• No results found

Uwiano wa picha na matini katika mabango ya matangazo ya ukimwi: mtazamo wa Kisemiotiki

N/A
N/A
Protected

Academic year: 2020

Share "Uwiano wa picha na matini katika mabango ya matangazo ya ukimwi: mtazamo wa Kisemiotiki"

Copied!
208
0
0

Loading.... (view fulltext now)

Full text

(1)

UWIANO WA PICHA NA MATINI KATIKA MABANGO

YA MATANGAZO YA UKIMWI: MTAZAMO WA

KISEMIOTIKI

TasnifuYa

~MANI

HELLENWANJlKU

lliyotolewa kwa madhumuni

ya kutosheleza baadhi ya

mahitaji ya Shahada ya Uzamili katika Chuo Kikuu

cha Kenyatta

2006

KENYATIA UNlVERSi

I

1 RA

(2)

UNGAMO

Tasnifu hii ni kazi yangu mwenyewe na haijatolewa kwa mahitaji ya Shahada katika Chuo Kikuu kingine chochote.

KIMANI HELLEN WANJlKU

Tasnifu hiiimetolewa kwa Chuo Kikuu kwa idhini yetu kama wasimamizi.

~...>.,..l.--O

--DKT. C. M. NDUNGO

(3)

TABARUKU

Kwa mume wangu mpendwa Philo, na watoto wangu Eddy, Chris na Diana! Mapenzi yenu yalinitungisha nia ya kuendelea kuchuana na vitabu hata pale mambo yalipokaribia kunichusha, kuniatilisha, kunisikitisha na kunishawishi kukata tamaa. Tulijua tulipotoka lakini hatukujua tulipokwenda ... tukapiga hatua kujaribu! Sasa hapa tulipo ...

(4)

SHUKRANI

Ahimidiwe Mwenyezi Mungu! Tasnifu hii ni zao la rehema na baraka zako.

Shukrani zangu ziwaendee wasimamizi wangu waadhama, Dkt. C. M. Ndungo na Dkt.A.N. Mwihaki kwa wasaa wao walioutwaa kuniongoza, kunishauri na kunitia moyo kila hatua ya utafiti huu. Dkt. Mwihaki, nimefarijika na msaada wa vitabu na kazi zako tangu nillpoanza utafiti. Nawashukuru wote wawili kwa maoni na maarifa mlionipa ill kuituja tasnifu hii hadi kufikia kiwango ilivyo sasa.

Nawashukuru wahadhiri wote wa Idara ya Kiswahili na Lugha za Kiafrika kwa kunielimisha na kunitia shime katika kila hatua ya masomo yangu. Wahazili, Mary Khaemba na Ann Kimotho, twaeni shukrani zangu kwa mahimizo yenu wakati wa kozi hii.

Nawashukuru wasomi wengine tulioanza pamoja safari hii ya usomi, tukafaana kwa vitabu na mawazo. Tulikuwa masahibu tukaoneana imani na kuhimiliana katika yote tuliyoyafanya. Nitawezaje kuwasahau akina Kea, Nelly, Salome, Kihara, Mungai na Wachira. Mlinishajiisha kila nilipokaribia kufa moyo. Shukrani zisizo kifani ziwaendee, Munuku Ann, King'ori Ann, Karuga Mary, Gitau Elizabeth na Savala kwa kunifaa kwa vitabu na mawazo. Nawaombea kila la heri.

Kutimia kwa tasnifu hii kusingefikiwa pasi mchango wa watafitiwa walioshirikishwa nyanjani, kwa maswali ambayo kwao wao yalikuwa hayana faida bali udhia na usumbufu wangu. Haiyumkiniki kumtaja kila mmoja kwa jina katika nafasi hii. Kwa hivyo, wote nawashehenezea shukrani zangu kwa mchango wenu.

(5)

Maelezo ya Istilahi Muhimu

Bango Ishara Maana Matini Msimbo Semiotiki Stiari Uchanganuzi Matini

Uchanganuzi Picha na Ishara

Ukinzano

Utata

Kipande cha karatasi ngumu kama kadi, au bati lililoangikwa mahali - kwenye barabara au maeneo mengineo. Katika muktadha huu ni ilani/tangazo.

Alama, kidokezi au kielekezi chochote katika tangazo.

Fahiwa za neno na picha.

Kifungu cha maandishi au taarifa

inayojisimamia katika kueleza dhana fulani. Mfumo wa mawasiliano.

Taaluma inayoshughulikia ishara za mawasiliano.

Maana fiche inayoweza kufasiriwa kutokana na matini na picha katika kazi.

Uhakiki unaotumia mbinu za kiisimu katika kuangalia jinsi visehemu mbalimbali

vilivyosawiriwa ili kuwasilisha maana na ujumbe. Uhakiki unaotumia mbinu zisizo za kiisimu katika kuangalia jinsi viunzi tofauti vya picha na ishara vilivyosawiriwa ili kufanikisha uwasilishaji wa maana na ujumbe.

Hali ya maana katika kipashio fulani au picha fulani kupingana au kukosa upatanifu.

(6)

VIFUPISHO

AAWORD Association of African Women for Research and Development. (Ushirika wa Wanawake wa Afrika wa Utafiti na Maendeleo.)

ART Antretroviral Therapy.

(Huduma ya Tiba ya Kupunguza Makali ya UKIMWI.)

ARV Antiretrovirals.

(Madawa ya Kuimarisha Afya ya Wagonjwa wa UKIMWI.)

DASCOP District AIDS/STD Coordinating Programme. (Washirikishi wa Ngazi za Wilaya wa Mipango ya kupambana na UKIMWI na Magonjwa ya Zinaa.) KDHS Kenya Demographic and Health Survey.

(Uchunguzi wa Demografia na Afya ya Jamii Nchini.)

KNASP Kenya National HIV/AIDS Strategic Plan.

(Mikakati ya Kitaifa ya Kupambana na UKIMWI.) NACC National AIDS Control Council.

(Baraza la Taifa la Kupambana na UKIMWI.) NASCOP National AIDS/STD Control Programmme.

(Mpango wa Taifa wa Kupambana na UKIMWI na Magonjwa ya Zinaa.)

UNAIDS United Nations Programme on HIV/ AIDS. (Ushirika wa Kimataifa katika Mipango ya Kupambana na UKIMWI.)

(7)

IKISIRI

Lengo la kazi hii ni kuchanganua uwiano wa maana za picha na matini katika mabango ya matangazo ya UKIMWI kwa kuzingatia tathmini za wapokezi. Watafitiwa ambao walishirikishwa katika utafiti huu waliteuliwa kutoka maeneo ya Githurai na Kiandutu katika wilaya ya Thika, Vitengo vya watu wenye umri, kazi, elimu, tajriba, falsafa na mielekeo tofauti vilihusika. Kwa kurejelea misimbo ya nadharia ya Semiotiki kwa mujibu wa Barthes uchanganuzi wa ishara zote za kisanaa na kiisimu katika mabango thelathini na matano yanayohusu ugonjwa hatari wa UKIMWI yamechanganuliwa.

Kazi hii imegawanyika katika sehemu tano. Sura ya kwanza imetanguliza kazi yote kwa kuangazia mada ya utafiti, maswali, malengo, upeo na mipaka ya utafiti. Mengine yaliyoshughulikiwa katika sura hii ni misingi ya nadharia, tahakiki za maandishi yanayohusiana na mada hii, ukusanyaji na uwasilishaji wa data. Sura ya pili imeshughulikia viunzi vya matangazo kwa nia ya kupata maana msingi katika mabango ya UKIMWI, kwa kutalii yale yanayojidhihirisha wazi pasi kuhusisha tajriba, mielekeo na falsafa za mtu binafsi na za kijamii. Sura ya tatu, imeangazia ujumbe katika mabango ya matangazo ya UKIMWI pamoja na kuhakiki dhamira za miguso tofauti. Uhakiki huo uliegemea upande wa yaliyomo kwenye tangazo kama vile: mada, maudhui, wahusika, pamoja na msuko wa picha na matini kwa kurejelea maoni ya watafitiwa.

(8)

YALIYOMO

Ukurasa

Mada

i

..

Ungamo 11

b

k

...

Ta aru u

111

Shukrani

:

iv

Maelezo ya Istilahi v

Vifupisho .

......•••.•.•....••...•.••..•.•.••.••..• ~

.

lki . .

..

slrl ~l

...

Ya

iyomo

V111

SURA YAKWANZA: UTANGULIZI

1.0

Usuli wa Utafiti

c

1

1.1 Swala la Utafiti 5

1.2

Maswali ya Utafiti

.

7

1

.

3

Malengo ya Utafiti

.

7

1

.

4

Tahadhania 8

1

.

5

Sababu za Kuchagua Mada

8

1.6

Upeo na Mipaka ya Utafiti

.

10

1.7 M··

ismgi

.ya N

a

dh

arra

.

11

1.8.0

Udurusu wa Maandishi

.

16

(9)

1.8.2

Tafiti katika Lugha Zingine

18

1.8.3

Tafiti katika Lugha ya Kiswahili..

22

1.9.0

Mbinu za Utafiti

25

1.9.1

Sampuli

26

1.9.2

Ukusanyaji wa Data

28

1.9.3

Uchanganuzi wa Data

28

1.9.4

Uwasilishaji wa Data

29

SURA YA PILI: VIUNZI VYA MATANGAZO

2.1.0

Picha na Ishara

31

2.1.1

Maana za Picha na Ishara

34

2.2.0

Vichwa Vikuu

41

2.2.1

Matangazo Yanayoshirikisha Vichwa Vikuu

-41

2.2.2

Matangazo Yasiyo na Vichwa Vikuu

-47

2.3

Wakala wa Tangazo

54

SURA YA TATU: UJUMBE KATIKA MATANGAZO

3.1.0

Ujumbe katika Picha na Matini..

63

3.1.1

Maafa ya kuambukizwa UKIMWI

69

3.1.2

Matumizi ya Kondomu

79

3.1.3

Ususiaji wa Ngono

88

(10)

3.1.5

Hiari katika Ushauri na Uchunguzi..

96

SURAYANNE: UWIANOWA MAANANAUJUMBE

4.1.0

Uangavu

106

4.1.1

Amali ya Anwani

.

107

4.2.0

Matini Ndefu

118

4.2.1

Kiashiria

119

4.2.2

Kihimili Maana

121

4.2.3

Kielekezi

.

123

4.2.4

Kihisishi

.

128

4.3

Muktadha

132

4.4.0

Muwala na Mshikamano

134

4.4.1

Mshikamano Tegemezi

.

136

4.4.2

Mahusiano Linganuzi

.

140

4.5

Uakifishi

.

142

4.6.0

Tamathali za Semi

.

145

4.6.1 Stiari 145

4.6.2

Usafid

i.

146

4.7.0

Mbinu za Kipekee

150

4.7.1

Takriri

.

150

(11)

4.8.0

Kuchanganya Msimbo

156

4.8.1

Kujitambulisha na Jamii- Lugha

157

4.8.2

Kurejelea Dhana

159

4.8.3

Mwingiliano wa Mifumo- Lugha

160

SURA YA TANO: HITIMISHO

5.1.0 Matokeo ya Utafiti 171

5.2.0

Mahitimisho ya Utafiti..

176

5.3.0 Mapendekezo

179

]V(Cllr~j~l~()•••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••1~1

(12)

SURA

YA KWANZA

UTANGULIZI

1.0

Usuli wa Utafiti

Mawasiliano ni kipengele muhimu zaidi kinachodhihirisha ustawi wa teknolojia na sayansi katika nchi yoyote He. Mawasiliano mwafaka yanahitajika ili kuharakisha uimarishaji wa afya ya jamii. Maendeleo na uvuvumkaji wa nchi yoyote hutegemea afya ya wananchi wake na uwezo wa wananchi kukabiliana na jukumu la ujenzi wa

taifa (NASCOP2005).

Kuna ukosefu wa ujuzi na maarifa ya kujikinga na kuzuia magonjwa sugu yanayokuwa kikwazo katika ujenzi wa taifa. Kumakinisha mtu na jamii kwa jumla ni jukumu la wizara ya afya, mashirika ya kiserikali na yasiyo ya kiserikali ambayo yanahusiana moja kwa moja na ustawi wa afya ya mtu binafsi au jamii kwa ujumla

(NACC2005).

Mwaka 1999 mwezi Desemba, ugonjwa wa UKIMWI ulitangazwa kuwa janga la kitaifa, kutokana na jinsi ulivyoangamiza watu wengi nchini. Kwa mujibu wa ripoti ya NACC (2005), katika muda wa dakika tano, ugonjwa huu sugu, huangamiza watu watatu. Idadi ya watu wanaokufa kutokana na UKIMWI ni takribani watu

105,000 kila mwaka. Hii ni idadi ya zaidi ya watu 350kwa kila siku (NACC2005).

Ugonjwa huu unaendelea kuangamiza mamilioni ya watu kila uchao. Kwa mujibu

(13)

wanawake, wanaume na watoto wanaoishi na virusi vya UKIMWI wakati huu.

Zaidi ya asilimia 95 wakiwa katika mataifa yanayoendelea. Nchini Kenya, mmoja

kati ya kila watu tisa ana virusi vya UKIMWI. Idadi ya visa hivi inazidi kuongezeka

kutoka 10,000 mnamo 1987 na kufikia visa 96,000 vipya, mnamo 2003. Hili ni

ongezeko la zaidi ya mara kumi katika kipindi cha miaka 15.

Katika harakati za kumakinisha umma, mbinu nyingi za mawasiliano hususan

mabango yanayoangikwa katika maeneo tofauti zimetumika. Matangazo ya

UKIMWI katika mabango ni njia ambayo imehusisha masuala tofauti katika

mazingira ya wasanii mbalimbali, kwa kusudi la kuzindua, kushawishi,

kutahadharisha, kufahamisha, kuelimisha na kurekebisha mielekeo na mitazamo

ya wananchi. Mashirika mengi ya kiserikali na yasiyo ya kiserikali yamechukua

hatua ya kutumia mabango kama mkondo wa uwasilishaji wa masuala nyeti

nchini. Mkondo huu wa uwasilishaji wa ujumbe umewezesha wananchi kuusoma

ujumbe mara kwa mara wapitiapo mahala palipoangikwa mabango

yanayotangazia masuala mbalimbali. Hivyo njia hii imejibainisha kama yenye

uwezo wa kutahadhalisha na kudhibiti mielekeo ya wananchi.

Suala hili la utangazaji hufuma majukumu mapya kufungamana na maisha na

maendeleo ya jamii kwa mujibu wa wakati. Matangazo ni kipengele muhimu

katika mfumo wa kumakinisha umma ill kumaizi mengi yanayowazunguka. Hili

litaweza tu kutokea pale tu, maana na ujumbe unaolengwa na mwasilishi

unamfikia mpokezi pasi utata au upotoshi. Kuwasilisha dhana fulani kwa jamii

(14)

la ugonjwa sugu wa UKIMWI lafaa kuzingatiwa kwa uwazi zaidi kwa vile

limefungamanishwa na masuala ambayo jamii nyingi huyaona mwiko kuyataja

kwa udhahiri (Gachara 2005).

Msukumo wa utafiti huu ni kuchunguza uhusiano kati ya picha na matini katika

mabango ya UKIMWI. Mtafiti anachukulia kwamba maana halisi au ambazo

zinaibuliwa huweza kuzungukiwa na utata na upotoshi wa ujumbe iwapo

hakutakuwepo na uwiano wa ishara za kisanaa na ishara za kiisimu kwenye

mabango na pia iwapo picha na matini zitazua fasiri zaidi ya moja. Isitoshe

utoshelevu wa mabango ya matangazo ya UKIMWI utategemea ujuzi wa wananchi

wa kusoma na kujua yanayoelezwa.

Mtafiti amejaribu kutafuta ni kwa njia gani mabango ya matangazo ya UKIMWI

yanaweza kuwasilisha maana na ujumbe kwa njia toshelevu. Mtafiti amekusudia

kuwa kwa kubainisha wazi vigezo vya uwiano wa picha na matini katika

uwasilishaji wa maana na ujumbe katika mabango, utafiti huu umechangia katika

utatuzi wa matatizo yanayokumba taaluma ya mawasiliano hasa kuhusiana na

suala ibuka la ugonjwa wa UKIMWI.

(15)

Uamilifu wa taaluma ya semiotiki, katika uchanganuzi - miundo ya maana katika

kazi ulianza na wanaprague mwaka 1920-1930 hususan, Jan Mukaravosky. Hata

hivyo, semiotiki ilianza kutumikizwa katika uchanganuzi wa ishara na vielelezo

picha katika kazi ya Roland Barthes ya mwaka 1955. Kazi zake Barthes ziliipa

taaluma ya semiotiki msukumo mkubwa katika uchanganuzi wa maana za ishara

alipoainisha fasiri za maana katika Pasta ya Panzani (Tanaka, 1994). Kwa mujibu

wa Barthes, matangazo huwasiliana na wapokezi kwa nia ya kuwapasha ujumbe na

maana fulani. Matangazo ni mwafaka zaidi kama kichocheo cha fasiri za kisemiotiki kwa vile huhusisha ishara za kiisimu na pia kisanaa katika kufikisha

ujumbe kwa hadhira. Mtazamo wa kisemiotiki unafaa zaidi katika kufasiri maana

na ujumbe, kueleza utaratibu na njia za ubunifu na uzuaji wa maana na pia

matatizo ya ufasiri, katika matangazo.

Barthes (1964) anaeleza kuwa, mfumo wa ishara kama vile picha, vielelezo,

michoro na hata lugha hushughulikiwa kama vipengele vinavyozua ujumbe na

fasiri mbalimbali za maana. Picha huchunguzwa kama mfumo lugha, na lugha

huchunguzwa kama mfumo ishara. Hivyo mifumo ya kiisimu na mifumo ya

kisanaa huchunguzwa kama mifumo ya kiishara inayotegemeana katika kuibua

mifumo ya maana na ujumbe.

Wazo hili linashadidiwa na Gombrich (1977) anayesisitiza umuhimu wa kuangalia

picha na ishara zinazornzunguka mwanadamu katika vipengele vyote vya maisha.

(16)

Umuhimu wa picha umo katika uwezo wake wa kuwasillsha ujumbe ambao

haungesimbwa kwa njia nyinginezo. Katika kazi zinazohusisha ishara anuwai,

mtazamo wa kisemiotiki huchunguza amali na uamilifu wa kila kipashio cha

ishara, na kuvifungamanisha katika kukamilisha uzima wa mifumo ya maana na

ujumbe kikamilifu.

Mtazamo wa kisemiotiki unachukulia kuwa katika mawasillano huwa kuna ishara

zinazosimbwa, na ung'amuzi wa maana na ujumbe wa ishara husika utafikiwa pale

tu ishara zenyewe zitasimbuliwa ipasavyo (Barthes, 1986b). Barthes anadokeza

kuwa, kuna aina tatu za ishara za kisemiotiki zinazochangia fasiri za maana na

ujumbe: ishara za kiisimu au umbo lugha linalowakilisha dhana katika mfumo

lugha, hizi huwa ni kigezo bainifu; ishara-lugha fiche na stiari picha. Ishara hizi

husimba maana na ujumbe ambao husimbuliwa tu na wapokezi kwa mujibu wa

tajriba na amali mbalimbali za kijamii. Ni katika mkabala huu, tumetathmini umuhimu wa ishara za kisanaa ambazo zinafanikisha mawasiliano sawa na ishara

za kiisimu.

1.1Swala la Utafiti.

Utafiti huu umechanganua uhusiano kati ya picha na matini katika mabango ya

matangazo ya UKIMWI. Tumetathmini uwiano kati ya maana za picha na matini

katika mabango ya matangazo ya UKIMWI. Mtafiti ameibusha kutokana na matini

na picha miktadha tofauti inayozalisha uwiano wa maana na ujumbe katika

mabango ya UKIMWI. Kipengele hiki cha ishara za kisanaa kama vile picha

(17)

kubeba maana na ujumbe. Watafiti wengi kama vile, (Ojwang 1986, Michira 1993, Aloo 2002), wamebobea katika kipengele cha matangazo ya biashara kwa kuzingatia zaidi mwingiliano wa matini na muktadha. Katika tafiti zilizotangulia, uwiano kati ya picha na matini haujaonyeshwa namna unavyofanikisha mawasiliano kwa kuimarisha ufasiri wa maana na ujumbe unaofikia hadhira.

(18)

1.2 Maswali ya Utafiti.

Uafiti huu umeongozwa na maswali haya:

• Je, picha na matini zilizotumika katika mabango ya matangazo ya UKIMWI,

zinawasilisha ujumbe na maana sawa?

• Msuko wa picha na matini katika mabango ya matangazo ya UKIMWI

umefanikisha vipi ufasiri wa maana na ujumbe?

• Ni vigezo vipi vya uwiano wa picha na matini vinavyofanikisha ufasiri wa

maana na ujumbe?

• Ni mbinu zipi zinazoweza kuboresha ufasiri wa maana na ujumbe katika

mabango ya matangazo ya UKIMWI?

1.3 Malengo ya Utafiti

• Kuchanganua picha na matini zilizotumika katika mabango ya matangazo

yaUKIMWI.

• Kuchanganua namna muundo wa picha na matini unavyofanikisha ufasiri

wa maana na ujumbe.

• Kutathmini vigezo vya uwiano wa picha na matini vinavyofanikisha ufasiri

wa maana na ujumbe.

• Kutoa mapendekezo ya namna ya kuboresha ufasiri wa maana na ujumbe

(19)

1.4 Tahadhania

• Kuna uwiano kati ya matini na picha katika mabango ya matangazo ya

UKIMWI.

• Kuna utata wa maana za picha na matini katika mabango ya matangazo ya

UKIMWI.

• Msuko wa picha na matini hufanikisha, ufasiri wa maana na ujumbe katika

mabango ya matangazo ya UKIMWI.

• Mabango kama mkondo wa mawasiliano yanaweza kuboreshwa zaidi ili

yawasilishe maana na ujumbe kwa njia mwafaka.

1.5 Sababu za Kuchagua Mada

Utafiti huu umefanywa kwa kuzingatia kwamba matangazo ni kipengele muhimu

kinachohusika katika kuizindua, kuishawishi, kuimakinisha, kuiongoza na

kuirekebisha mielekeo na mitazamo ya jamii. Matangazo huhusisha masuala

mbali- mbali katika nyanja tofauti - siasa, elimu, afya na maadili katika mifumo ya

kijamii.

Matangazo yamekuwa kwa kiwango kikubwa dhihirisho la ulimwengu

unaobadilika haraka mno hasa katika maendeleo ya kisayansi na teknolojia ya

mawasiliano. Ni katika sajili hii ya matangazo, tunaweza kuona jinsi lugha

inavyopanuliwa ili kupambana na mabadiliko kwa mujibu wa uhalisi wa maisha ya

(20)

Mtafiti amezingatia mabango ya matangazo ya UKIMWI yaliyoandikwa kwa Kiswahili kwani anachukulia kuwa lugha ya Kiswahili ni lugha ya wote- wasomi na wasiosoma. Lugha hii ina uwezo wa kuhamasisha wote kuhusu masuala ibuka kama vile ugonjwa wa UKIMWI kwa kuwa hutumika na hueleweka na idadi kubwa

ya watu nchini. Isitoshe, Kiswahili ni lugha ya taifa na pia ndiyo lugha inayotumiwa na Wakenya wengi katika mawasiliano. Mbali na hayo, mabango kama njia ya utangazaji, yanaweza kutapakazwa kote nchini na hivyo kufikia idadi kubwa ya watu katika maeneo tofauti .

(21)

amechukulia kuwa mabango ni njia ya utangazaji inayoweza kutanda kote nchini katika kuhamasisha wananchi kuhusu ugonjwa wa UKIMWI na kwa hivyo palikuwa na haja ya kutathmini utoshelevu wake kama njia mojawapo ya mawasiliano inayohusisha ishara za kisanaa pamoja na zile za kiisimu.

1.6 Upeo na Mipaka ya Utafiti

Ingawa njia za utangazaji kuhusu suala la UKIMWI ni nyingi, utafiti huu umelenga tu mabango pekee, yaliyotundikwa kwenye barabara, vituo vya afya na maeneo mengine tofauti nchini. Mabango yameteuliwa kutokana na uwezo wa njia hii ya utangazaji kufikia idadi kubwa ya watu katika maeneo tofauti. Vilevile uteuzi wa mabango umezingatia kusudi la mtafiti la kutathmini utaifa katika upokezi wa matangazo ya UKIMWI. Picha na matini za mabango ya matangazo ya UKIMWI zimetathminiwa ili kuchunguza fasiri za maana za wapokezi tofauti kwa vile hili ni suala linaloathiri kila mtu kwa njia moja au nyingine nchini. Mtafiti amejikita tu

kwa fasiri za wapokezi kwa vile mabango hayo yanaashiria wasomaji tofauti na msomaji ndiye wa mwisho aliye na nafasi na mchango katika kuyachambua na kuelewa maana. Hivi ni kusema kuwa, nia na maoni ya waasilishi wa mabango husika hayakuakisiwa na utafiti huu.

Mabango yamechanganuliwa, kwa kuzingatia maudhui tofauti yanayozingatiwa na

(22)

ushirika wa wote katika kuangarniza UKIMWI. Kwa kila kitengo mabango saba yameshughulikiwa. Jumla, mabango thelathini na matano yaliyoendelezwa zaidi kwa lugha ya Kiswahili yamechanganuliwa. Katika mabango mengi imebainika kuwa hata iwapo lugha ya Kiswahili ilihusishwa pakubwa, vilevile maneno ya Kiingereza na Sheng yalichopekwa. Maneno au kauli zilizochopekwa zimetolewa kisawe chake katika Kiswahili na kuchanganuliwa. Hata hivyo, mtafiti hakuhusika katika kurekebisha mifumo ya sarufi na makosa ya hijai yaliyojidhihirisha katika

matangazo kama vile- *mjaa-rnzito. Mifumo yote ya mawasiliano ikiwemo ishara za kiisimu na kisanaa imeehanganuliwa jinsi ilivyojitokeza katika tangazo ili kudhihirisha fasiri za maana.

1.7

Misingi ya Nadharia

Nadharia ambayo ni mwafaka zaidi na ambayo imetoa msingi maridhawa wa uchanganuzi wa picha na matini katika mabango ya matangazo ya UKIMWI ni nadharia ya semiotiki. Semiotiki ni neno lililotoholewa kutoka neno lenye asili ya Kiyunani lenye maana ya uhakiki wa ishara. Hii ni nadharia yenye historia ndefu, yenye mielekeo ya uchunguzi wa ishara iliyozuka katika karne ya tano, wakati wa

(23)

Kushika kasi kwa nadharia ya semiotiki katika miaka ya 1960-1970 kumeambatana

na mwelekeo wa kuuasi na kuacha umuundo, ulioonekana kama uliofungika au

usiobadilika (Royle, 1995). Mikabala hii inahusishwa sio tu na Jacques Derrida,

mbali pia na wahakiki wengine kama Julia Kristeva, Michael Foucalt, Jacques

Lacan, Loius Althusser na Paul De Mann (Blamires, 1991). Nadharia ya semiotiki

katika kuangaza suala la uashiriaji humulika jinsi kazi hizo zinavyowasiliana na

wasomaji. Nadharia hii inajishughulisha na jinsi mpokezi anavyoipokea kazi fulani

anayoisoma (Innis, 1985).

Nadharia hii haisisitizi tu masuala ya kifasiri au jinsi tunavyofasiri kazi fulani tu

mbali pia usomaji wetu wa kazi na kujiuliza kwa nini kazi hizo huwa na maana

zilizo nazo kwa wasomaji tofauti. Kama wanavyosema Andrew Bennet na Nicolas

Royle (1995), jamii hushiriki mfumo wa kanuni na taratibu zinazokubalika na

jamii husika. Jamii moja huweza kutumia ishara za aina sawa na kuelewana katika

ufasiri wa maana na ujumbe. Hata hivyo ufasiri hutofautiana kwa watu binafsi.

Kwa mfano, neno 'mvinyo' linapotajwa huenda likatoa wazo au ishara tofauti

miongoni mwa watu wenye tajriba tofauti.

Aidha, kama wasemavyo wahakiki wa Chuo Kikuu cha Yale - Geoffrey Hartman, Hillis Miller, Paul De Mann na Harold Bloom, kuna uwezekano wa matini kuwa na

fasiri nyingi zinazolingana au kukinzana na zote zikakubalika. Mhakiki ana wajibu wa kupasua ishara za kisanaa na kiisimu,vipengele vyake vyote ili kuweka wazi

(24)

matumizi ya kiashirii na kiashiriwa chake na maana yaks huhamishwa au

huahirishwa (Blamires, 1991).

Licha ya nadharia ya semiotiki kufaidi na mikabala hiyo, imefaidi pia kutokana na

mawazo ya mwana-isimu wa Ki-Swizi, Ferdinard de Saussure, pamoja na

mwanafalsafa wa Ki-Marekani anayejulikana kama Charles Pierce (1977). Pierce

anahusishwa na kielelezo cha ishara kinachohusishwa na pembe tatu: ishara,

yambwa na kifasiri. Zingatia mchoro unaodhihirisha aina hizo za ishara kwa

mujibu wa Pierce ambao tofauti na mchoro wa Ferdinard de Saussure uliozingatia

zaidi isimu huu umejikita kwa ishara za kisanaa.

Ishara

Yambwa Kifasiri

Kwa mujibu wa mwanafalsafa huyu, kila ishara huwa na yambwa au kitendwa

kinachorejelewa. Kifasiri ni kile kinachochochewa katika akili ya anayefasiri ishara

hiyo. Pierce anaamini kuwa kila ishara ina misingi inakotegemezwa ili kufasiriwa

kwake kuwezekane. Misingi hiyo huzua ishara aina tatu: kielekezi, ishara stiari na

taashira. Misingi hii mitatu ya ishara itawekea misingi ya uchanganuzi wa matini

(25)

kudhihirisha fasiri nyingi za maana na ujumbe. Mtafiti ameweza kuhakiki kwa

kina ishara tofauti zilizoko katika mabango tofauti na kutambua maana

zinazosemwa wazi na kudhihirisha jinsi zinavyopingana ki-itikadi na yasiyosemwa

wazi.

Mhakiki mwingine aliyewekea misingi nadharia hii ni Barthss (1964, 1977, 1981,

1984b, 1986b). Barthes, anadokeza kuwa, lengo kuu katika kuhakiki matini, ni

kuivunja katika sehemu ndogo alizoziita leksia. Hivi ni kama vitengo vidogo vya

usomaji vinavyodhihirisha misimbo au kanuni fulani ambazo huwa muhimu

katika kuifasiri kazi fulani. Alizitambua aina tano kuu za misimbo ambazo

zitawekea misingi maridhawa utafiti huu.

Kwanza, kuna msimbo wa matukio. HUll unahusu msuko wa kazi. Msimbo huu

umemsaidia mtafiti katika uhakiki wa usanii wa picha na matini katika mabango

ya matangazo ya UKIMWI, na kutathmini jinsi picha zinavyoambatishwa kwenye

matini ki-athari na ki-sababishi,

Pili, ni msimbo wa kihemenitiki. Huu unahusu uchunguzi wa matendo ya

binadamu kama vile - upendaji, uchukiaji wa kazi kutokana na taharuki

zilizojengwa. Msimbo huu umemsaidia mtafiti katika kuchunguza kufumbatwa

kwa maana katika viunzi mbalimbali vya tangazo na namna vinavyojengeana

katika kutaharukisha wapokezi katika ufasiri wao wa maana na ujumbe. Msimbo

(26)

Tatu, kuna msimbo wa kisemu. Neno semu hutumika kuzielezea sifa bainifu za kisemantiki. Hizi ni sifa zinazotuwezesha kuipata picha fulani katika kazi, kwa

kuibua fahiwa za maana. Msimbo huu umemwezesha mtafiti kufafanua picha na

matini kwa kutumia unasibishi wa maana kwa kiwango kikubwa. Aidha,

umetuwezesha kugundua kuwa maana nasibishi ina uzito kuliko maana msingi ya

maneno, kwa vile hufafanua yale yasiyosemwa wazi na maneno, ishara na picha

katika mabango tuliyoyashughulikia ya UKIMWI.

Nne, upo msimbo wa ki-ishara. Huu ni msimbo muhimu katika usomaji na uhakiki wa kazi yoyote. Ishara huwakilisha viashiriwa fulani. Uhusiano kati ya ishara na kiashiriwa hujengewa na dhana zilizoko mawazoni. Msimbo huu umemsaidia mtafiti kutathmini viwakilishi na viwakilishwa vya maana katika

mabango ya matangazo ya UKIMWI.

Tano, kuna msimbo wa kirejelezi. Msimbo huu unajengwa kutokana na viashirii vya utamaduni na tajriba ya maisha. Kiashirii huweza kuwa kile kile bali

kinachorejelewa kikawa tofauti kwa mujibu wa utamaduni na tajriba ya maisha.

Msimbo huu umeupa utafiti huu nguzo imara katika kutathmini jinsi wapokezi wa

mabango ya matangazo ya UKIMWI nchini wanavyofasiri maana na ujumbe kwa

mujibu wa tajriba zao za maisha na falsafa za kitamaduni na kijamii.

Misimbo hii ya nadharia ya semiotiki imemsaidia mtafiti kuibusha fasiri tata

katika picha na matini za mabango ya matangazo ya UKIMWI. Aidha, kwa

(27)

ya UKIMWI mtafiti ameweza kujumulisha maoni ya watafitiwa ili kupendekeza

namna ya kuboresha mabango yanayohusu masuala ibuka kama suala la UKIMWI

nchini.

1.8.0

UDURUSU

WA

MAANDISHI

Udurusu huu utahusu maandishi ya kijumla kuhusu semiotiki, tahakiki za tafiti

bayana za lugha zingine na kisha tafiti katika lugha ya Kiswahili.

1.8.1MaandishiyaJumla kuhusu Semiotiki

Semiotiki kama ilivyosemwa hapo awali, ni utohozi wa neno linalotokana na lugha

ya Kiyunani lenye maana ya ishara. Neno hili linatokana na muungano wa

maneno mawili. Maneno haya ni 'Logos'(maneno) na Semeion (yanayohusiana na

ishara). Hivyo semiotiki ni sayansi inayojihusisha na mifumo ya ishara na

uashiriaji. Baadhi ya wataalamu wanaiita semiolojia badala ya semiotiki.

Watalamu wengi kama vile: Pierce 1931, 1977, Stokoe 1972, Voloshinov 1973,

Guiraund 1975 Eco 1976 Barthes 1964, 1977, 1984b, Innis 1986 wamekubaliana

kuwa semiotiki hujishughulisha na namna waandishi wanavyowasilisha ishara

zinazofumbata na kusimba maana, hivi kwamba wasomaji wanafanya juhudi

kupata na kusimbua maana iliyosimbwa.

Ishara zote ziwe za kiisimu au za kisanaa hushughulikiwa kisemiotiki. Ishara hizo

huwa na maana iliyo dhahiri. Maana hii dhahiri hurejelewa kama maana halisi au

maana msingi ya ishara. Maana hii haihusishwi na hisia au mahusiano

(28)

kijamii. Mtazamo wa kisemiotiki uliohusiana na mwana isimu wa kiswizi,

Ferdinard de Saussure, ulijikita zaidi katika maana hii msingi bila kuingilia maana

batini ya ishara husika.

Wataalamu kama vile: (Pierce 1931, Eco 1976, 1977, 1978 , Barthes 1977, Innis

1986) wanahusisha ishara na maana msingi na pia maana batini kwa kuegemea

mantiki. Maana msingi wanasema ni kile kilichomo katika matini, picha, mchoro,

kibonzo, bango na kadhalika. Maana batini husimbuliwa na mpokezi kwa kufasiri

namna picha, mchoro, kibonzo au bango husika lilivyosawiriwa. Hata hivyo

wanasema kuwa maana hizi huingiliana hivi kwamba hakuna mipaka mwafaka

inayoweza kuwekwa waziwazi. Hili linatokana na wazo linaloelezwa na Voloshinov

(1973: 105) ya kuwa, maana msingi ni gari la kusafirishia fasiri za maana batini na

nasibishi, hivi kwamba ung'amuzi na ufasiri wa maana hizi hauwezi

kutenganishwa kwa njia yakinifu.

Semiotiki husaidia kuangazia ufasiri wa maana kwa kuwa ishara haziwasilishi tu

maana lakini huwa zenyewe kifaa cha kuibulia maana. Ishara lazima ziwasiliane na

kuwasilisha maana pale tu, wapokezi wenyewe watajishughullsha kwa mapana na

marefu kupata na kusimbua maana kwa vile haziwasiliani kidhahiri.

Ni kutokana na sayansi hii inayojishughullsha na ishara, tunatambua kuwa lugha

zote hukusudia kuwasiliana lakini sio mawasiliano yote hutokea kutokana na

lugha. Barthes (1984b) amedhihirisha mchango wa semiotiki katika kuhusisha

(29)

Semiotiki, hivyo basi hutudhihirishia kuwa hakuna njia ya mawasiliano inayofaa

kudunishwa au kuonekana bora zaidi ya nyingine. Ukweli ni kuwa maana haiwi

katika njia au mkondo wa mawasiliano kama vile, matini, bango, picha na

kadhalika. Maana hupatikana tu iwapo imewekezwa na kukabidhiwa kwa ishara

fulani ya kisanaa au ya kiisimu. Hakuna kitu ambacho ni ishara hadi pale

tunakifasiri kama ishara. Chochote kinaweza kuwa ishara iwapo kinachukuliwa

kama chenye uashiriaji fulani. Hivi ni kusema kuwa ishara na uashiriaji

huambatana na hali kubalifu za mahusiano ya ishara kwa mtu binafsi na jamii

kwa ujumla. Semiotiki imeainishwa katika mitazamo kama vile:

Semiotiki jumu1ifu inayoshughulikia nyanja zote zinazohusisha ishara na

uashiriaji.

Semiotiki ya ldjamii inayohakiki ishara na kuzihusisha na mitazamo na

falsafa za kitamaduni na kijamii. Uchanganuzi huu hutuwezesha kufahamu

kuwa tofauti katika ufasiri wa maana za ishara hutokana na mawazo na hali

kubalifu za mtu binafsi na zile za kijamii zinazopokezanwa kizazi hadi

kizazi na hutofautiana kutegemea tamaduni mbalimbali.

Semiotiki mawasiliano. Huchanganua matini za televisheni, radio,

filamu, vibonzo, magazeti, matangazo katika majuzuu na mabango na picha

ili kusimbua maana zilizosimbwa. /

Mitazamo hii ndiyo dira inayotawala na kuelekeza utafiti wetu.

1.8.2 Tafiti katika Lugha Zingine

Hams ndiye mtaalamu wa kwanza kuwekea msingi utafiti katika uwanja wa

(30)

lugha ya utangazaji aligundua kuwa lugha hutokea katika muungano fulani na

hivyo basi akatafiti aina za miungano hiyo kwa kutumia mtazamo wa uchanganuzi msambao. Utafiti wake ulihusisha kipengele cha mshikamano katika mipangilio ya

kauli au sentensi katika matangazo ya biashara. Utafiti huu umejengea utafiti wetu

hasa katika kuchunguza mipangilio ya maneno katika matini zilizoko katika

mabango ya matangazo ya UKIMWI, ili kubainisha maana kinzani na fasiri tata.

Tofauti iliopo ni kuwa, utafiti huu haukuzingatia tu mshikamano wa matini pekee

bali umechunguza:

• Utendakazi wa matini.

• Maana na ujumbe unaowasilishwa na matini.

Isitoshe, mbali na kuzingatia kipengele cha lugha ya maneno (ishara za kiisimu),

utafiti huu umeshughulikia ishara zisizo za kiisimu kama picha na ishara, ambazo

zina uwezo wa kuwakilisha maneno zaidi ya elfu moja katika uwasilishaji wa

maana na ujumbe.

Lambert (1989) alifanya utafiti juu ya sarufi na uamilifu wa muktadha katika

matini. Alinuia kueleza mwingiliano wa sarufi na muktadha katika kutunga na

kufasiri matini kimuktadha. Alifanya hivyo kwa kuzingatia vigezo vya uchanganuzi

wa muktadha kisha akaainisha aina za miktadha inayobuni matini mbalimbali.

Utafiti huu unahusiana na utafiti wake kwa sababu unatafiti muktadha kama

mojawapo ya vipengele vinavyochangia ung'amuzi na ufasiri wa maana na ujumbe katika matini na picha katika mabango. Hata hivyo, utafiti wetu haukujikita katika

(31)

kigezo toshelevu cha kuibua maana ya ujumbe, bali kuna vigezo vingine vingi

vinavyochangia ung'amuzi na ufasiri wa maana na ujumbe katika matini na picha

(Guiraund.uczs).

Wataalamu wengine kutoka maeneo mengine waliosaidia kuwekea msingi utafiti

huu ni Vestergaard na Schr0eder (1985). Katika kazi yao, wamedhihirisha kuwa lugha ya matangazo ya kibiashara huambatana na hali, wakati mielekeo na

matarajio ya jamii. Lugha inayotumika kushawishi na kuiathiri jamii kuhusu

bidhaa fulani huzingatia bidhaa zenyewe zinazotangazwa, zinalenga hadhira gani

-kiumri, kiellmu, jinsia na daraja la kiuchumi. Wanaeleza namna lugha

inavyotumiwa katika matangazo ya biashara ill iweze kutimiza malengo fulani.

Watangazaji wanazingatia suala la mahitaji ya kijamii ya hadhira yao ill kuweza

kuyatumia mahitaji yale kuiathiri na kuishawishi hadhira ile. Kazi hii imekuwa

muhimu katika utafiti wetu. Tofauti ni kuwa walishughulikia kipengele cha

matangazo ya kibiashara ilhali utafiti wetu umejikita zaidi katika kipengele cha

matangazo ya huduma, hususan huduma za afya katika jamii.

Mtafiti mwingine aliyeshughulikia swala la utangazaji ni Inglis (1972) anayesema kwamba matangazo ya biashara huunganisha bidhaa au huduma zinazotangazwa

na mielekeo na matarajio ya jamii husika. Kuweza kuathiri na kushawishi jamii,

tangazo lolote linafaa kuzingatia hall na hisia za hadhira kuambatana na mazingira

na muktadha wa wakati na utamaduni. Kazi hii imekuwa nguzo imara ya utafiti

wetu, tofauti ni kuwa alizingatia matangazo ya biashara ilbali utafiti wetu

(32)

Mtafiti mwingine aliyechanganua lugha ya matangazo ya biashara ni Barthes (1984b). Aligundua fasiri tata na polisemi za maana katika matangazo na

akapendekeza matumizi ya lugha elekezi inayoambatana na misingi ya jamii

husika. Judith Williamson (1983) alichunguza maana ambazo hazisemwi wazi katika matangazo. Maana hizi nasibishi huibuliwa na wapokezi wa matangazo

yenyewe. Tanaka (1994) alitathmini utata katika matangazo unaoweza kuibua

farakano kati ya hali halisi, miongoni mwa hadhira na jamii kwa ujumla kutokana

na fasiri potovu. Forceville (1996) alichunguza stiari picha katika matangazo ya biashara katika mabango kutoka nchi mbalimbali kama vile: Ulaya, Ujerumani, Ufaransa na kadhalika. Alikusudia kudhihirisha kuwa picha hubeba tamathali

kadhaa zikiwemo tashibiha, stiari, jazanda na taashira. Tafiti hizi zote zimeupa

msingi imara utafiti huu. Tofauti ya tafiti hizo na utafiti huu ni kuwa, utafiti huu

umeshughulikia kipengele mahsusi cha utangazaji kinachoonekana kupuuzwa na

watafiti hao - kipengele cha matangazo ya huduma.

Gachara (2005) ameshughulikia lugha ambayo inatumiwa katika kampeini za

kuhamasisha umma kuhusu ugonjwa sugu wa UKIMWI. Alilinganisha na

kulinganua utoshelevu wa matini zilizoandikwa na zile za kiusemi katika uwasilishaji wa ujumbe kwa umma. Katika utafiti wake aligundua kuwa matini

zilizoandikwa zilikuwa toshelevu zaidi ya zile zilizokuwa katika hall ya usemi.

Utafiti wake umejengea utafiti huu kwa kubainisha ni nini kinachochofaa

kusemwa wapi, lini na kwa akina nani. Hata hivyo utafiti huu unatofautiana na

(33)

yaliyotolewa kwa Kikuyu hasa nyimbo na matangazo katika redio na televisheni.

Isitoshe utafiti wake ulikuwa jumulifu katika kuelezea utoshelevu wa matini zote

zilizoandikwa pasi kutujulisha ni gani illyo toshelevu zaidi na kwa sababu gani, na

zile ambazo si toshelevu ni nini hasa kinachofaa kufanywa ill pia ziwe toshelevu.

Utafiti wetu umechunguza kipengele kimoja mahsusi - mabango ill kutathmini

utoshelevu wake kwa watu wote nchini, kwa kuoanisha muktadha, ishara za

kiisimu na zile za kisanaa katika uibuaji wa maana na ujumbe.

1.8.3Tafiti katika Lugba ya Kiswabili

Kitsao (1975) alifanya utafiti wa kimtindo kuhusu maandishi katika uandishi wa

barua, magazeti na riwaya. Alitumia nadharia ya mtindo ill kubainisha mitindo ya

matumizi lugha katika viwango vya sarufi na semantiki. Utafiti huo umejengea

utafiti huu kwa kuzingatia usanii wa matini katika mabango, hasa kwa kuzingatia

kuwa, katika kuchunguza maana, msomaji anaanza kwa hatua ya kukisia maana za

kazi nzima. Msomaji hawezi kuzielewa au kuzifahamu sehemu za kitu (matini na

picha) bila kuelewa kitu kizima chenyewe, na pia hawezi kukielewa hicho kizima

bila ya kuzifahamu sehemu zake. Sehemu za kazi na ukamilifu wa maana

unategemeana. Tofauti, ni kuwa utafiti huu haujikiti kwa riwaya na magazeti na

barua ball umezingatia usanii wa matini na picha katika kufanikisha ung'amuzi na

ufasiri wa maana na ujumbe katika mabango ya matangazo ya UKIMWI.

Habwe (1999), alifanya utafiti kuhusu uchanganuzi usemi katika hotuba za

Kiswahili nchini Kenya. Alitumia mitazamo ya Halliday na Hassan (1976) na

(34)

sana katika hotuba hizo. Pia allgundua kwamba maana katika hotuba hizo huwa

zaidi ya maneno yanayotumiwa. Hivyo maneno yallbeba maana fiche. Wanasiasa

waligeuza maana ill kutosheleza hall tofauti, matarajio yao pamoja na yale

wanayoyadhania kuwa matarajio na mahitaji ya hadhira zao. Utafiti huo

umetumiwa kama msingi wa utafiti huu hasa katika kubainisha kuwa yasiyosemwa

wazi hupingana na yasemwayo wazi. Hata hivyo kazi hii imetofautiana na yake

kwani alishughulikia lugha ya kisiasa.

Michira (1993) allchunguza lugha ya wachuuzi na matangazo redioni. Utafiti wake

ulijikita katika misingi ya nadharia ya elimu-mitindo. Alishughulikia uteuzi na

matumizi ya msamiati katika mitindo hiyo miwili ya matumizi lugha. Aligundua

kuwa aina zote mbill za matumizi lugha huonyesha mchanganyiko wa misimbo,

sintaksia na lugha sahili ambayo ina makosa mengi ya kisarufi. Utafiti huu

umefaidi kutoka kwa utafiti huo hasa katika kubainisha mbinu, mikakati na

vipengele vya matini katika mabango, vinavyofanikisha ufasiri wa maana na

ujumbe. Kazi hii imetofautiana na utafiti huo kwa vile alishughulikia lugha ya

usemi.

Mtafiti mwmgme allyeshughulikia swala la matangazo ni Ojwang' (1986)

aliyechunguza matini za matangazo ya uajiri wa kazi katika magazeti. Ojwang'

alishughulikia matangazo kutoka magazeti na majarida matano, kutoka nchini

Kenya na kuchunguza jinsi lugha ya matangazo haya illvyokuwa kielelezo cha

muktadha wa mawasillano na utamaduni chipukizi wa mashirika na makampuni

(35)

wapi na kwa nani huathiriwa pakubwa na muktadha wa mawasiliano na

utamaduni wa wale ambao wanahusika (Dittmar, 1976).

Aloo(2002) alichunguza matangazo ya biashara katika redio na televisheni. Utafiti wake ulidhihirisha jinsi matangazo ya biashara yanavyoshawishi hadhira bila

kuifahamisha vya kutosha kuhusu bidhaa zinazotangazwa. Utafiti wake pia

ulidhihirisha mbinu mbalimbali za ushawishi pamoja na mbinu za lugha

zinazotumiwa na watangazaji katika matangazo ya biashara. Utafiti huo umejengea

utafiti huu hasa kwa kubainisha mbinu za lugha zilizotumika katika usanii wa

maandishi katika mabango ya matangazo ya UKIMWI. Tofauti ni kuwa utafiti

wake ulishughulikia matangazo ya biashara na hasa matangazo katika hali ya

usemi bali sio matini zilizoandikwa.

Uhakiki wa tafiti za humu nchini na ziIe za maeneo mengine, umebainisha kuwa

kipengele cha matangazo ya huduma kinafaa kushughulikiwa ili kudhihirisha

kama mbinu zinazotumika katika matangazo ya biashara hutumika pia kufanikisha

matangazo ya huduma. Aidha, tafiti nyingi zimechukulia kuwa lugha ya maneno

ndiyo pekee inayowasilisha maana na ujumbe. Imebainika kuwa tafiti hizi bayana

zimechunguza sifa na kanuni za muktadha na matini katika uwasilishaji wa maana

na ujumbe. Tafiti hizo zimetuwezesha kuona uhitaji wa kuchunguza ishara zisizo

za kiisimu kama picha na ishara za kisanaa, kama msingi wa uwasiIishaji wa

(36)

muktadha hazijashughulikiwa katika tafiti hizo ili kudhihirisha namna

vinavyochangiana na kutegemeana katika kuwasilisha maana na ujumbe.

1.9.0

Mbinu za Utafiti.

Utafiti huu ulihusisha mbinu za aina mbili.

Utafiti Maktabani ulihusu usomaji wa mapana wa makala, machapisho,

majarida na tasnifu zinazohusiana na mada yetu ya utafiti ili kuimarisha hoja za

utafiti huu. Vitabu ambavyo waandishi wameshughulikia matangazo tofauti

tofauti, makala yanayohusu uchanganuzi matini na yale yanayozingatia

uchanganuzi wa picha na ishara mbalimbali vimerejelewa. Mtafiti amerejelea pia,

vitabu ambavyo vinaelezea zaidi kuhusu nadharia ya semiotiki. Huduma za

mtandao zimemfaa vilevile.

Utafiti Nyanjani ulifanywa kwa nia ya kutathmini ufasiri wa maana na ujumbe

katika mabango ya matangazo ya UKIMWI kwa wapokezi tofauti tofauti.

Watafitiwa walioshirikishwa walitoka katika maeneo ya miji katika wilaya ya

Thika. Maeneo ya Thika yaliteuliwa kwa kuwa tarakimu zilidhihirisha kuwa, mji

huu una idadi kubwa ya maambukizo ya UKIMWI nchini ambayo ni 34% (NACC

2005). Maeneo yaliyoshughulikiwa ni Githurai kuwakilisha maeneo ya kimji yaliyo

na mseto wa watu wa makabila na biashara anuwai na maeneo ya Kiandutu

yaliyowakilisha maeneo yenye umaskini uliokidhiri. Hivi ni kumaanisha kuwa,

mtafiti alijaribu kupata fasiri za maana kutoka kwa watu wenye falsafa na mielekeo

tofauti nchini kwa kuwa suala la UKIMWI huhusishwa na hadhi ya kiuchumi, na

(37)

1.9.1Sampuli.

Mtafiti amechanganua mabango thalathini na matano kuambatana na mada kuu,

maudhui na malengo tofauti, kwa mujibu wa Baraza la Kupambana na UKIMWI

Nchini (NACC2005).

Mada

Matumizi Ya Kondomu

Ususiaji Wa Ngono

Maafa Ya UKIMWI

Kuishi Na Waliougua UKIMWI

Huduma Za HUU

Jumla

Idadiya Mabango.

7

7

7

7

7

35

Mabango haya yamekusanywa kwa njia mbili. Mabango yaliyotundikwa kwenye

barabara na maeneo mengine, na ni makubwa zaidi, yamepigwa picha. Pili, yale

madogo yaliyoangikwa katika maeneo tofauti; mtafiti ameyakusanya kwa minajili

ya uchanganuzi katika utafiti huu.

Hatua ya pili ilihusu uteuzi wa mabango mawili kutoka kwa kila kategoria

yaliyopatiwa watafitiwa walioteuliwa kwa kutumia mbinu kusudio kwa vile kuna

masuala mengi ambayo mtafiti alitilia maanani kama yaliyoweza kuathiri ufasiri

wa maana na ujumbe katika mabango husika. Mbinu ya hojaji ilitumika. Hojaji

iliyotumika katika utafiti huu ni hojaji wazi iliyomtaka mtafiti kuibua fasiri tofauti

(38)

iliandikwa na kuwasilishwa kwa watafitiwa kwa lugha ya Kiswahili kwani mtafiti

alichukulia kuwa, lugha ya Kiswahili inaweza kutumika kama chombo cha

mawasiliano nchini kwa wote. Sampuli ya watafitiwa waliohusishwa, walitoka

eneo la Thika kutokana na ithibati kuwa maenezi ya ugonjwa wa UKIMWI katika

eneo hili umekuwa janga kwa muda mrefu, Isitoshe, kwa mujibu wa ripoti ya

NACC(2005) inadhirisha wazi, kuwa miji yenye idadi kubwa zaidi ya maambukizo

ni kama vile: Thika - 34%, Busia - 29%, Nakuru - 26% na Kisumu - 29%. Katika

vituo vya kukagua akina mama waja- wazito, miji hii hususan mji wa Thika

umedhihirisha kiwango kikubwa cha maambukizo katika mwaka 1990-2004.

Mtafiti aliteua maeneo mawili ya Wilaya ya Thika - Githurai ikiwakilisha sehemu

za miji yenye mchanganyiko wa makabila mengi na pia kutokana na umaarufu

wake kama kituo cha biashara anuwai hivyo tulipata sampuli wakilishi ya vitengo

mbalimbali vya watu. Maeneo ya Kiandutu yaliteuliwa kuwakilisha maeneo duni

na yenye umasikini uliokithiri. Umaskini ni kigezo muhimu kinachodhihirisha

ukosefu wa maendeleo katika masomo na tajriba zinginezo zinazoathiri uwazaji wa

mtu na jamii kwa ujumla. Uchaguzi wa maeneo haya ulizingatia shabaha ya utafiti

hasa kuhusiana na ung'amuzi na ufasiri wa maana na ujumbe katika mabango ya

matangazo ya UKIMWI kuambatana na vitengo mbalimbali vya watu nchini,

wenye matarajio, mielelekeo na falsafa tofauti. Watafitiwa ishirini kutoka kila

eneo la Kiandutu na Githurai walishirikishwa, jumla ya watafitiwa waliotoa fasiri

(39)

1.9.2 Ukusanyaji wa Data.

Watafitiwa walikabidhiwa mabango kumi kila mmoja kati ya mabango yote thalathini na matano yaliyokuwa yamepigwa picha na kukusanywa, ili kuyatathmini na kuyafasiri. Fasiri zote za maana na ujumbe zilizoibuliwa zilijazwa kwenye hojaji wazi zilizokuwa zimetayarishwa na mtafiti. Wale ambao hawakuweza kusoma na kuandika, mtafiti aliwaongoza kwa kutumia hojaji hiyo hiyo.

1.9.3 Uchanganuzi wa Data

Mtafiti amechanganua picha na matini kwa kuongozwa na misimbo ya nadharia ya semiotiki kwa mujibu wa Barthes, (1964, 1977, 1981, 1984b) iliyokuwa dira ya kuongoza uhakiki wa:

• Yaliyomo katika mabango.

• Maana ashiriwa na maana husishi katika picha na matini kwa kurejelea maoni ya watafitiwa.

• Maoni na hisia za watafitiwa kuhusu maana wazi na maana fiche katika matini.

• Vigezo vya uwiano wa picha na matini.

Pili, mtafiti amechanganua miktadha inayosaidia katika ufasiri na welewa wa maana na ujumbe katika mabango. Maoni ya watafitiwa yamerejelewa ili kuondoa unafsishi wa maoni ya mtafiti. Fasiri na maoni ya watafitiwa kuhusu mabango ya UKIMWI yamekadiriwa kufuatia asilimia ya watafitiwa waliotoa mchango wao ifuatavyo:

(40)

X= Idadi ya watafitiwa wote arubaini.

Takwimu hizi zimechangia katika kudhihirisha fasiri za watafitiwa, ung'amuzi na

ufasiri wao wa mahusiano ya ishara, maana na ujumbe katika mabango ya

UKIMWIpamoja na hisia zao kuhusu picha na matini zilizoshirikishwa.

1.9.4 Uwasilisbaji wa Data

Matokeo katika tasnifu hii yamewasilishwa kwa njia ya maelezo yaliyojumuisha

mabango yaliyohakikiwa. Aidha, matokeo yote kutokana na hojaji wazi ambazo

zilikabidhiwa watafitiwa yamechanganuliwa, yakapangwa na kuwasilishwa kwa

kutumia majedwali. Uwasilishaji wa data ni elezi kwa kiasi kikubwa. Maelezo haya

yamejumulisha na kudhihirisha fasiri za watafitiwa wote walioshirikishwa katika

utafiti nyanjani na kujumuisha utangulizi na mahitimisho ya sura mbalimbali ili

kuonyesha ukamilifu wa maelezo kwa kuzingatia malengo ya utafiti.

Hitimisho.

Katika sura hii tumeshughulikia vipengele muhimu katika utangulizi wa utafiti

vikiwemo swala la utafiti, malengo na maswali ya utafiti, mbinu za kukusanya,

kuchanganua na uwasilishaji wa data. Misingi ya nadharia mwafaka kuongoza na

kuelekeza utafiti huu zimeelezwa. Msingi wa nadharia na mbinu za utafiti

zinasisitiza nafasi ya picha na ishara katika kuwasilisha maana na ujumbe na

namna mpokezi anavyofasiri picha na ishara zilizoshirikishwa katika mabango ya

matangazo ya UKIMWI. Katika sura inayofuata tumeshughulikia maana halisi,

(41)

SURAYAPILI

VIUNZI VYA MATANGAZO

Utangulizi

Sura hii tumeangalia jinsi mtazamo wa kisemiotiki unavyoshughulikia maana

msingi katika picha na matini. Katika kazi zinazohusisha ishara anuwai kama

vile matangazo, mtazamo wa kisemiotiki huchunguza mfumo wa maana kupitia

kwa uratibu wa viunzi tofauti katika matangazo (Barthes 1984b). Msisitizo huwa

katika msuko wa picha na ishara zinazochukuliwa kama kiini kinachofuma

maana na ujumbe katika matangazo husika. Maana msingi ni maana halisi ya

picha ambayo haihusishi hisia, tajriba na falsafa za mtu binafsi na za kijamii. Hii

ni maana ambayo yeyote ataipata kwa kuwa inapatikana waziwazi kutoka kwa

tangazo husika na ndiyo huhimili ujumbe unaoibuliwa na wapokezi mbalimbali

(Williamson, 1978).

Tumetathmini maana msingi katika matangazo ya UKIMWI kwa kujikita kwa

viunzi vyote vinavyoshirikishwa kwenye bango vikiwemo: picha na ishara kwa

kuzingatia namna zilivyosukwa pamoja na matini zilizoambatishwa. Matini

zimetengwa katika vitengo vifuatavyo:

• Vichwa vikuu.

• Wito.

(42)

Imehalisi kuchunguza ni vipi utangamano mwafaka wa viunzi hivyo vyote

vinavyohusishwa, unavyokuwa nguzo imara ya kujengea maana msingi

zinazojidhihirisha katika mabango ya matangazo mbalimbali ya UKIMWI.

2.1.0 Picha na Ishara

Picha na ishara zimechukua nafasi kubwa katika mabango ya matangazo mengi

ya UKIMWI ili kuiteka nadhari ya hadhira. Picha na ishara zinazoshirikishwa

ndizo zinazochukua sehemu kubwa ya mawazo yanayopitishwa, kwa kuwa

yanayoonwa hukumbukika na kubakia katika nadhari ya hadhira kuliko yale

yanayosomwa (Jefkins 2002).

Msanii wa picha na ishara katika matangazo huwajibika kuziwasilisha kwa njia

inayoeleweka kwa kuakisi tajriba na matarajio ya hadhira yake. Kwenye data

zetu picha na ishara zimesaniiwa kwa njia inayodhihirisha umakinifu katika

uteuzi, kwa kuhakikisha kuwa picha zinaoana na ujumbe unaotolewa. Mabango

haya yamesukwa kwa njia yenye mvuto, rangi za kupendeza na kwa uratibu

unaoitaharukisha hadhira. Mpokezi anapolitazama bango fulani, linamvutia

toka mwanzo mpaka mwisho ill apate maana yake kikamilifu. Hivi ni kusema

kuwa, kuna mwingiliano fulani, kati ya yaliyomo katika tangazo na wapokezi,

kwa mujibu wa uwezo wao wa utambuzi wa mahusiano ya ishara. Mfano mzuri

wa tangazo linaloiteka nadhari ya kila mpokezi, kutokana na muktadha

mwafaka unaoakisi matarajio ya jamii ya wakati huu, rangi zenye mvuto, lugha

(43)

Katika tangazo hili, maana msingi inajidhihirisha wazi, hata rwapo matini

zilizoambatishwa ni haba ambapo tunapata ni kauli moja fupi:

JIKINGE..AIDS isReal!

JIKINGE...UKIMWI niUhaIisi!

Picha hii imeratibiwa kwa njia ambayo mpokezi anaipata maana msingi pasi

kutegemea ufafanuzi wa matini. Sawia, picha na ishara ambazo zimeambatishwa zinaonekana kutimiza majukumu yafuatayo kulingana na

maoni ya watafitiwa:

• Kuvuta tabasuri ya wapokezi.

(44)

• Kusaidia msomaji wa tangazo kukumbuka kiini cha ujumbe hata

baadaye.

• Kutoa ufafanuzi zaidi kuhusu suala linalotangazwa.

• Kuboresha muktadha na kumtamanisha msomaji kwa yaliyomo katika

tangazo.

• Kuhimili maelezo ya matini.

• Kuimarisha vidokezi muhimu na imara ili kuvibaidi na vidokezi hafifu na

sadifu.

• Kubainisha hadhira lengwa na kuitenga kutokana na hadhira sadifu.

Kwa kuzingatia yaliyomo katika bango, kwa mbali tanapata mastakimu ya

kifahari iliyozingirwa kwa ua imara. Mazingira yametunzwa vyema, kuashiria

haiba na utukufu wa wenyeji wa makazi hayo. Hata hivyo, haya yote hayaipi

familia iliyosawiriwa naima yoyote, kwa vile sononeko na majonzi yanashamiri

nyusoni za wahusika katika bango hili. Inaonekana wazi wameondokewa na

mmoja hasa kutokana na pengo lililoko baina ya mama na mtoto wao msichana.

Mikono yao imewekwa katika namna inayodhirisha hali ya kukata tamaa. Asili

ya simanzi kuu walionao wahusika hawa inaelezewa kinaganaga na jeneza lililo

kando nyuma yao, linalodhihirisha kuwa kifo kimewapokonya mwandani wao

kutokana na janga la UKIMWI. Matini imeambatishwa kudhihirisha kuwa

UKIMWI ni uhalisi bali si ugonjwa wa kupuuzwa na kufanyiwa masihara na

(45)

Ni dhahiri kuwa picha na ishara zinazoshirikishwa katika tangazo huweza

kuwapa shauku wasomaji au pia kuwapunguzia shauku zao kulingana na jinsi

zilivyowasilishwa na kutumiwa.

2.1.1 Maana za Picha na Ishara

Katika uchanganuzi wa kisemiotiki, picha na ishara huchukullwa kama kitengo

mojawapo cha usemi, kinachotarajiwa kuwasiliana na wapokezi kwa kuchochea

au kusaili dhana fulani (Tanaka 1994). Katika hall hii, usemi sio kifaa cha

unenaji bali umbo la kijamii la kuwasilisha ujumbe na kuingiliana. Hivyo basi,

picha huwa na sura na sifa za usemi zinazojidhihirisha katika msuko au

muundo wa tangazo. Msuko wa picha huwa na mchango mkubwa katika

kuathiri mkondo wa maana na ujumbe kwa wapokezi. Matangazo husomwa

kufuata mpangilio wa juu chini unaojengea mshikamano wa mifumo ya maana

(Gombrich 1977).

Matangazo mengi yaliyoambatishwa picha yameathiriwa pakubwa na mazoea ya

usomaji wa matini hivi kwamba msuko wa picha zenyewe katika mabango

hufuata mkondo wa usomaji kutoka kushoto kuelekea kulia. Msuko huu ni

muhimu katika kuelekeza jicho la wapokezi katika kutalii na kutathmini

yaliyoshughulikiwa katika tangazo. Miundo ya matangazo yanayoshirikisha

picha hullnganishwa na miundo ya sentensi. Kwa mfano, katika sentensi

yanayofahamika hutangulia mwanzo ili kuelekeza wapokezi kwa mapya

(46)

Halima ni mhadhiri.

Halima kama mhusika anafahamika, lisilojulikana ni kuhusu kazi anayoifanya ambayo sasa inabainishwa. Mpangilio huu umetumika katika mabango mengi

ya matangazo ya UKIMWI.

Kichwa kikuu kinadokeza hususan yale yanayofikirika kufahamiwa na hadhira

lengwa na kuambatishwa picha inayochukua nafasi kubwa ya tangazo Hi

kukijadili na kukihimili. Picha hii inafafanua mambo ambayo yamedokezwa katika kichwa kwa kina, na kumwelekeza msomaji wa tangazo kulitalii na

kulielewa swala linalojadiliwa vyema.

Mushkili katika ung'amuzi wa maana unaoweza kuibuliwa na picha,

unasuluhishwa kwa matini zinazoambatishwa Hi kumwezesha mpokezi kujikita tu kwa vidokezi imara asije akayumba sana na kupotosha maana. Matini hizi

zinazoambatishwa kuihimili picha na kutoa ufafanuzi zaidi zinakuja baadaye,

aghalabu upande wa kulia au chini ya picha zenyewe. Vestergaard na Schr0eder

(1985) wanadokeza kuwa matangazo mengi yanayoambatisha picha katika

kufafanua maana na ujumbe hufuata mpangilio huu unaozingatiwa katika lugha andishi.

Wasanii wa matangazo yanayohusisha picha na ishara, hutanguliza kwa kiini

cha tangazo katika kichwa, hatimaye picha huambatishwa na kutolewa

(47)

huu wakutanguliza yanayofahamika na kukubalika katika jamii ya wakati wa

leo, na kuyafafanua zaidi kwa picha na ishara zinazofuatiliwa na matini fafanuzi

BANGONA.2

ni bango hili la Na. 2.Tangazo hili linadhihirisha mwambatano fulani wa viunzi

mbalimbali ambavyo vinashirikishwa katika tangazo vikiwemo:

• Kichwa cha tangazo.

• Picha.

(48)

• Wakala wa tangazo.

• Picha ndani ya picha.

Kichwa kinalenga moja kwa moja kwenye maana lengwa

Picha ambayo imeambatishwa inaonyesha umoja wa

wote: wanaume kwa wanawake, wazee kwa vijana, na Wakristo kwa Waislamu

katika juhudi za kupambana na janga la UKIMWI. Umoja huu wa wote

unadhihirishwa na picha ya wanaume watatu na wanawake wawili

waliounganisha viganja vya mikono ishara ya umoja ni nguvu na utengano ni

udhaifu hususan katika mapambano dhidi ya UKIMWI.

Katika kufafanuamaana kwa kina na kwa uwazi zaidi, picha hii ina wanaume

watatu. Mmoja ni Mwislamu kwa mujibu wa kofia aliyojivika kichwani. Wa pili,

ni Mkristo kutokana na tasbihi aliyoiweka shingoni inayotofautiana na tasbihi

za kiislamu. Tasbihi yenyewe imening'inia kifuani. Mwanamume wa tatu

haifahamiki yeye ni muumini wa dini gani na pia wanawake wawili waliomo

kwenye picha. Wote wameunda nusu mduara kwa kushikanisha viganja vya

mikono yao pamoja ill kusawiri haja ya ushirika. Macho yao yamekondolewa na

kuangazwa kuashiria umakinifu wa kila mmoja katika kadhia hii ya kuangamiza

UKIMWI nchini. Picha hii imeambatishwa matini:

Msisitizo unatokea kwa urejeleshi wa mada hizo tatu kusudio chini ya picha, na

(49)

1. Usifanye mapenzi kabla ya ndoa.

2. Kuwa mwaminifu kwa mpenzi mmoja daima.

3. Kama huwezi kufanya mawili hayo,jildnge nakondomu.

Kiunzi cha tangazo hili kinachofuata ni wito. Wito unaotolewa ni marudio ya

maneno yaliyotolewa katika kichwa. Hivi ni kusema kuwa, wito huu ni

msisitizo bayana wa mada kuu katika tangazo kwa vile ni marudio tu ya

maneno yale yale yaliyo kwenye kichwa kikuu, lakini wakati huu yameandikwa

kwa herufi ndogo zikilinganishwa na hati zilizotumiwa kwenye kichwa kikuu

cha tangazo hili.

Chini ya wito huu ni picha ndogo iliyo ndani ya picha kubwa, inayodhihirisha

muumano wa viganja vya mikono vinavyounda aina ya mzunguko. Duara

lililoundwa kwa kushikarnanisha viganja vya mikono linashadidia maana

iliyotangulizwa katika kichwa kuhusu juhudi za pamoja kuangamiza UKIMWI.

Katika kuhitimisha msuko wa tangazo, ni wakala wa tangazo hili unaochangia

uimarishaji na kuaminika kwa maana na ujumbe katika tangazo:

National AIDS Control Council.

Baraza La Kupambana na UKIMWI.

Kila kijisehemu kina ujumbe mdogo kinachochangia kitengo kikuu cha mfumo

kamilifu wa maana msingi katika tangazo. Hivyo, kuna utegemeano na

ujengano wa vipashio tofauti katika ujenzi wa maana msingi inayojidhihirisha

katika tangazo. Kwa mfano, wito wa tangazo unasisitiza tu, yaliyotangulizwa

katika kichwa, ilhali wakala wa tangazo unaimarisha vidokezi muhimu katika

(50)

tangazo. Tangazo lingine ambalo linadhihirisha mwambatano na ujengano wa

viunzi tofauti katika kuimarisha welewa wa wapokezi ni bango hili la Na. 3.

Tangazo hili lina viunzi vifuatavyo:

Kichwa kikuu ambacho kimeandikwa kwa muundo wa nusu duara,

MEN: CAST THE WINNING DICE AGAINST AIDS.

WANAUME: WATUPA DADO YA USHINDI DHIDI YA UGONJWA WA

UKIMWI.

Picha inayoambatishwa tangazo hili ni ya mshumaa unaowaka uliozingirwa na

(51)

ni mweusi na umezingirwa na duara dufu lililokoza rangi ya kijivu. Kuzingira

mshumaa wenyewe ni dado nyingi zilizotupwa na kurusharushwa kwenye

maeneo yote katika tangazo. Dado zenyewe zinadhihirisha sehemu za juu zenye

madoa mawili na matano na ubavuni, madoa mawili au matatu. Ishara

inayowakilisha jitihada za umoja wa wanaume katika mapambano dhidi ya

UKIMWI imeambatishwa kote katika tangazo hili. Kuhimili ishara hii ni picha

ndogo ya mchoro wa wanaume wawili walioshikana bega kwa bega na

kufuatana hatua kwa hatua kudhihirisha umoja katika juhudi za wanaume

kuushinda ugonjwa wa UKIMWI. Kuhitimisha viunzi vya tangazo hili ni wito

unaotoa arifa kwa wanaume kuhusu yanayotarajiwa:

NI JUKUMU LA WANAUME KUUSHINDA UKIMWI.

Wakala wa tangazo hili ni:

INTERNATIONAL AIDS CANDLEliGHT MEMORIAL.

SHIRIKA LA KIMATAIFA LA KUPAMBANANA UKIMWI LA MNARA WA

MISHUMAA.

Tangazo hili linadhihirisha mwambatano na uhusiano kati ya picha na wakala

wa tangazo. Picha ya mshumaa unaowaka na kuangaza kote imehimiliwa na

wakala: SHIRIKA LA KIMATAIFA LA KUPAMBANA NA UKIMWI LA MNARA

WA MISHUMAA. Wakala huu unalenga kwenye maana ya tangazo kwa

kushirikiana na ishara ya juhudi za wanaume katika mapambano dhidi ya

UKIMWI inayojengea na kuhimili maana msingi inayodhihirika katika kichwa

cha tangazo. Ishara hii ilionekana haifahamiwi na hadhira kubwa. Takribani

(52)

kuchangia maana. Hili ni dhihirisho kuwa utambuzi wa maana msmgi hutegemea uhusiano baina ya tajriba ya mpokezi na yale yaliyomo kwenye tangazo na inafaa yale yote yanayoshirlkishwa kwenye tangazo yaakisi tajriba na matarajio ya wapokezi.

Matangazo haya pia, yanadhihirisha kuwa maana msingi katika mabango ya matangazo ya UKIMWI, inaibuka kutokana na mjengeano wa viunzi tofauti katika kuibusha maana zinazoshamiri waziwazi. Yeyote ambaye angekumbana na matangazo hayo angeweza kuzitambua na kuzisoma bila shida yoyote. Maana hizi za kimsingi hazihimiliwi na utamaduni, imani au chukulizi awali mbalimbali ila hujidhihirisha wazi katika kazi za kisanaa (Barthes 1964). Sehemu inayofuata tutatathmini kila kipengele ili kuona jinsi kinavyochangia katika mshikamano wa maana msingi inayodhihirika katika tangazo.

2.2.0 Vichwa VIkuu

Ushahidi unaojitokeza katika data zetu ni kuwa kuna aina mbili ya matangazo:

• Matangazo yanayoshirikisha vichwa vikuu.

• Matangazo yasiyo na vichwa vikuu.

2.2.1 Matangazo Yanayoshirikisha Vichwa Vikuu

Vichwa vikuu vingi katika matangazo huwa ni vifupi. Huwa ni kauli za neno moja au sentensi fupi. Maneno katika vichwa hivi yamepambwa kwa fonti kubwa yakiazimia kutimiza malengo yafuatayo:

(53)

• Kufuatisha welekevu wa tangazo.

• Kuleta uangavu wa tangazo.

Aidha, vichwa hutoa ujumbe jumulifu wa yaliyomo katika tangazo kwa njia ya

iktisadi. Kichwa huweza kubainisha moja kwa moja kiini cha tangazo. Mfano

rnzuri ni tangazo hili la bango Na. 4.

(54)

Kichwa cha tangazo hili, kimeandikwa kwa hati zenye kuvuta nadhari ya

hadhira kwa mbali kutokana na jinsi kilivyokoza rangi ya majivu na kunakshiwa

vizuri huku kikizingirwa kwa rangi ya kahawia nyepesi:

CONDOM

KONDOMU

Kichwa hiki kimehimiliwa na picha iliyosawiri vibonzo vinne. Kibonzo kilicho

katikati mwa picha kimebeba na kusheni maana msingi inayoshadidiwa na

matini:

ASKARI WA WOTE: TUMIA VIZURI KILA WAKATI UKIFANYA MAPENZI.

Kibonzo hiki kimechorwa kikiwa tambo la jitu ambalo limetutumka misuli.

Hakijadhihirisha uana vizuri, hivi kwamba iliwachukua muda watafitiwa

kuamua kama kimewakilisha mwanamke ama mwanamume. Watafitiwa

asilimia 62 hawakufikia uamuzi mahsusi kama kibonzo chenyewe ni mwanamke

au ni mwanamume. Mushkili huu unajitokeza kwa vile uso unadhihirisha sura

za kiume, viatu pia ni vikubwa mno hivi kwamba vinaonekana kama vya kiume.

Machoni kimevalia miwani. Vazi kilichojivika linaonekana kama kanzu ya kike

lililopindwa kwa mkunjo unaoligeuza umbo na kulifanya kuonekana kama

kondomu. Hili ni dhihirisho wazi kuwa suala la matumizi ya kondomu linahusu

wote. Kimeshika fimbo mbili kubwa, kila mkono una fimbo. Kimetanua miguu

kama kinachopiga hatua kufikia kitu fulani. USQ una ishara ya tabasamu na

(55)

Vibonzo vingine vitatu vilivyosawiriwa vinaonekana kama vitoto

vikilinganishwa na pande la kibonzo kinachowakilisha askari. Kibonzo cha

kwanza kilichosawiriwa na tumbo kubwa kimepewa jina mahsusi la:

'Pregnancy'

Uja uzito

Mikono yote miwili inakuna kichwa, macho pima kimekondoa, na machozi

yanakitiririka. Uso unadhihirisha fadhaa na wahka mkubwa. Aidha, kimeduwaa

na hakina raha kamwe. Miguu vilevile imetanuliwa pasi kufahamu njia gani

inayofaa kufuatwa. Kimekolezwa rangi ya samawati.

Kibonzo cha pili kinachoonekana nyuma ya kibonzo cha askari kimepewa jina la

HIV- virusi vya UKIMWI. Kibonzo hiki ni kimbaumbau na hakiri zaidi

kikilinganishwa na kile cha askari. Miguu kimetagaza pia ishara ya makeke na

mbio za kasi zaidi. Kina rangi ya kahawia iliyoiva na kupakana na kijivu.

Kibonzo cha tatu, kimepewa jina la STIs - Sexually Transmitted

Infections-Magonjwa ya Zinaa. Vilevile kibonzo hOOkinakimbilia usalama na rangi yake ni

kijani hafifu. Tangazo hili limeambatishwa wito: Tumia oizuri kila wakati

unapofanya mapenzi. Wito huu unahitimisha yaliyoanzishwa na kichwa kikuu

cha tangazo hili.Wakala wa tangazo hili ni:

GOal International Humanitarian Organization.

Shirika la Mataifa la Ufadhili wa Binadamu, la al.

Ndani ya herufi 0 kuna picha ya ramani ya ulimwengu ishara wazi kuwa

(56)

uwiano kati ya viunzi mbalimbali vya tangazo hili tunapata uhusiano jenzi na

tegemezi. Aidha, wito unatilia mkazo mada kuu inayojitokeza katika kichwa cha

tangazo na kuhimiliwa vyema na picha.

Uwiano wa viunzi mbalimbali katika uimarishaji wa maana msmgi za

matangazo ya UKIMWI pia unajitokeza katika bango hili la Na. 5. Kichwa kikuu

katika tangazo hili kimeandikwa kwa hati kubwa:

TULlZA BOLI!

BANGONA.S

(57)

Kichwa chenyewe kinalenga moja kwa moja kwenye shabaha ya tangazo. Picha

iliyoambatishwa katika tangazo hili inaonyesha mchezaji nambari kumi (10)

mwenye rnzubao na wasiwasi kwa kufika kwenye ukingo wa uwanja. Inambidi

kuukanyanga mpira ghafla ili kuutuliza usitoke nje ya uwanja. Mkono mmoja

nyongani na mwingine unakuna kichwa. Anaonekana kutanzwa na kuvotana na

mawazo asijue la kufanya. Nyuma yake kuna nguzo za lango la goli. Goli lenyewe

linaonekana halina mlinzi. Katika kuimarisha maana msingi, ni matini

iliyoambatishwa:

UWANJA MDOGO: KAMDUDU KAKO, TUMIA CD.

Tell it straight! ...Sema wazi!...

Tangazo hili limekolezwa rangi ya nili inayojitokeza pia katika ramani ya Kenya

ambayo imeambatishwa kama picha ndogo ndani ya picha kubwa. Ramani hii

imezingirwa kwa duara. Katikati mwa ramani kuna duara lingine ndogo

lililoambatishwajina la wakala wa tangazo. Wakala wa tangazo ni:

Family Planning Association of Kenya

Shirika la Mpango wa Uzazi Nchini Kenya.

Viunzi tofauti vya tangazo hili vinadhihirisha uhusiano rejeleshi na sisitizi wa

maana msingi. Kichwa kikuu kinarejelea yaliyomo kwenye picha

yanayosisitizwa na kufafanuliwa na matini fupi iliyoambatishwa.

Muundo wa picha pia unajumuisha taipografia, vielelezo kama vile rangi,

ujalidi, aina ya karatasi, mfumo wa hati za maandishi na msuko wa vijisehemu

mbali mbali na jinsi vinavyofumana ili kufanikisha uwasilishaji wa maana kwa

(58)

mifumo ya kisemiotiki. Uratibu wa mifumo hii ya kisemiotiki ndiyo ambayo inaiwezesha na kuielekeza hadhira katika ufasiri wa maana na ujumbe.

Matangazo mengi katika mabango ya UKIMWI yametumia vichwa vikuu ili kutoa muhtasari wa yale yaliyomo kwenye picha hivi kwamba mpokezi asiye na muda wa kutathmini yaliyohusishwa kwenye matini fupifupi zilizoambatishwa chini au kando ya picha, ataweza kuelewa maana ya tangazo kwa kusoma kichwa tu cha tangazo. Aidha, matini fafanuzi zinazoambatishwa zinaandikwa kwa hati ndogo zisizoonekana kwa umbali. Vichwa vikuu vinawasilisha maana kwa njia yenye iktisadi lakini iliyo na uzito na uwezo wa kujumuisha hoja kuu za tangazo.

2.2.2 Matangazo Yasiyo na Vichwa Vikuu

(59)

matini fupifupi ambazo hazitoi ufafanuzi wowote kuhusu dhana

zinazowasilishwa.

Wapokezi wanaachiwa uhuru wa kuibua maana kutegemea UJUZl wao wa

mahusiano ya ishara za kisanaa. Matangazo ya aina hii katika data, ni yale

yanayohusisha maswala ya ngono na pia yale yanayohimiza matumizi ya mipira

ya kondomu katika kujikinga. Mfano mzuri ni tangazo katika bango la Na. 6a.

(60)

Tangazo hili limesawiri vijana wawili ambapo kuna mwanamume na

mwanamke wa umri wa kati. Kijana mwanamume amevalia kizibao cha rangi

nyeupe kilichopindwa kwa rangi nyeusi ambacho kimewacha sehemu ya kifua

wazi. Amevalia mkufu. Mdomo ameufumba na macho yake hayaonekani

kutokana na miwani aliyoivalia. Mikono yake imetanuliwa kama iliyoshika

sehemu za nyonga yake ishara ya kujithamini na mbwembwe za ujana. Kando

yake kuna miwani ambayo imeambatishwa picha ndogo ya pakiti ya Trust.

Msichana naye amevalia fulana ambayo nyororo yake imefunguliwa kiasi. Uso

wake hauna raha na midomo imekolezwa rangi ya kahawia iliyoiva na

ameufumbua kiasi. Kichwa chake kimeinamishwa. Mavazi yao na marembo

yanadhihirisha kuwa wao ni vijana wa kisasa, waliolelewa mjini. Nyuma yao

wawili kuna wavu usioonekana vizuri. Picha hii imeambatishwa matini:

Maisha iko sawa

na Trust.

Matini hii imeambatishwa matangazo mengi yanayohimiza matumizi ya mipira

ya kondomu kuzuia maenezi ya UKIMWI. Kile ambacho kinabadilishwa ni

picha pekee. Mfano mzuri wa mabadiliko tu ya picha unadhihirika katika bango

(61)

Tangazo hili limesawiri wanaume wawili na wanawake wawili wa umri wa

makamo. Mwanamume mmoja ameketi huku yuamvuta mwenzake kama

kwamba yuarnzuia asiurushe mpira. Mkono mmoja ameutumia kujihimili.

Amevalia shati jeusi na bushuti la rangi ya manjano. Raha inadhihiri usoni

References

Related documents

Our results show that, although tetrasomic inheritance creates additional con fi gurations of lineages that have unique probabilities of coalescence compared to those for

The full load performance with VGT was compared with the case of mechanically controlled waste-gated turbocharger, so that the potential for a higher Brake Mean

In our examination, we have tried different inside and outside releases like void, surface and crown utilizing factual parameters, for example, skewness and

ABSTRACT : In this paper, Model based approach is implemented to control a heat exchanger prototype using optimization technique for parameter tuning of PID

Further work will involve the modification of the sliding mode controller using a time-varying switching gain and improvement in modeling of the actuator over a broader

We therefore screened for gain-of-function enhancers of jing gain of function in the eye and identified the Drosophila homolog of the disease gene of human a

The usage of used water for irrigation purposes has become one of the sustainable ways of reuse. It reduces the water scarcity for farmers and also it helps in

In the present work jatropha and pongamia biodiesel blend B20 is used in a single cylinder with cooled EGR and the performance and emission characteristics of blend are