibora na Wange'ndo, (2004:50-60) hadithi sharti ijenge

taharuki. Aidha wamesema kuwa taharuki hii huzua udadidisi wa wasomaji.

(26)

Maoni yao ni kuwa hadithi ambayo ni ya kweli itakuwa na sifa hii ya

kitaharuki. Kwa mantiki hiyo kasoro kubwa ambayo hadithi inaweza kuwa

nayo ni kukosa kuibua taharuki miongoni mwa wasomaji. Utafiti huu ni tofauti

na wetu. Mtindo wa taharuki umeangaziwa hata hivyo si kwa upana. Utafiti

wetu uliweza kuchunguza kwa kina jinsi mtindo wa mbinu rejeshi unaibua

taharuki kwa msomaji.

Walibora (1996) katika riwaya ya siku Njema amehakiki kazi hii na kutumia

mbinu rejeshi katika sura ya kwanza. Hapa mwandishi anaeleza maisha ya

mama yake vile alikuwa mwimbaji wa nyimbo za taarabu na jinsi alimpa

malezi bora hata hivyo mamake mtunzi alikuwa marehemu. Walibora

ameangalia sifa za mhusika katika riwaya. Utafiti wetu umekuwa tofauti na

huu. Tumeshughulikia vile wahusika wanaathiriwa na mtindo wa mbinu rejeshi

katika hadithi fupi za Kiswahili.

Mkangi (1997) ametumia mbinu rejeshi ya kibinafsi katika riwaya ya Walenisi.

Mhusika mkuu Dzombo anakumbuka jinsi alivyoasishwa kazi kutokana na

harakati zake za kuwazindua wafanyikazi wenzake. Mtunzi amewasilisha

mandhari ya ukoloni. Utafiti wetu uliweza kuchunguza jinsi mandhari

yanayoibuka kupitia matumizi ya mbinu rejeshi yanavyomuathiri mhusika.

Mbinu hii pia imetumiwa katika diwani ya Hekaya za Abunuwas na

Hadithi Nyingine katika hadithi ya kisa cha majuha wawili na wanawake.

Mtunzi wa hadithi hii arneonyesha ile athari iliyowapata wahusika na kuwa na

17

(27)

hisia za huzuni. Utafiti wetu pia uliweza kuchunguza kwa kina hisia

mbalimbali zinazowapata wahusika mtunzi anapotumia mbinu rejeshi katika

hadithi fupi za Kiswahili.

Wamitila, (2002) alisema kwamba kazi yoyote ya fasihi huwa na mwanzo, kati

na mwisho. Alitoa maoni kuwa kazi ya hadithi fupi inatarajiwa kuwa na

mtindo wa lugha ambao una uwezo wa kuwanasa wasomaji wa kazi ya fasihi.

Maoni yake ni kwamba mbinu za mtindo wa lugha ndizo zinamwongoza

mwandishi kufikia Lengo Lake. Hata hivyo Wamitila alisema kuwa mtindo wa

mbinu rejeshi hautakiwi kutumiwa kwa upana kama tanzu zingine mathalani

riwaya.

Aidha anasisitiza kuwa msomaji anapatwa mvuto ambao unamletea hisia alizo

nazo kumhusu mhusika fulani. Zinaweza kuwa ni hisia za kuchukia, kupenda,

kuhurumia, kusikitikia, kujitsmbulisha, kusinya, kukerwa na kadhalika. Ikiwa

msomaji amevutwa na mhusika huwa ana hamu ya yatakayompata. Wamitila

amesema mvuto hasi ni ule wa kinyume yaani kuchukia, kukerwa, kusnywa na

kadhalika. Mvuto hasi katika hadithi fupi hupatikana katika wahusika wawi au

asidi. Mvuto hasi katika hadithi fupi hupatikana katika wahusika nguli

kinyume na riwaya.

Utafiti wetu ulikuwa na tofauti na Wamitila kwa vilie alishughulikia matumizi

ya mbinu rejeshi katika riwaya. Utafiti wetu uilijikita katika athari ya mbinu

rejeshi katika hadithi fupi za Kiswahili. Aidha utafiti wetu utaangazia jinsi

(28)

mbinu rejeshi imekuwa na uwezo wa kumvuta msomaji ili aendelee kusoma

hadithi husika.

Wafula (1999) anasema kuwa mtindo wa mbinu rejeshi umetumiwa katika

tamthilia ya Marejeo. Wafula anadai kuwa mtunzi wa kazi hii ametumia

mbinu rejeshi kwa kuangazia vitendo viwili ili kuwasilisha ujumbe wake.

Mtunzi ameshughulikia ujumbe na mandhari. Utafiti wetu umeweza

kuchunguza kwa kina jinsi mbinu rejeshi huathiri ujumbe na mandhari ya

mtunzi katika hadithi husika.

Wamitila (2002:13) katika kitabu chake cha Uhakiki wa Fasihi anasema kuwa

mtindo wa mbinu rejeshi hutumiwa na mwandishi wa fasihi pale ambapo

anayarudia maswala au mambo ya nyuma. Wamitila anaeleza vile mwandishi

anaweza kutumia mtindo huu akiangazia sababu kadhaa. Kwanza

alizungumzia swala la kuwapa wasomi msingi au usuli wa hali ya mhusika au

wahusika mbalimbali. Aidha Wamitila anasema kwamba mtindo huu

unatumiwa ili kuweka misingi imara ya kuendeleza dhamira ya maudhui ya

kazi inayohusika. Utafiti wake unaeleza vile mbinu rejeshi katika riwaya ya

Kiu ya M.S Mohamed inajitokeza. Hapa mhusika ambaye ni Bahati

anayasimulia maisha yake na kabla ya kufikia hali ya sasa ya kupuuzwa na

kutengwa. Bahati ameathiriwa na matukio ya nyuma. Hii ndio sababu

anayasimulia maisha yake ya hapo awali. Aidha utafiti wetu utaangazia athari

ya mbinu rejeshi kwa wahusika.

(29)

Wamitila anasisitiza kuwa msomaji anapatwa na mvuto ambao unamletea

hisia. Mvuto ni hisia alizo nazo kumhusu mhusika fulani. Zinaweza kuwa ni za kuchukia, kupenda, kuhurumia, kusikitikia, kuj itambulisha, kusinya,

kukerwa na kadhalika. lkiwa msomaji amevutwa na mhusika fulani huwa ana

hamu ya kujua yatakayompata. Msomaji anaweza kuwa na mvuto chanya au

mvuto hasi. Mvuto hasi ni ule wa kinyume yaani kuchukia, kukerwa,

kusinywa na kadhalika. Mvuto wa aina hii unapatikana katika wahusika wawi

au asidi. Mvuto hasi katika hadithi fupi hupatikana katika wahusika nguli

kinyume na riwaya. Utafiti wetu unajikita katika kipengele cha mtindo cha

mbinu rejeshi najinsi inaibua mvuto kwa msomaji.

Walibora na Wang'endo (2004:59-60) wamesema kuwa ni sharti hadithi ijenge

taharuki. Aidha wamesema kuwa taharuki hii huzua udadisi wa wasomaji.

Taharuki ni mbinu inayotumiwa ili kuwafanya wasomaji au hadhira kutaka

kujua ni nini kitakachofuata. Maoni yao ni kuwa hadithi ambayo ni ya kweli

itakuwa na sifa hii ya taharuki. Kwa mantiki hiyo kasoro kubwa ambayo

hadithi inaweza kuwa nayo ni kukosa kuibua taharuki miongoni mwa

wasomaji. Maoni ya wataalamu hawa ni kuwa hadithi ambayo haina taharuki

itakuwa imepwaya na kuwa ovyo.

Kwa mujibu wa Wafula na Njogu (2007:69-70) katika Nadharia za uhakiki wa

Fasihi, mtindo wa mbinu rejeshi umetumiwa na Mazrui katika tamthilia ya

Kilio cha Haki kuthimbitisha namna matendo yaliyopita yanavyoathiri matukio

na maamuzi ya wahusika Musa na Dewe. Utafiti wetu ulichunguza kwa kina

(30)

jinsi mbinu rejeshi huathiri mtukio ya wahusika yaliyopita.

Babu (2010) amesema kuwa hadithi huwa zimekolezwa taharuki inayotarijiwa

kumvuta msomaji ili aendelee kuisoma na pia zina mwisho wa kushtukiza.

Anasisitiza kuwa mbinu hii hutumiwa kama ya kupitisha muda na kukuza

ploti. Utafiti wetu aidha uliangazia jinsi mbinu rejeshi uibua taharuki kwa

msomaji wa hadithi fupi.

Naye Mwanzi (1997) katika tasnifu yake ya uzamivu ameshughulikia mtindo

wa hadithi fupi za ngugi Wathiong'o , Leonard Kibera na Grace Ogoti.

Amezingatia matumizi ya lugha kama vile taharuki, mazungumzo na ishara.

Utafiti wetu ulikwa tofauti na wa Mwanzi. Tuliweza kuchunguza kwa kina

athari ya mtindo wa mbinu rejeshi katika hadithi fupi za wahariri Mwenda

Mbatia na Tribemwangi.

Muusya (2012) ametoa maoni kuhusu matumizi ya lugha katika hadithi fupi.

Amesema kuwa mwandishi mzuri wa hadithi fupi ni yule ambaye matumizi

yake ya lugha yatakuwa na athari wkwa msomaji wa hadithi fupi. Aidha

alitafiti mandhari katika hadithi za kiswahili. Matokeo yaliweza kugudua

kuwa waandishi wa hadithi fupi husawiri madhari iliyojikita katika en eo moja.

Anaeleza kwamba mandhari haya hayabadiliki na ikiwa yanabadilika uwa ni

kwa kiwango kidogo. Hivyo akasema kwamba mandhari yanayosawiriwa

hutengemea mwandishi mwenyewe na tajriba yake katika mazingira

(31)

anayoishi. Utafiti wa Muusya ulikuwa tofauti na wetu kwa kimsingi kwamba

utafiti huu ulijikita katika kuchunguza athari ya mbinu rejeshi katika hadithi

fupi za kiswahili.

1.7 Mbinu za utafiti

1.7.1 Muundo wa Utafiti

Utafiti huu ni wa kimaelezo. Maelezo yametolewa kuhusu namna mbinu

rejeshi inavyotumiwa katika hadithi teule. Aidha maelezo kuhusu athari ya

mbinu rejeshi katika kuwasilisha ujumbe yametolewa.

1.7.2 Mahali paUtafiti

Utafiti huu umejikita katika maktaba. Usomaji mpana wa maktabani

ulifanywa. Usomaji huu ulilenga kwa kina diwani mbili za hadithi fupi na yale

yaliandikwa kuhusu mbinu rejeshi na nadharia ya elimumtindo. Mtafiti

alisoma makala mbalimbali yalioandikwa kuhusu mada ya utafiti kama vile;

vitabu, tasnifu, magazeti na majarida. Kutokana na makala haya mtafiti alipata

mwongozo juu ya yaliyoandikwa kuhusu mada napia kujua yale yaliyofanyiwa

utafiti na wataalamu wengine. Mtafiti aliyanakili mambo muhimu aliyoyasoma

kuhusu mada ya utafiti. Miongoni mwa yale aliyoyatengwa ni matumizi ya

mbinu rejeshi na athari ya mtindo huu katika diwani mbili teule za hadithi fupi.

1.7.3 Uteuzi wa Sampuli

Mtafiti alizingatia mbinu kusudio kwa sababu alilenga diwani mbili za

(32)

hadithi fupi ambazo zimehaririwa na watunzi wawili wa kazi ya fasihi. Kazi

hizi ni Mwendawazimu na Hadithi Nyingine (2000) na Kunani Merikani na

Hadithi Nyingine (2011). Pamoja na hayo mbinu kusudio ilitumiwa

kuchanganua athari ya mbinu rejeshi katika diwani hizi mbili. Diwani za

Mwendawazimu na Hadithi Nyingine na Kunani Merikani na Hadithi

Nyingine ziliteuliwa. Kazi hizi mbili ziliteuliwa kwa sababu ziliweza kumfaa

mtafiti katika utafiti wake wa kuchunguza athari ya mbinu rejeshi katika

hadithi fupi za kiswahili. Kazi hizi zimehaririwa na waandishi tofauti. Bali

na tofauti ya waandishi, ni kazi ambazo zimeangazia matumizi ya mbinu

rejeshi ambalo ndilo wazo kuu la mtafiti katika mada yake. Mtindo wa

mbinu rejeshi umeteuliwa ili uweze kuchunguzwa kwa kina. Sababu ni

kwamba utafiti huu ulinuia kuchunguza athari ya mbinu rejeshi katika hadithi

fupi za kiswahili. Mbinu kusudio ilitumiwa kuteua hadithi kumi na nne

ambazo ni asilimia hamsini na sita kati ya hadithi ishirini na tano.

Mwendawazimu na Hadithi Nyingine

Hadhithi: Ukurasa:

1. Mwendawazimu l-10

2. Korti ya kishenzi. 28-44

3. Walicheka Kicheko .45-49

4. Mbio za sakafuni 50-54

5. Mboni ya Jicho 55-60

6. Jitu la kisasa : 66-72

23

(33)

7. Hachukuliki.. 73-90

Kunani Merikani na Hadithi Nyingine

Hadithi Ukurasa

I. Kunani Merikani 1-15

2. Mja ni mja 16-33

3. Kwa nini'r.. 56-70

4. Siri 71-77

5. Mapenzi chungu 78-84

6. Mtengo wa panya I13-119

7. Maji aliyavulia nguo!. 144-164

1.7.4 Ukusanyaji waData

Katika utafiti huu njia kuu ya kukusanya data ilikuwa ni usomaji wa kina.

Katika kusoma mtafiti alinukuu sehemu ambapo mbinu rejeshi imetumika.

Data iliyotumika katika utafiti huu ilikusanywa kutoka kazi mbili za fasihi

andishi. Kazi hizi ni Mwendawazimu na Hadithi Nyingine na Kunani Merikani

na Hadithi Nyingine. Mtafiti alisoma vitabu hivi kwa kina na kuyaandika

mambo yale muhimu yanayohusu utafiti huu. Miongoni mwa yale

yaliyotengwa ni matumizi ya mtindo wa mbinu rejeshi na kuandikwa kando

kama mojawapo ya data ya utafiti.

1.7.5 Uchanganuzi wa Data

Data iliyokusanywa baadaye ilidondolewa na kunukuliwa. Mwishowe

(34)

ilichanganuliwa kwa kuzingatia malengo ya utafiti na vilevile kuzingatia

nadharia ya mtindo. Katika uchanganuzi huu aina mbalimbali za mbinu

rejeshi zilichuguzwa. Vilevile athari ya msuko wa maudhui na usawari wa

wahusika ziliangaziwa kulingana na malengo yetu.

1.7.6 Uwasilishaji wa Matokeo

Data iliyokusanywa i1iwasilishwa kwa njia ya maelezo kwa kuzingatia sura

mbalimbali. Uwasilishaji wa data ulifanywa kwa kuongozwa na malengo ya

utafiti pamoja na mihimili ya nadharia teule ambayo ni nadharia ya

elimumtindo.

1.8 HITIMISHO

Sura hii imejadili mambo ya kimsingi ambayo yanahusiana na utafiti huu.

Haya ni pamoja na swala la utafiti, malengo ya utafiti na sababu za kuchangua

mada. Aidha misingi ya nadharia imeshughulikiwa. Upeo wa mipaka na

yaliyoandikwa kuhusu mada yameangaziwa. Mwishowe mbinu za utafiti

zimeshughulikiwa pamoja na uteuzi wa sampuli, ukusanyaji wa data,

uwasilishaji wa data na uwasilishaji wa matokeo.

(35)

SURA YAPILI

ATHARI YA MBINU REJESHI KA TIKA UWASILSHAJI WA

MAUDHUI

2.0 UTANGULIZI

Sura hii imezingatia athari ya mbinu rejeshi katika diwani ya Mwendawazimu

na Hadithi Nyingine (2000) ambayo imehaririwa na Mwenda Mbatiah na

Kunani Merikani na Hadithi Nyingine (2011) ya Iribemwangi. Sura hii

ilishughulikia mchango wa mbinu rejeshi katika uwasilishaji wa maudhui na

usawiri wa wahusika katika hadithi fupi. Mihimili ya mbinu rejeshi

imezingatiwa. Nayo ni; matumizi ya mbinu rejeshi huonyesha kile kilimpa

mhusika motisha katika hadithi, mbinu rejeshi hurudia tukio fulani kuhusu

mhusika, mbinu rejeshi huibua taharuki kwa kuzingatia vipengele vya hadithi

fupi na matumizi ya mbinu rejeshi uwasilisha dhamira ya mtunzi katika

hadithi.

2.1 Mchango wa mbinu rejeshi katika usawiri wa wahusika na

uwasilishaji wa maudhui.

Fasihi yoyote, iwe andishi au simulizi huwa na wahusika. Kwa kuwa

wahusika wanatokana na kubuniwa na msanii, hatuwezi tukawaona, bali

tuanawasihi tu. Ingawa tunaweza kuwaona wahusika katika maigizo ya

(36)

tamthilia, huwa wanawakilisha wahusika jinsi wanavyoumbwa na msanii.

Hivyo msanii huwatumia kama vyombo vya kuwasilisha ujumbe ( KLB

1989:1).

Kwa mujibu wa Maitaria (2012:5) wahusika ni viumbe wanaotenda mambo

katika hadithi. Wanaweza kuwa binadamu au hata viumbe wasiokuwa na uhai

kama vile wanyama, shetani, mizuka au vizuu.

Wamitila (2008:33) anasema kuwa wahusika wanadhibitiwa kwa kiasi

kikubwa na majukumu yao ya kiujumi katika kazi za kifasihi zinazohusika.

Maelezo ya Wamitila ni kuwa wahusika wa fasihi wanaweza kutazamwa kwa

jira za kidrama. Amemnukuu mwanatolorojia maarufu Mieke ambaye alitaja

sifa kadha za kumtambua mhusika. Kwanza, ni kuuchunguza urudiaji wa sifa

zitakazotajwa na mhusika huyo. Pili, ukusanyaji wa ujalishaji wa sifa ambazo

zinasaidia kuelezea wasifu fulani. Tatu, uhusiano wa mhusika mmoja na

wahusika wengine. Nne, kuchunguza mageuko ya mhusika - ni kwa kiasi gani

mhusika fulani anabadilika au kugeuka kitabia katika kazi inayohusika?

Matumizi ya mtindo wa mbinu rejeshi katika hadithi fupi za Kiswahili

yameweza kuwasawiri wahusika kwa kuleza tabia zao za hapo awali.

Vipengele kama vile mandhari, dhamira na maudhui huwa na mchango

mkubwa katika athari hii. Katika kiwango kikubwa mandhari yanawaathiri

wahusika kama wahusika wanaweza kuathiriana wao kwa wao. Wahusika

wanaweza kuathiriwa na mazingira, hali ya kimaumbile, mikasa na hata

(37)

tabianchi.

Mbinu rejeshi ni mtindo wa lugha unaotumiwa na waandishi wengi wa hadithi

fupi ili kupanua mawanda yake. Kwa kufanya hivyo sehemu kubwa ya

mhusika huweza kumulikwa.

2.1.1 Mwendawazimu-Rose Shake.

Mwandishi ameirudisha hadithi nyuma kwa kuelezea matukio yaliyopita.

Mzee Katona anasoma gazeti kuhusu mwanadada mmoja aliyevamiwa na

majambazi watatu katika barabara kuu ya mjini Nairobi na kupokonywa

shilingi elfu hamsini alipokuwa akitoka benki. Hapa mhusika Katona ana

mawazo kuhusu visa vya unyang'anyi wa pesa ambavyo vinatokea mjini

Nairobi. Hii ni mbinu rejeshi ya kibinafsi. Kwa mfano katika nukuu ifuatayo

kuna maelezo kuhusu visa vya vinavyotokea mjini Nairobi

Ni juzi tu kulikuwa na kisa cha jamaa mmoja aliyeghibiliwa

kwamba atazidishiwa pesa zake maradufu akisali pamoja na

"makasisi" wawili waliokuwa na kipawa cha kuwaombea watu.

Katika maombi yaliyofanyika katika kichocheo kimoja karibu

na kituo kimoja cha magharibi cha "Tea Room, jamaa huyu

alifumbua macho baada ya"Amen na kujikuta peke yake.

Shilingi zake elfu kumi na moja na viatu alivyambiwa avivue

katika kusali vikawa vimeporwa (uk. 2-3).

Aidha Mzee Katona anaonekana akiwa na mawazo zaidi kuhusu vile mkewe

alimshawishi ili waambatane pamoja akienda kuchukua kiinua mgongo. Hata

(38)

hivyo mzee Katona hakuyakubali maoni ya mkewe kwa sababu ameishi

Nairobi kwa miaka kadhaa na haoni sababu ya kuandamana na bibi yake

Ndunge.

Mtunzi ametumia mbinu rejeshi ya kibinafsi na kuweza kuwasawiri wahusika.

Maelezo haya yote ya mwanadada, jamaa na Mzee Katona yameweza

kuwasawiri wahusika na tabia zao. Makasisi wanaotajwa na mwandishi si

makasisi wa kweli bali ni wezi ambao wamejibandika jina la dini. Hawa si

waumini wa Mungu maana wanaiba mali ya wenyewe.

Mzee Katona ni mtu mwenye tamaa kwa sababu hataki kuandamana na bibi

yake kwenda kuchukua kiinua mgongo. Shida anazozipata mzee Katona

zinasababishwa na kukosa kutilia maanani maoni ya mkewe Ndunge. Kama

angemsikiliza mkewe, yanayompata kwa sasa hayangempata. Hii ndio sababu

ana mawazo mengi kuhusu wizi wa ulaghai unaoendeleajijini Nairobi.

Mwandishi ameweza kuwasilisha masuala ya wizi na tamaa. Haya yanajitokeza

kupitia wahusika kama Mzee Katona, wezi wanaojifanya kuwa makasisi na

kisa cha mwanadada aliyeibiwa na majambazi.

Ndunge ni mhusika ambaye ana maono na anampenda mume wake Katona. Ni

mnyenyekevu na anatumia lugha yenye heshima. Mwandishi anatumia mbinu

rejeshi ya ndani na kuonyesha vile Ndunge aliweza kumpa mumewe nasaha

kuhusu safari yake. Haya yanawasilishwa na nukuu ifuatayo:

(39)

"Mume wangu si vyema kwenda peke yako. Unaweza kuporwa mali

hiyo na majambazi. Tafadhali tuandamane ili tuweze kusaindiana kuzilinda pesa hizo majambazi watasita kutuvamia tukiwa pamoja

kuliko ukiwa peke yako ... "(uk. 3)

Ndunge anatumia lugha yenye unyenyekevu. Hii ni dhibitisho kuwa huyu ni mhusika mwenye heshima kwa mumewe.

2.1.2 Kunani Merikani--Iribemwangi

Hadithi hii imeanza na mbinu rejeshi ya muktadha mpana. Mwandishi ambaye

ni msimulizi anayasimulia maisha yake ya tangu utotoni. Ameeleza ile tamaa

aliyekuwa nayo ya kwenda Merikani katika enzi zake za utotoni. Kule

kumulika maisha ya mhusika ya hapo awali kumeweza kuibua maudhui ya tamaa na kumsawiri msimulizi kama mhusika mwenye tamaa kupitia maelezo

yafuatayo;

Nilipokuwa mtoto mdogo nilitamani sana kwenda Merikani, kwa

hakika nilitamani sana kupanda ndege. Wakati huo, uzuri au ubaya wa ndege ulikuwa wa kufikirika tu; kwa hakika sikumbuki kufikiri ubaya wowote ... (ukl). Merikani. Ni tamaa iliyoniandama sana wakati wa miaka yangu ya awali (uk.l)

Mtunzi anadhamiria kuonya jamii dhidi ya tamaa katika maisha. Mwandishi ana tamaa ambayo iliweza kumpa motisha, akasoma hadi Merikani na kuweza

kutimiza ndoto zake. Rata hivyo kuna baadhi ya wahusika ambao wameweza kuwa na tamaa yenye mwelekeo hasi na kupotoka katika maisha yao.

(40)

Kulingana na mwandishi wahusika hawa ni kama mkurugenzi, kasisi na Liz.

Ni tamaa ambayo i1iweza kumfanya mkurungezi kwenda Merikani na kuacha

kazi yenye hadhi nchini. Mwandishi ametumia mbinu rejeshi ya muktadha mpana na kueleza maisha ya mkurugenzi na vile aliathiriwa na tamaa na

mwishowe akaanza kuishi maisha ya dhiki. Anaeleza jinsi Mkurugenzi

alikuwa akifanya kazi ya kifahari akiwa nchini Kenya. Mwishowe mwandishi

anaonyesha vile Mkurugenzi anasosoneka akiwa nchini Merikani (3-4).

Mkurgenzi na familia yake wameathiriwa na maisha wanayoishi kwa sasa kwa

sababu ya tamaa. Alikuwa anaishi maisha ya ubwanyenyenye akiwa nchini

Kenya lakini kwa sasa yeye na familia yake wanaishi maisha ya ufukara.

Mkurugenzi anafanya kazi ya shokoa huku Merikani kisa na maana

hakutosheka na mapato aliyekuwa akiyapata katika nchi yake.

Mwandishi amemsawiri mhusika kasisi kama mhusika mwenye tamaa kwa

matumizi ya mbinu rejeshi. Kasisi alipatwa na tamaa ambayo ilimpeleka

Merikani na kuacha kuendeleza injili ya Bwana. Mwandishi anaeleza kuwa si

Mkurugenzi ambaye alikuwa na tamaa ya kwenda Merikani bali kulikuwa na

wengine kama kasisi ambaye mwishowe aliweza kuathiriwa na tamaa

aliyekuwa nayo. Mtunzi ametoa maelezo yafuatayo kuhusu tamaa iliyompata

kasisi.

I1ifika wakati kasisi akapatwa na wazimu wa kwenda Merikani. Mwanzo akitafuta visa ya kwenda kule kama mwanafunzi lakini

31

(41)

hatimaye "akafanikiwa" kapata mwaliko kuhudhuria mkutano mkubwa wa dini. I1ivyo ni kwamba bahati, kama vile msiba, haiji pekee; huja na mwezake ...(uk 6-7).

Hii ni mbinu rejeshi ya muktadha mpana. Sifa za kasisi zinajitokeza. Yeye

ni mhusika mwenye tamaa kwa sababu hatosheki na mapato anayoyapata

kutokana na kuendeleza inj ili.

Kasisi aliishi maisha ya wastani na familia yake akiwa nchini. Kwa sasa

anaishi maisha ya dhiki na shida. Ameshindwa na kuendelea na elimu na

kuanza kutafuta kazi hapa na pale. Mwishowe hakufanikiwa kuipeleka familia

yake Merikani kama alivyotarajia. Kwa sababu ya tamaa alianza kuogopa

kushikwa na mkono wa sheri a na hii ndio sababu alikosa kukutana na jamaa

yake katika uwanja wa ndege huko Merikani.

Liz naye kwa kukosa kufanikiwa kwenda Merikani na kuishi huko kama ahadi

ya baba yake, aliamua mwishowe atasafiri hadi Merikani liwalo liwe. Tamaa

ndio ilimfanya kumtafutia mtoto wake bibi yaani Natasha bila hata kujali hali

yake na kumfanya kupatwa na ugonjwa wa Ukimwi. Natasha anamwandikia

Liz barua na kumpasha juu ya siha yake na kumueleza vile aliweza kumkosea

mtoto wake. Haya yanaelezwa kwa matumizi ya mbinu rejeshi ya muktadha

mpana. Barua ifuatayo imetoa maelezo zaidi.

13-03-200

Kwa Liza

(42)

Salamu zangu bibie. Natumai kuwa hali yako ni nzuri tangu

nilipokuletea mwanao miaka ipatao miwili sasa. Mimi nipo ingawa bado sijampata Mwafrika mwingine WA kutaka niolewe Na mwanaye

japo Kwa muda, labda nikushukuru kwa sababu ya fadhila hiyo

uliyonitendea. Hata ssuliyoyatenda, yaani kumkosea mwanao heshima ulivyomkosea, na mengine nitakayokupasulia hivi punde?.

Lakini samahani kwa hayo, kusudi la kukuandikia barua hii haikuwa

kuzungumza mambo ya dawa. Nilitaka kumjulia h"alialiyekuwa mume wangu. Nimekuuliza ni lipi la mno Merikani hata ukamletea mwanao maafa uliyomletea. Uliponilipa nikaolewe naye, hata

hukusaili kujua haliyangu. Haliyangu si nzuri kiafya, lakini nilihitaji

fedha, fedha! Tangu miaka minne iliyopita niliguduliwa kuwa nimeambukizwa virusi vya ukimwi, na kwa sababu hiyo, nimekuwa

mhitaji wa fedha ili kuweza kujikimu kwa chakula kifaacho na

dawa. Hii ndio ilikuwa sababu nilikubali ombi lako jambo shingo

upande na kwa moyo mzito. Nilibaini kwamba kama singefanya hivyo, ningekufa mapema, labda hata sasa ningekuwa marehemu, na sikuwa tayari kufa kijana ...

Kila la kheri,

Natasha carrier (uk14).

Barua hii inatoa maelezo kuhusujinsi Liz alimuoza Natasha kwa

(43)

mwanaye Sisika bila hata kujali hali ya Tasha ambaye alikuwa na maradhi ya

Ukimwi. Hii ni thiibitisho kuwa Liz alikuwa na tamaa. Mwandishi

ameyamulika maisha ya Liz yenye tamaa na kumsawiri kama mhusika mwenye

tamaa. Shida zinazompata mtoto wake zinasababishwa na yale maisha ya

kwenda Merikani. Mwanawe kwa sasa ni mlaguzi wa dawa za kulevya kama

yeye na isitoshe, ameabukizwa maradhi ya Ukimwi.

Kama tulivyosema hapo awali wahusika wa hadithi fupi huwa wachache.

Ukweli ni kuwa kuna wahusika wengine ambao wamesadia kuendeleza hadithi

ingawa sio wahusika wakuu. Matumizi ya mbinu rejeshi huwasawiri wahusika

wasaidizi. Mfano wa wahusika hawa ni kama Natasha, watoto wa kasisi

kama Liz, Sisika ambaye alikuwa mtoto wa Liz na Natasha bibiye Sisika.

Mwandishi ameyasawiri maudhui mbalimbali kama tamaa, matumizi ya dawa

za kulevya, maradhi ya Ukimwi, elimu na kazi. Suala la tamaa lajitokez kwa wahusika kama msimulizi. Alitamani sana kwenda nchini Merikani na

mwishowe akafanikiwa na akarudi nchin na shahada yaphD. Hapa mwandishi

amejaribu kuonyesha jamii kuwa kuna tamaa ambayo inaweza kuwa na

mwelekeo chanya na kuweza kumfanya binadamu kuishi maisha yenye

mafanikio. Msimulizi kwa sasa anaishi maisha ya furaha akiyalinganisha

na yale ya Mkurugenzi, kasisi, mke wa kasisi na watoto wa kasisi kama

Liz.

Kwa wahusika hawa matarajio yao yaligonga mwamba na mwishowe

(44)

wanapata dhiki badala ya mafanikio. Mkurugenzi anaishi maisha ya

kuhurumiwa maana anafanya kazi usiku na mchana huku akidhulumiwa.

Kasisi naye hana lingine isipokuwa kutafuta kazi hapa na pale ndio

aweze kupata mkate wa siku. Liz amekuwa mlaguzi wa dawa za kulevya

pamoja na mwanaye. Wahusika hawa wameathiriwa na matukio ya

nyuma ambayo ni majuto kwa sasa.

Maudhui ya dini na elimu aidha yamesisitizwa. Kasisi alikuwa anaeneza injili

ya Mungu. Suala la elimu linajitokeza wakati msimulizi anayaeleza maisha

yao ya shuleni na mkurugenzi. Msimulizi naye anaenda Merikani na kumaliza

masomo yake. Kazi ni muhimu sana katika jamii. Mkurugenzi alikuwa

akifanya kazi ambayo ilimfanya kuishi maisha ya mlalaheri. Kasisi alifanya

kazi ya kuendeleza ya Mungu na iliyowakimu maishani.

2.1.1 Korti ya Kishenzi - David Maillu

David Maillu anadhamiria kulenga dhana ya elimu na utamaduni katika

jamii. Mwandishi anaeleza vile elimu na utamaduni katika jamii

zimekizana na kuleta mgogoro baina ya waliosoma hasa wale wenye

elimu ya juu na wale ambao hawajasoma. Aidha vijana wanaonywa

kuhusu uhusiano wa kimapenzi katika ujana wao ambao kwa upande

mmoja unaathiri hasa jinsia ya kike.

Mtunzi ametumia mbinu rejeshi ya ndani ambayo inaibua mbinu rejeshi

ya kibinafsi. Mhusika Kanu anaathiriwa na habari alizoletewa juzi

(45)

kuhusu uhusiano wa kimapenzi baina ya mume wake na mhazili. Kanu

alipoteza uwezo wa kupanga na kuendesha shughuli zake. Anapatwa na

fikra kuhusu maisha yake, mapenzi, ndoa na watoto. Hii ni mbinu rejeshi

ya kibinafsi.

Jana alipoletewa habari kuwa mumewe anatembea na mhazili

wake, uwezo wa kupanga na kuendeleza shughuli zake ulimwishia

(uk29).

Kanu anapatwa na fikra za maisha yao na Ngoloso wakiwa shuleni.

Mtunzi ameweza kueleza vile vijana hawa waliweza kuongelelea katika

bahari ya mapenzi bila kuwa na mbinu tosha kwa matumizi ya mbinu

rejeshi. Anaeleza vile maisha ya Kanu yaliweza kuathiriwa na matukio

yaliyopita kupitia mbinu rejeshi ifuatayo.

Kabla ya kuoana, Agnes Kanu na Onesmas Ngoloso walijikuta

katika bahari ya mapenzi bila ya kuwa mbinu tosha za

kuongelea. Walipatana humo kwa muda. Ngoloso alikuwa

chuo kikuu akisomea uanasheria, naye Kanu alikuwa

mwanafunzi wa shule ya upili. Wote walikuwa vijana wabichi. Katika bahari ya mapenzi wanagenzi wasio na

uzoefu wa kuongelea hukumbwa na ajali nyingi. .. (uk 29).

Hapa mbinu rejeshi kadhaa zimefuatana na kuweza kuibua mbinu rejeshi

ya kikufu. Mbinu rejeshi hizi zimeweza kuwasawiri wahusika kwa kutoa

siri zao kama vile; mhazili, Kanu na Ngoloso. Maisha ya Agnes Kanu

na Onesmas Ngoloso .yanaelezwa na sababu zinazomfanya Kanu kuwa na

(46)

mateso anayoyapata kwa sasa. Kanu hakuweza kumaliza masomo ya

shule ya upili kwa sababu alipata mimba akiwa katika kidato cha pili

naye Ngoloso akiwa katika chuo kikuu akisomea uanasheria. Jambo ili

lilimlazimisha Kanu kuacha shule na kuolewa na Ngoloso.

Uhusiano wa kimapenzi wa Ngoloso baina ya mhazili wake ni jambo la

siri hivyo Iikafichuliwa na matumizi ya mbinu rejeshi.

Sifa za Ngoloso na Faith zinajulikana kupitia mapenzi yao. Mwandishi

anaeleza uhusiano wa Ngoloso na Faith vile ulianza na vile Ngoloso alikuwa

na mbinu za kuwatongoza wan awake kwa kuirudisha hadithi nyuma.

Tangu mapenzi ya Faith na Ngoloso yaanze, mwanamke

huyu alijihisi kwamba, aliyokuwa akifanya siyo sawa lakini

angefanyaje na Ngoloso alikuwa bosi wake na bali na

hayo Ngoloso alikuwa na sifa chungu nzima zilizowafanya

wan awake wengi kuvutiwa naye ...(uk32).

Ngoloso ni mhusika ambaye amekosa uwajibikaji. Si kielelezo chema katika

jamii. Anamnyanyasa Faith ambaye ni mhazili wake kupitia mapenzi nje

ya ndoa. Ingawa hisia za Faith zinamuarifu kuwa yale anayoyafanya

hayafai, hana suluhisho kwa sa sa maana Ngoloso ni bosi wake.

Kanu ni mlezi wa watoto wao: Ana fikra kuhusu vile ataendelea na

kuwalea watoto wao peke yake alipopata habari ya uhusiano

37

(47)

wakimapenzi wa mumewe na mhazili wake.

Ngoloso hana utu maana anafanya mapenzi na mhazili wake na

kumnyima mkewe mapenzi.

Ngoloso m mhusika asiyewajibika kwa sababu anatafuta mbinu za

kumuacha Kanu kupitia fikra alizokuwa nazo ili aweze kumuoa Faith

ingawa alijua ukoo ulimpenda Kanu sana. Nukuu ifutayo inatoa maelezo

zaidi.

Bwana Ngoloso alifikiria njia kadha wa kadha za kumfukuzia

Kanu ili aweze kupata njia ya ndoa baina yake na Faith.

Lakini hakuweza kupata njia mwafaka. Alifahamu kwamba

wazazi wake walimpenda Kanu na hawangesikiliza sababu

zake za kutaka kumfukuza (uk 35).

Mwandishi ameweza kuyasawiri maudhui mbalimbali. Suala la mapenzi na

ndoa limeangaziwa. Ngoloso anafanya mapenzi nje ya ndoa. Aidha maudhui

ya elimu yanajitokeza wakati mwandishi anaeleza maisha ya Ngoloso na

Kanu wakiwa shuleni. Ngoloso aliweza kumaliza masomo yake na

kupata kazi ya uanasheria. Kanu naye hakuweza kumaliza masomo yake.

Alipata mimba na kuolewa na Ngoloso.

(48)

2.1.4 Siri- Stephen Munyasi.

Hadithi hii imeanza na mbinu rejeshi ya muktadha wa karibu. Mwandishi

anadhamiria kueleza jamii kuhusu athari ya vyombo vya teknolojia ya

kisasa kwa vijana. Kwa mujibu wa mada ya hadithi hii, mwandishi

ameweza kuficha siri za wahusika Siri na mama yake akizingatia mbinu

rejeshi.

Siri ana mawazo kuhusu rafiki yake aliyempata katika mtandao. Mawazo

haya yamemsababisha kuumwa na kichwa huku maneno ya mpenzi wake

yakimpitikia akilini mwake huku akimwita kirukanjia (uk 71-72).

Siri ameathiriwa na mapenzi kiasi cha kuwa na fikra kuhusu mpenzi

aliyempata katika Facebook. Hata hivyo haya ameyaweka kama siri.

Anaathiriwa na mapenzi ya mpenzi wake na kuanza kuumwa na kichwa.

Iwapo hangekuwa na uhusiano huu tena wa mpenzi aliye mbali

hangekuwa na mawazo ambayo yanamtatiza.

Mamake mzazi anaathiriwa na tabia ya Siri mpaka anawaza na kuwazua

ni nini cha mno kinachosababisha binti yake Siri kuwa na tabia ya kutojieleza

ni jambo gani linalomuathiri. Hapa ndipo mama mzazi anapatwa na fikra

kuhusu tatizo la bintiye. Mamake Siri hakuweza kueleza mwanawe kile

kilisababisha kifo cha mumewe. Jambo hili aliliweka kama siri na ndio maana

anaona kama Siri ameligudua (uk73).

(49)

Bi Mkata pamoja na Siri ni wasiri. Kati yao wawili hakuna anayetaka

kueleza shida zake. Mamake Siri ameweka siri kuhusu kilichosababisha kifo

cha mumewe naye Siri ameficha shida inayamkabidhi kwa mamake ingawa

anasononeka.

Kuna matumizi ya mbinu rejeshi ndani ya mbinu rejeshi wakati mhusika

Siri anakumbuka kuhusu riwaya aliyoisoma ya wahusika wawili. Mtunzi

ameanza na mbinu rejeshi ya kibinafsi mwishowe anasimulia hadithi ya

wahusika wawili waliopendana katika nukuu ifuatayo:

Alikumbuka riwaya aliyokuwa amesoma kuhusu wahusika wawili waliopendana kama chanda na pete. Wahusika hawa walifunga ndoa ya kukata na shoka lakini wakatalikiana miezi mwili tu baada ya arusi yao (uk 74).

Maudhui ya ndoa na talaka yamewasilishwa. Aidha Siri ni msomi kwa

sababu anakumbuka yale aliyeyasoma kuhusu wapenzi wawili wailopendana.

Jambo hili linamuathiri Siri hadi sasa ndio sababu analikumbuka.

Mhusika Siri alibakwa akiwa na miaka minane na kuamua kutosonga

karibu na mwanamume. Haya yanajitokeza wakati anapokumbuka tukio la

ubakaji ambalo linamuathri kwa sasa (uk76).

Iwapo Siri angetilia maanani ahadi yake ya kutojihusisha na mapenzi

kiholelaholela, shida alizo nazo kwa sasa hazingempata. Rafiki wa

(50)

facebook ameweza kumuabukiza maradhi ya Ukimwi. Sijali ameanza

urafiki na mabinti wengine wakati Siri hakuwa karibu.

Wakati uhusiano huu ulivunjika na kuelewa fika kuwa ana maradhi ya

Ukimwi, Siri anajiua na kuweza kuipa dunia mkono wa buriani. Kabla

ya kifo chake alimwandikia mamake barua na kumharifu kuhusu rafiki

yake aliyempata kutoka kwa facebook Sijali na ni yapi yaliyotokea baada

ya urafiki wao.

Kwa mama mpendwa, Bi Mkata,

Nasikitika kukufahamisha kwamba nina ugonjwa wa ukimwi.

Niliambukizwa na kijana mmoja aliyekuwa rafiki yangu niliyempata kwenye mtandao wa facebook. Niliamini ahadi zake, kisha yakawa na kutimia yalivyo sasa hivi licha ya kuahidiwa maisha ya uaminifu na raha mustarehe. Nilivutiwa na pasipo kujua kuwa anasambaza gonjwa hili kwa yeyote anayenaswa mtengoni.

Usinichukie kwa sababu nishajichukia. Ongea na Bw. Mroho akuonyeshe miradi niliyokuwa nimeandika kwa jina lako ili usiteseke. Rafiki yangu, Roka, atakupatia kadi ya kutoa pesa mtamboni katika benki ya Wanyonge niliyompa jana. Mama, amini kuwa Roka, hakujua masaibu wala mipango yangu ya kulitekeleza hili.

Mwanao, Siri Mkata (uk77).

Mwandishi ametumia mbinu rejeshi ya muktadha mpana aidha ya

muktadha wa karibu. Barua hii imefichua siri zote za mhusika Siri

(51)

alizokuwa amemficha mamake Bi Mkata. Uhusiano wake wa kimpenzi na

mpenzi wake Sijali na mali ambayo mamake atakayeimiliki baada ya

kifo chake. Mhusika siri ni msiri. Ameweza kumficha mamake uhusiano

wake na rafiki yake Sijali hadi dakika ya mwisho.

Mtunzi ameonyesha i1e athari inayoweza kuwapata wahusika ambao

wanajihusisha na uhusiano wa marafiki kutoka vyombo vya tekinolojia

bila hata kujali hali yao ya kiafya.

Suala la mapenzi nje ya ndoa hasa kwa vijana wa sasa Iimesisitizwa.

Vijana wengi katika jamii wameweza kuathiriwa na mapenzi wanaofanya

kiholelaholela bila hata kujali athari ya hayo mapenzi.

2.1.5 Walicheka Kicheko - John Habwe.

Mwandishi ameyarejerea maisha ya Zainabu na Mogambi wakati ndoa

yao ilikuwa bichi kwa kutumia mbinu rejeshi ya muktadha mpana.

Maelezo haya yamepichua siri za wahusika hivyo kuweza kuwasawiri.

Walipooana Mogambi alikuwa hatoki. Yuko pale

kama paka na JIVU lake. Hata si fungate Hata

baadaye alikuwa siku zote yuko ... (uk. 45).

Mogambi kwa wakati huu alikuwa bwana aliyewajibika katika ndoa yao

na Zainabu. Mtunzi ameonyesha vile matukio ya mhusika yalikuwa ya

furaha na yenye starehe. Hii ni dhihirisho kuwa tabia zake zilikuwa za

(52)

kupendeza hasa kwa mke wake.

Mbinu rejeshi inayofuata ni ya kibinafsi. Starehe walizokuwa nazo Mogambi na Zainabu hazipo kwa sasa. Zainabu anakumbuka ile siku ya Jumamosi

Mogambi alikunywa hadi akajitapikia. Mwandishi ametumia mbinu rejeshi

ya kibinafsi ambayo imeweza kuibua mgogoro baina ya Zainabu na nafsi

yake na pia Mogambi. Aidha tabia za Mogambi na Zainabu zinajitokeza.

Haya yanajitokeza kupitia nukuu lifuatalo.

Hii tabia ya Mogambi ya kuchelewa imekuwa ya muda. Anakumbuka siku ile ya Jumamosi alipofika nyumbani amekunywa hadi kujitapikia,

Zainabu hakuwa na budi i1a kumpiga kofi tatu (uk.46-47).

Zainabu anaathiriwa kiasi cha kumchapa mumewe kofi tatu. Mbinu rejeshi hii

imeleta mgogoro wa kisaikolojia kwa mhusika. Mhusika anakubwa na

mvutano wa ndani kwa ndani. Mwandishi amewaathiri wahusika Mogambi

na Zainabu kwa kuibua mgogoro ambao unamsaidia kuwasawiri. Zainabu

amechangia kusaidia katika kujaribu kukomesha tabia ya mumewe ya

ulevi kwa kumchapa kofi tatu na kuweza kupingania haki yake.

Sifa za Mogambi na Zainabu zinajitokeza. Ulevi wa Mogambi ni tukio

ambalo limekuwa la mazoea ambalo linamfanya kulewa kiasi cha kujitapikia

na kudondokwa na mkojo kama mtoto mchanga. Mwandishi amenuia

kutengua kitendawili cha ndoa ambazo zimetiliwa mbolea na ulevi na

kuwazidua wahusika- kama Zainabu ili waweze kujitetea. Tabia za

(53)

Mogambi na Zainabu zimefichuliwa na mtunzi kwa matumizi ya visegere nyuma hivyo basi kuweza kuwaathiri. Mogambi ni mlevi ambaye hajali utu wake. Kule kulewa kiasi cha kujikojolea kumempotezea utu. Naye Zainabu ni mtetezi wa haki za wanawake katika jamii.

Maudhui ambayo yanayoibuka katika hadithi hii ni ya ndoa, ulevi na haki za wanawake. Zainabu anatetea haki za wan awake kwa kukataa dhuluma ya mumewe anayomfanyia kupitia ulevi wa kupindukia.

2.1.6 Mbio za Sakafuni -0. Ong'utu

O. Onguti katika "Mbio za Sakafuni" amewasawiri wahusika Mosoti, Okiomo na Gladys kwa matumizi ya mbinu rejeshi. Mbinu rejeshi mbalimbali zimewasilishwa kama vile; mbinu rejeshi ya muktadha mpana, mbinu rejeshi

ya ndani na mbinu rejeshi ya kibinafsi.

Mapenzi ya Gladys baina ya Okiomo na Mosoti yalianza wakiwa katika shule za upili. Wanafunzi hawa walipokuwa wakisoma katika shule ya upili ndio walianza kumpenda Gladys wakiwa katika kidato cha kwanza. Mtunzi anaeleza vile Okiomo na Mosoti hawangeweza kujua kama wana urafiki na msichana mmoja Gladys maana hawakuambiana siri zao kupitia urejeshi ufuatao.

Gladys alikuwa mwanafunzi katika shule ya upili ya wasichana ya Nyahururu. Okiomo alikuwa katika shule ya upili ya wavulana ya Sameta na Mosoti

(54)

alikuwa akisomea shule ya wavulana ya

Mosocho .... Mosoti na Okiomo walikuwa wamemtaka

mapenzi Gladys walipoingia kidato cha kwanza.

Mosoti na Okiomo hakuambiana siri zao (uk 52).

Mwandishi ametumia mbinu rejeshi ya ndani kwa kuonyesha vile hali

ilivyokuwa au mandhari yanayojitokeza wakati Okiomo na Mosoti

wanaenda kumtembelea mpenzi wao Gladys bila kujuliana hali. Anaeleza

vile Okiomo alianza kusinzia baada ya muda wasaa moja na mwishowe

alipatwa na hofu (uk 53).

Aidha kuna maeleza kuhusu Okiomo na vile alikuwa akifanya wakati

Mosoti aliona mbalamwenzi na kukimbilia usalama wake.

Wakati huu Okiomo alikuwa ameanza kusinzia kwani

saa moja ilikuwa imeshapita. Aliposikia sauti fulani

alianza kushikwa na hofu ... (uk 53).

Mwishowe matumizi ya mbinu rejeshi ya kibinafsi yanajitokeza. Okiomo na

Mosoti waliweza kukimbilia usalama wao kwa kuogopa wasionekane na

babake Gladys ambaye walifikira amekuja kuwaadhibu. Okiomo aliposikia

kwamba nyasi aliyokuwa amejifunika nayo imeondolewa alifikiria ni

babake Gladys amekuja kumshambulia. Wakati huu naye Mosoti alitoka

ndani ya nyasi alifikria kwamba ni babake Gladys amekuja kumwadhibu.

Mbinu rejeshi kadhaa zimeweza kuwasawiri wahusika ambao

wamemsaidia mwandishi kuwasilisha dhamira yake. Aidha mandhari

References

Related documents

Avail- ability of the full genome sequence and use of another popula- tion will allow determining more precisely hot and cold regions in bread wheat because, in light of

Crossing over between the genes for frizzling and for dominant white was found to be about 18 percent. This finding along with those of other wprkers permits the tentative

The fuzzy based expert system applied to the battery scheduling based on the measured real time data or forecasted data as follows: Time(T), The Battery State of

Modelling stability analysis and control of a direct AC/AC matrix converter based systems MelakuMihretIEEE (2011) presented about direct and indirect space vector

Following the collection of the first harvests the F1 plants were again selfed and then all of the leaves and side branches were removed so that second harvests of seed were

Our results show that, although tetrasomic inheritance creates additional con fi gurations of lineages that have unique probabilities of coalescence compared to those for

2) Despite the design principles and standards contained in both codes IS and Euro standards codes are same, but they vary in configuration, design criteria, detailing and

A segment based texture analysis method is developed by Chan et al. Segment the crowd into variable motion directions; then, extract some segment features like