• No results found

Fani na maudhui katika mashairi ya magazeti ya taifa leo

N/A
N/A
Protected

Academic year: 2020

Share "Fani na maudhui katika mashairi ya magazeti ya taifa leo"

Copied!
146
0
0

Loading.... (view fulltext now)

Full text

(1)

FANI NA MAUDHUI KATIKA MASHAIRI YA MAGAZETI YA TAIFA LEO

NA

MOGENI MAGOMA ERICK C50/CE/22694/2010

TASNIFU ILIYOWASILISHWA KATIKA IDARA YA KISWAHILI NA LUGHA ZA KIAFRIKA KATIKA CHUO KIKUU CHA KENYATTA KWA MINAJILI YA

KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJI YA SHAHADA YA UZAMILI

(2)

ii UNGAMO

Kazi hii ni yangu mwenyewe na haijawahi kutolewa katika Chuo Kikuu kingine kile.

Sahihi:________________________ Tarehe:________________________

Mogeni Magoma Erick

C50/CE/22694/2010

Tasnifu hii imewasilishwa kwa idhini yetu kama wasimamizi wa kazi hii wa Chuo Kikuu cha Kenyatta.

Sahihi:____________________________ Tarehe:_________________________

Profesa Kitula King‟ei

(Idara ya Kiswahili na lugha za Kiafrika)

Sahihi:__________________________ Tarehe:_________________________

Daktari Edwin Masinde

(3)

iii TABARUKU

Kazi hii naitabarukia marehemu mamangu Bi. Paskalia Kerubo ambaye ndiye nguzo

(4)

iv SHUKURANI

Shukrani zangu za dhati kwanza nazitoa kwa Maulana kwa kunijalia afya wakati wote

nilipokuwa nikishughulikia kazi hii. Pili ningependa kutoa shukurani zangu za dhati kwa

waelekezi na wahadhiri wangu, Profesa Kitula Kinge‟i na Daktari Edwin Masinde kwa

uelekezi wao ambao ndio nguzo kuu katika matokeo ya kazi hii.

Mbali na wasimamizi, shukrani ziwaendee wahadhiri wote katika idara ya Kiswahili kwa

kunifundisha, kuielekeza na kunipa dira kamili katika safari hii ndefu na yenye

misukosuko. Nyote Mungu awabariki.

Pia nawashukuru ndugu zangu Risper, Dennis, Lilian, Videlis na Charles kwa kunipa

moyo na kwa maombi yenu. Shukrani zingine zimwendee Bi. Mildred kwa kuipiga chapa

kazi hii.

Vilevile namshukuru mke wangu Bi Everline Kemunto kwa kusimama nami kwa hali na

mali hasa kwa kuzidi kuniombea kwa kipindi chote nilipokuwa naishughulikia kazi hii.

Shukurani zangu pia ziwaendee watoto wangu Brian na Kerubo.

Aidha ningependa kuwashukuru wanafunzi wenzangu kama Kiange, Gladys, Joy,

Nyandoro, Onsarigo, Karani na wengine wote waliochangia kwa njia moja au nyingine

(5)

v IKISIRI

(6)

vi ABSTRACT

(7)

vii YALIYOMO

UNGAMO... ii

TABARUKU ... iii

SHUKURANI ... iv

IKISIRI ...v

ABSTRACT ... vi

YALIYOMO ... vii

SURA YA KWANZA: UTANGULIZI ...1

1. 0 Usuli ...1

1. 1 Suala la utafiti ...2

1.2 Malengo ya utafiti ...3

1.3 Maswali ya utafiti ...3

1.4 Sababu za kuchagua mada ...4

1.5 Upeo na mipaka ya utafiti ...4

1.6 Yaliyoandikwa kuhusu mada ...5

1.8.0 Mbinu za utafiti ...13

1.8.1 Muundo wa utafiti ...13

1.8.2 Mahala pa utafiti ...14

1.8.3 Sampuli lengwa ...14

1.9.0 Ukusanyaji wa data ...14

1.9.1 Upangaji wa Data ...14

1.9.2 Uchanganuzi wa Data ...15

1.9.3 Uwasilishaji wa data ...15

1.9.4 Hitimisho...15

SURA YA PILI: FANI NA MAUDHUI KATIKA USHAIRI WA KISWAHILI ...16

2.0 Utangulizi ...16

2.1.0 Fani Katika Utunzi Na Uwasilishaji Wa Ushairi ...16

2.1.1 Taswira. ...22

2.1.2 Jazanda ...24

2.1.3 Chuku ...24

(8)

viii

2.1.5 Takriri ...26

2.1.6 Tashhisi ...27

2.1.7 Kuchanganya ndimi ...29

2.1.8 Inkisari ...29

2.1.9 Mazida...30

2.1.10 Tabdila ...31

2.1.11 Kuboronga Sarufi ...31

2.1.12 Methali ...34

2.1.13 Utohozi. ...34

2.1.14 Tashbihi...36

2.1.15 Tanakali za sauti /onomatopoeia ...36

2.1.16 Misimu ...37

2.1.17 Nidaa/Siyahi ...37

2.1.18 Nahau ...38

2.1.19 Isitiari. ...38

2.2.0 Maudhui Katika Ushairi Wa Kiswahili...39

2.2.1 Dhana ya Maudhui ...39

SURA YA TATU: UCHAMBUZI WA FANI NA MAUDHUI YA MASHAIRI YA MAGAZETI YA TAIFA LEO ...45

3.0 Utangulizi ...45

3.1 Uwasilishi wa fani na maudhui ya kijamii ...49

3.1.1 Shairi la Tupate Fahamu ...49

3.1.2 Shairi la Napinga utoaji mimba ...51

3.1.3 Shairi la Jongoo na Jogoo ...53

3.1.4 Shairi la Ni Nani Changudoa ...56

3.1.5 Shairi la Tafakari ewe msichana ...58

3.2. Uwasilishi wa Maudhui ya Kiuchumi...61

3.2.1 Shairi la Ukosefu wa Ajira ...61

3.2.2 Shairi la Nikawalisha ...63

3.2.3 Shairi la Nchi Iko Kilindini...66

(9)

ix

3.2.5 Shairi la Maskini Wateseka ...74

3.3 Uwasilishi wa Fani na Maudhui ya Kisiasa ...77

3.3.1 Shairi la Majimbo Yatufaa ...77

3.3.2 Shairi la Katiba Gani Itazaliwa. ...81

3.3.3 Shairi la Haki iko Hegi ...85

3.3.4 Shairi la Niwanauliza, Siasa ni Vita ...88

3.3.5 Shairi la Kura Tusiuze. ...94

SURA YA NNE: DHIMA YA GAZETI LA TAIFA LEO KATIKA KUENDELEZA UTANZU WA USHAIRI NCHINI KENYA ...101

4.0 Utangulizi ...101

4.1 Dhima ya gazeti la taifa leo katika maendeleo ya ushairi nchini Kenya ...103

4.2 Mchango katika fani ...103

4.2.1 Taswira ...103

4.2.2 Balagha / Mbalagha ...105

4.2.3 Tashbihi...105

4.2.4 Tashhisi / uhaishaji ...106

4.2.5 Takriri ...106

4.2.6 Inkisari na mazida ...107

4.3.0 Mchango kimaumbo ...108

4.4.0 Mchango kimaudhui ...108

4.4.1 Maudhui ya kijamii ...108

4.4.2 Maudhui ya kisiasa ...109

4.4.3 Maudhui ya kiuychumi ...109

4.4.4 Mchango wa umbuji wa wahusika ...110

4.5.0 Hitimisho...110

SURA YA TANO: HITIMISHO NA MAPENDEKEZO ...111

5.0 Utangulizi ...111

5.1 Hitimisho...113

5.2 Mapendekezo kwa utafiti zaidi ...116

MAREJELEO ...118

(10)

x

KIAMBATISHO B: NAPINGA UTOAJI MIMBA ...123

KIAMBATISHO C: JONGOO NA JOGOO ...124

KIAMBATISHO D: NI NANI CHANGUDOA? ...125

KIAMBATISHO E: TAFAKARI EWE MSICHANA ...126

KIAMBATISHO F: UKOSEFU WA AJIRA ...127

KIAMBATISHO G: NIKAWALISHA ...128

KIAMBATISHO H: NCHI IKO KILINDINI ...129

KIAMBATISHO I: SHEREHE AU TWAPORA...130

KIAMBATISHO J: MASIKINI WATESEKA ...131

KIAMBATISHO K: MAJIMBO YATUFAA ...132

KIAMBATISHO L: KATIBA GANI ITAZALIWA? ...133

KIAMBATISHO M: HAKI IKO HEGI ...134

KIAMBATISHO N: NIWANAULIZA, SIASA NI VITA? ...135

(11)

1

SURA YA KWANZA UTANGULIZI

1. 0 Usuli

Magazeti ya Taifa Leo Jumamosi na Taifa Jumapili yamekuwa yakiendeleza mashairi ya

Kiswahili kwa muda mrefu sasa. Waandishi, wachapishaji pamoja na wahariri huwa na

malengo maalum ambayo wanatarajia kuyatimiza.

Mashairi haya yanatarajiwa kuwa na hadhira pana katika jamii nchini Kenya hasa

ikizingatiwa kwamba gazeti la Taifa Leo ndilo tu ambalo huchapishwa kila siku katika

lugha ya Kiswahili. Pia, kutokana na ukweli kuwa somo la Kiswahili ni la lazima katika

shule za msingi na upili nchini Kenya bila shaka wengi wa wanafunzi na wakufunzi

hutarajiwa kulisoma gazeti hili.

Pia vyuo vyote vya ualimu hasa wa shule za kimsingi hufunza somo hili kama la lazima.

Aidha vyuo vikuu nchini Kenya hufunza somo la Kiswahili. Hivi leo nchini Kenya

kikatiba Kiswahili kimepewa hadhi ya lugha ya taifa na rasmi (Katiba ya Kenya, 2010).

Ulimwenguni Kiswahili kimekuwa lugha ya kimataifa. Hii ina maana kuwa vipengele

vyote vya lugha hii vinafaa kuendelezwa ili kukidhi mahitaji ya jamii nchini Kenya.

Katika mashairi haya maudhui mbalimbali hudhihirika. Ni dhahiri kuwa hamna fasihi

ambayo inaibuka katika ombwe tupu. Mashairi yana uhusiano na maisha katika jamii.

King‟ei, K. Na Kisovi, C. (2005) fasihi hutumia fani au ufundi fulani wa kimasimulizi ili

kuwasilisha maudhui fulani kuambatana na matakwa ya mwanafasihi. Maudhui ya fasihi

huchochewa na hali halisi katika jamii ya mwanafasihi na mazingira yake. Isisahaulike

(12)

2

kuelimishwa katika jamii yake na bila shaka, ameathiriwa sana kimawazo na maisha ya

jamii yake. Pale anapotunga kazi ya fasihi, mwanafasihi huweza kushughulikia maudhui

ambayo ni muhimu kutokana na hali halisi katika jamii anamoishi na anamojifunza.

Ingawa hivyo kuna haja ya kufanya utafiti wa kina ili kuonyesha ni maudhui yapi

yanaendelezwa katika mashairi ya Magazeti ya Taifa Leo Jumamosi na Taifa Jumapili,

maudhui hayo huendelezwa vipi na ni ipi nafasi ya gazeti hilo katika maendeleo ya jamii

nchini Kenya. Miongoni mwa masuala ambayo hushughulikiwa na mashairi haya ni yale

ibuka kwa hivyo utafiti huu utayashughulikia yanayohusu siasa, jamii na uchumi.

1. 1 Suala la utafiti

Kuna tafiti nyingi ambazo zimetangulia utafiti huu na kugusia swala la fasihi na vyombo

vya habari. Kirichia (2012) amegusia usawiri wa wanasiasa kama wahusika katika

makala za habari kwenye gazeti la Taifa Leo Nchini Kenya yeye katika utafiti wake

alilenga kudhihirisha taswira mbalimbali za wanasiasa namna zinavyochorwa katika

gazeti la Taifa Leo. Ingawa utafiti huo unatumia gazeti la Taifa Leo kama wetu, wetu ni

tofauti kwa vile unaangazia fani na maudhui katika mashairi yanayowasilishwa katika

gazeti la Taifa Leo. Ushairi magazetini unadhihiri mabadiliko makubwa katika fani na

maudhui.Ingawa hivyo kuna haja ya kufanya utafiti ili kuonyesha maendeleo hayo.Kwa

hivyo utafiti huu utapata fursa ya kuonyesha fani na maudhui katika mashairi ya magazeti

ya Taifa Leo Jumamosi na Taifa Jumapili mwaka wa 2010-2012.

Utafiti huu ulidhamiria kuonyesha ni maudhui yapi yanavyoendelezwa katika ushairi

(13)

3

yanaendelezwa vipi na ni ipi dhima ya gazeti hili katika usawiri wa masuala nchini

Kenya.

Vilevile utafiti huu uliangazia ushairi magazetini kwa vile kuna baadhi ya mashairi

ambayo huchapishwa katika magazeti na hayapati fursa ya kuchapishwa vitabuni. Kupitia

utafiti huu jamii ilipata fursa ya kufahamu maswala nyeti ambayo hawangeyafahamu kwa

kutegemea vitabu vya ushairi pekee

magazeti ni njia muhimu ya kuwafahamisha wanajamii.Wale ambao hawawezi kupata

fursa ya kusoma mashairi vitabuni wanaweza kupata fursa kupitia kwa usomaji wa

magazeti. Hivyo, utafiti huu ulipata fursa ya kuonyesha ni maudhui yapi yanaendelezwa

katika ushairi unaochapishwa katika Magazeti ya Taifa Leo Jumamosi na Taifa Jumapili,

yanaendelezwa vipi na hatimaye kuonyesha dhima ya gazeti la Taifa Leo katika kusawiri

masualaibuka nchini Kenya.

1.2 Malengo ya utafiti

1. Kuchunguza fani na maudhui katika mashairi ya gazeti la Taifa Leo.

2. Kubainisha namna gazeti la Taifa Leo linavyosawiri maudhui hayo.

3. Kuonyesha dhima ya gazeti la Taifa Leo katika kusawiri masuala-ibuka nchini

Kenya.

1.3 Maswali ya utafiti

1. Je, ni maudhi gani yanashughulikiwa katika mashairi ya gazeti la Taifa Leo?

2. Maudhui hayo hushughulikiwa vipi?

(14)

4 1.4 Sababu za kuchagua mada

Sababu za kuchagua mada hii ni pamoja na ukweli kwamba gazeti la Taifa Leo ni la

kipekee la Kiswahili na kwa hivyo inatarajiwa kuwa inafikia hadhira pana na hivyo

hushughulikia maswala mbalimbali yanayoathiri jamii.Pia ushairi magazetini unadhihiri

mabadiliko katika fani na maudhui hasa ikizingatiwa kuwa jamii ya kisasa inakumbwa na

changamoto zinazotokana na matokeo ya mabadiliko katika sekta ya sayansi na

teknolojia.Kwa hivyo kuna haja ya kufanya utafiti ili kuonyesha mabadiliko katika fani

na maudhui yanayodhihirika katika utanzu huu wa ushairi magazetini na hatimaye

kuonyesha nafasi ya gazeti la Taifa Leo katika kuakisi mabadiliko hayo.

Dhima ya fasihi ni pamoja na kuonya, kuelimisha, kuhifadhi utamaduni, kuburudisha,

kuadilisha na kadhalika. Kwa hivyo kupitia kuonyesha masuala-ibuka haya dhima ya

fasihi itadhihirika. Utanzu huu wa ushairi umetengewa nafasi maalum katika gazeti hili

hivi kwamba huwa na ukurasa wake kila siku ya Jumamosi na Jumapili.

Ulimwengu wa sasa umekumbwa na mabadiliko mengi kwa sababu ya maendeleo

kiwakati, na hayo mabadiliko yamezua masuala mengi yakiwemo yale ibuka. Kwa

misingi hiyo tunataka kufanya utafiti ili kubainisha maswala ibuka hayo na kuonyesha

changamoto zake katika maendeleo ya jamii; na hivyo kuwawezesha watu kujua namna

ya kukabiliana na changamoto hizo. Kwa kufanya hivi tutakuwa tunaonyesha umuhimu

wa mashairi haya. Utafiti huu utawanufaisha wanafunzi wote wa Kiswahili, walimu,

washirikadau katika vyombo vya habari na jamii kwa ujumla.

1.5 Upeo na mipaka ya utafiti

Magazeti ni mengi nchini Kenya kama vile „The Standard‟, „The Daily Nation‟, „The

(15)

5

Utafiti huu utashughulikia masualaibuka katika mashairi ya Magazeti ya Taifa Leo

Jumamosi na Taifa Jumapili nchini Kenya mwaka 2010-2012. Sababu za kuyachagua

magazeti haya ni pamoja na kuwa yanaandikwa kwa Kiswahili na pia ni katika siku hizo

mbili katika juma ambapo mashairi huchapishwa. Sababu kuu ya kuchagua kipindi cha

mwaka wa 2010-2012 ni kuwa ni kipindi cha kisasa ambapo masuala mengi yakiwemo

yale ibuka hudhihirika

Utafiti huu umezingatia mashairi yaliyochapishwa katika Magazeti ya Taifa Leo

Jumamosi na Taifa Jumapili za mwaka 2010-2012.

Mtafiti atachagua magazeti ambayo yana maudhui ya kijamii, kisiasa na kiuchumi.

Mtafiti angependa kushughulikia masualaibuka mengi kama vile yanayohusu sayansi na

teknolojia, mazingira, utandaridhi na kadhalika lakini kutokana na ukosefu wa muda hili

halitafanyika.

Mathalan ni dhahiri kuwa mashairi yanayochapishwa katika Magazeti ya Taifa Leo

Jumamosi na Taifa Jumapili hudhihiri mgogoro uliopo baina ya mashairi huru na yale

yanayozingatia arudhi. Lakini utafiti huu hautajishughulisha na mgogoro huu kwa vile

malengo yake ni tofauti.

1.6 Yaliyoandikwa kuhusu mada

Suala la fani na maudhui katika fasihi limeshughulikiwa na waandishi, wahakiki na pia

watafiti mbalimbali. Senkoro (1988) alitafitia maudhui na mtindo katika mashairi ya

watunzi mbalimbali huku akitumia nadharia ya umaksi kama dira yake. Yeye katika

utafiti wake alipata kuanganzia vipengele mbalimbali vya mtindo huku akionyesha jinsi

(16)

6

mtindo ni namna ambavyo msanii huipa kazi ya fasihi sura ya kifani na kimaudhui kwa

njia ambayo msanii asingeweza kuipa hata kama jambo linalozungumziwa na wasanii

hawa ni lile moja. Katika kiwango hiki utafiti huu una mshabaha mkubwa na wetu lakini

tofauti ni kuwa utafiti wetu ulijikita katika mashairi yaliyochapishwa katika gazeti la

Taifa Leo katika kipindi cha 2010-2015. Tofauti nyingine pia inajitokeza kupitia kwa

matumizi ya nadharia iliyotumiwa. Wakati utafiti wa Senkoro ulitumia nadharia ya

umaksi utafiti wetu ulitumia mihimili ya nadharia ya kimtindo ya kirasimi iliyoasisiwa

na Leech na Short (1981).

Vilevile Nyongesa (2015) naye alifanya utafiti kuhusu mtindo na dhamira katika mashairi

ya washairi chipukizi kutoka Bungoma. Kwa ambavyo utafiti huu ulizingatia mtindo

pamoja na dhamira kuna mshabaha unaodhihirika baina ya matokeo yake na yale ya

utafiti wetu. Ingawa hivyo utafiti huu wa Nyongesa ulipungukiwa katika upande wa

kudhihirisha vipawa vya chipukizi ambao hawapati fursa ya kuchapisha mashairi yao

katika diwani. Kuna chipukizi wengi ambao hupata kuchangia maendeleo ya ushairi

nchini kupitia utunzi wao wa mashairi ambayo yanapata fursa ya kuchapishwa katika

gaziti la Taifa Leo kwa hivyo utafiti huu ulipata fursa ya kujaza pengo hilo.

King‟ei, K. na Kisovi, C. (2010) wanaeleza kuwa sanaa ya kifasihi inatokana na usanifu,

ufasaha au ufundi wa kuwasilisha mawazo au fikra za mwanadamu. Nia hasa ya

kuwasilisha mawazo kama hayo ni kudhihirisha hali fulani za maisha yake kama vile

furaha, huzuni, matatizo, fanaka, utetesi, kashfa, sifa, maelekezo au uchambuzi.

Wanazidi kuelezea kuwa ufundi huu wa kisanaa huwasilishwa kwa maneno yaliyoteuliwa

(17)

7

kwa hivyo fasihi hutumia fani au ufundi fulani wa kimasimulizi ili kuwasilisha maudhui

fulani kuambatana na matakwa ya mwanafasihi.

Kulingana nao fasihi ni zao la jamii kwa kipindi fulani katika historia. Hii ina maana

kuwa maudhui ya fasihi huchochewa na hali halisi katika jamii ya mwanafasihi na

mazingara yake. Pia ikumbukwe kuwa msanii ni zao la jamii yake kwani yeye

amezaliwa, kukuzwa na kuelimishwa katika jamii yake. Bila shaka atakuwa ameathiriwa

sana kimawazo na maisha ya jamii yake. Pale anapotunga kazi ya fasihi mwanafasihi

huweza kushughulikia maudhui ambayo ni muhimu kutokana hali halisi katika jamii

anamoishi na anamojifunza.

Maudhui ya jamii hukuwa na kubadilika kulingana na hali ya maisha ya jamii

inayohusika. Mwisho tunakubaliana kwa dhati na waandishi hawa kuhusu majukumu

yanayotekelezwa na fasihi kama vile:

i. Kukuza, kueneza, kuboresha na kuhifadhi utamaduni.

ii. Kukuza, kueneza, kupanua na kuhifadhi lugha.

iii. Kuitumbuiza jamii

iv. Kuhifadhi historia ya jamii.

v. Kuwahamasisha wanajamii kujikomboa kisiasa na kitamaduni.

vi. Kusifia viongozi au asasi za kijamii zilizo bora.

(18)

8

Waandishi hawa wanadai kuwa fasihi inafungamana sana na mitindo ya maisha ya kila

siku na ni dhahiri kwamba maudhui yake yanagubika kila kipengele cha maisha ya

mwanadamu.

Mlacha (1995) akiandika kuhusu vyombo vya habari na usambazaji wa fasihi alieleza

kuwa vyombo vya habari vina uhusiano mkubwa sana na fasihi hasa kwa vile vyote hivi

vimetawaliwa na lugha ambayo hasa ndio njia muhimu ya mawasiliano baina ya

binadamu.

Kwa maneno mengine mtu anaweza kusema kuwa vyombo vya habari na fasihi ni

vyombo vinavyotumiwa na binadamu kwa mawasiliano ingawa kimoja (ambacho ni

vyombo vya habari) kinatumiwa pia kama chombo cha kuiwasilisha fasihi kwa

binadamu.

Kwa njia hiyo pia gazeti la Taifa Leo likiwa chombo mojawapo la vyombo vya habari

huchapisha mashairi ambamo lugha hutumika kwa njia ya kipekee ili kuwasiliana na

binadamu.

Mathalan mwandishi huyo anaeleza kuwa vyombo vya habari na fasihi kimuktadha na

kiutekelezaji vina dhima sawa ingawa vinatofautiana. Mantiki inayoweza kuvifanya

vyombo hivi viwili vifanane zaidi na au hata vilingane ni ile ya kuelimisha.

Kuhusu vyombo vya habari Mlacha anaeleza kuwa vina nafasi kubwa sana katika kukidhi

lengo la mawasiliano katika jamii. Aidha, hii ndio njia mojawapo ya kuwafanya

wanajamii waweze kuyafahamu matukio tofauti ya kila siku katika jamii yao, waifahamu

(19)

9

Kuhusu mawasiliano Mlacha (1995) anaeleza kuwa vyombo vya habari, vikiangaliwa

katika ujumla wake, vina majukumu mawili muhimu sana. La kwanza ni lile la

kuielimisha jamii kunakotokana na hayo mafanikio ya kuwasiliana ambayo nayo

yanatokana na binadamu kuelewana katika ishara zao. Hii ndiyo maana wataalamu kama

akina Parry J. (1967:29) wanasisitiza kuwa ni katika ndani ya mfumo mzima wa

mawasiliano ambamo kuelimisha kunajitokeza kuwa jambo linalotawala. Hii inatokana

na hali ya kuwa mfumo wa kuwasiliana umekitwa zaidi katika kueleweshana na

kuhakikisha kuwa kile ambacho hakifahamiki au hakijaeleweka vizuri kinafafanuliwa na

kufikishwa kwa watu wote wanaohusika na wanaostahili kukifahamu. Lengo kuu sio

katika kubadili tabia au maisha ya yule anayepokea ujumbe moja kwa moja, bali kumpa

taarifa aweze kutafakari ishara zake na kuelewa kutokana na tafsiri yake ya ishara hizo.

Wapo wataalamu ambao wameonyesha kuwa upo uhusiano baina ya fasihi na vyombo

vya habari. Upubor (1985:159) ameviona vyombo vya habari kama namna ya kuchangia

ujuzi na uzoefu ambapo idadi kubwa ya watu wanaweza kuhusishwa kwa wakati mmoja.

Fasili hii ya Upubor anadhihirisha kuwa upo uhusiano unaoweza kubainika baina ya

vyombo vya habari na fasihi.

Kwa upande mwingine wataalamu wengine kama vile Igbenedion (1985:115) wanadhani

kuwa vyombo vya habari vinaweza pia kuwa na athari mbaya kwa hadhira, bado ni

vyombo ambavyo, kama asemavyo konde (1984:239), vinaweza kuwa silaha ya kulinda

hadhi ya binadamu, hasa tunapozingatia kipengele cha kuelimisha jamii.

Kuhusu fasihi Mlacha (1995) anaeleza kuwa inaweza kuangaliwa pia kama chombo cha

(20)

10

kwa hakika fasihi hukusanya habari na matukio ya muda mrefu katika jamii ambayo

yamechukuliwa kama sehemu ya utamaduni wa jamii hiyo. Lengo kuu la fasihi ni lile la

kuielimisha na hata kuiburudisha jamii, kama vile lilivyo lengo kuu la vyombo vya habari

gazeti la Taifa Leo likiwa miongoni mwao.

Fasihi huelezwa kwa kutumia lugha na ishara kama vile ujumbe wowote ule

unaopitishwa kwenye vyombo vingine vya habari. Lakini zaidi ya hayo, ndicho chombo

kinachouwakilisha utamaduni wa jamii na hapo ndipo ulipo umuhimu wa kuisambaza

fasihi ili iwafikie na kueleweka kwa wanajamii wote. Yenyewe haiwezi kujisambaza bila

msaada wa vyombo vya habari vinavyojitokeza kama vyombo muhimu sana katika

usambazaji na ukuzaji wa fasihi.

Hapa nchini vyombo vya habari vimeipa fasihi nafasi kubwa sana na hivyo kuipanua

hadhira yake. Kwa mfano katika uchapishaji wa gazeti la Taifa Leo ambamo kurasa

maalum zimetengwa ili kuendeleza vipengele vya fasihi siku ya Jumamosi na Jumapili

kila juma. Hii inaonyesha kuwa, jamii ambayo ndiyo yenye vyombo hivyo vya habari,

imeona umuhimu wa kuisambaza fasihi na njia bora ilivyojitokeza ni kutumia vyombo

kama vile redio, magazeti, televisheni na hata video.

Ni muhimu kuzingatia aliyoyaelezea Wasberg (1988:21) alipotaka kuonyesha nafasi ya

vyombo vya habari katika kuikuza fasihi. Yeye ameeleza wazi kuwa waandishi wengine

wamelazimika kutumia vyombo vya habari kusambaza kazi zao hasa kwa vile

(21)

11 1.7 Misingi ya kinadharia

Utafiti huu umeongozwa na nadharia ya kimtindo ya kirasimi iliyoasisiwa na

Leech na Short mwaka wa (1981). Kulingana na nadharia hii mawazo ya mtunzi

huwa yameumbwa kitambo. Huwa yapo na ni juu ya mtunzi huyo kuyanasa kwa

njia bora itakayomwezesha katika kueleza matukio hayo kwa njia mwafaka. Kila

mtunzi hujitokeza na kunasa ujumbe kwa njia yake ya kipekee. Hii ina maana

kuwa iwapo mtunzi atanasa ujumbe kwa njia isiyofaa basi hivyo ndivyo

atakavyouwasilisha. Vilevile iwapo ataunasa kwa njia bora ndivyo

atakavyouwasilisha.

Nadharia hii inaeleza kwamba kazi ya fasihi haiwezi kueleweka bila lugha. Kwa

hivyo, jinsi mtu atumiavyo lugha husaidia kutoa ujumbe wake kwa wasomaji au

wasikilizaji. Hivyo, lugha huwa ndiyo chombo muhimu cha mawasiliano katika

jamii zote za wanadamu.

Chambilecho Leech: (1969:4).

Kazi ya fasihi haiwezi kueleweka vizuri bila ya

lugha ambayo hutumiwa kuieleza. Ni vyema

kuelewa uhusiano ulioko kati ya lugha ya ushairi

na ujumbe wa mwandishi. (Tafsiri yetu)

Nadharia hii inasisitiza uhusiano kati ya ujumbe na lugha. Kulingana na Leech

(ibid) kazi ya fasihi hukusudia kuwasilisha hisi au tajriba fulani kwa wasomaji

au wasikilizaji. Aeleza kuwa nadharia hii ina vigezo vinavyotumiwa kuchambua

(22)

12

Leech aeleza kuwa mshairi hutumia lugha "kiajabu" na a thari za uchumi

haziwezi kutenganishwa na matumizi ya lugha kisanaa.

Kuyatilia uzito maelezo haya Senkoro (1982) aeleza kwamba ushairi ni utanzu

wa fasihi unaotumia mpangilio wa lugha ya mkato, ya picha, na yenye mapigo

mahususi katika kutoa maudhui. Anarudi kueleza kuwa ushairi hutumia lugha ya

mkato yenye kueleza maudhui yake kimuhtasari, na mara nyingi huya ficha

maudhui hayo ndani ya taswira na ishara.

Ngara (1982) aeleza kwamba matumizi ya lugha katika kazi ya sanaa ni njia moja

ya kuvuta hisi na hadhira. Kwa hivyo tutachambua muundo wa lugha katika

kujenga na kutoa ujumbe wa mwandishi.

Leech, N. (1981:15) akimrejelea Aristotle na Plato anaeleza kuwa yaliyomo na

jinsi yaliyomo yanavyowasilishwa ni kama mwili na roho. Hii ina maana ya

kuwa maudhui na namna yanavyowasilishwa ni mambo mawili yanayotegemeana

na kuathiriana.

Aidha Leech (ibid) anaeleza kuwa katika matini tunaweza kuchunguza muundo

kwa kina ili kuona ni maneno/sauti zipi zinazopendelewa zikilinganishwa na

zingine. Hili limetuwezesha kupata maan a aliyokusudia mtunzi wa kazi ya sanaa.

Mhimili huu umetufaa katika utafiti wetu kwa vile tumeutumia katika kuchambua

na kuhoji sababu za baadhi ya watunzi wa mashairi kutumia takriri ya sauti au

maneno katika kazi zao.

Mhimili mwingine ni kuwa maudhui na mtindo katika kazi ya kirasimi ni mambo

(23)

13

uliokamilika kati ya kinachoelezwa na jinsi kinavyoelezwa (Wafula R. na Njogu

K. 2007). Mhimili huu umetufaa katika utafiti wetu kwa vile tum eutumia katika

kutathmini yaliyomo na jinsi yaliyomo yanavyowasilishwa. Kwa mfano katika

kuchambua yaliyomo tumeongozwa na mambo matatu ambayo n i mada, maudhui

na mielekeo. Pia katika kuchambua jinsi yaliyomo yanavyowasilishwa

tumeongozwa na mambo kama vile vipengele vya lugha ambavyo vimejumuisha

maelezo ya moja kwa moja, kejeli, na sadfa miongoni mwa vingine.

Pia tumezingatia mbinu za kisarufi kama vile, matumizi ya vina, mizani, takriri,

inkisari, mazida n.k. Aidha tumezingatia namna kila mtunzi anavyotu mia

tamathali za usemi kama vile: stiari, tashbihi, tashhisi, balagha na kisengere

nyuma miongoni mwa zingine. Mhimili mwingine katika nadharia hii ambao

umekuwa wa manufaa katika utafiti wetu ni ule ambapo mwanasanaa anayetunga

kazi ya kirasimi humezwa na mkondo wa fikra uliomzunguka. Mhimili huu

umetuwezesha katika kutambua maudhui ya kisiasa, kiuchumi na kijamii ambayo

ndiyo humwathiri kila mtunzi katika maisha yake ya kila siku.

1.8.0 Mbinu za utafiti 1.8.1 Muundo wa utafiti

Utafiti huu ni wa kimaelezo. Utafiti wa kimaelezo ni ule ambao hutegemea maelezo

katika uwasilishi na uchanganuzi wake. Utafiti huu utajikita katika maktaba. Mtafiti

amesoma magazeti ya Taifa Leo, makala, majarida, vitabu na tasnifu mbalimbali

(24)

14 1.8.2 Mahala pa utafiti

Utafiti huu umejikita maktabani na nyanjani sababu kazi hizi zinapatikana huko. Pili,

katika maktaba tumepata makala ya kusoma yanayoeleza misingi ya nadharia ya uhalisia

kwa uwazi na pia yaliyoandikwa kuhusu mada.

1.8.3 Sampuli lengwa

Sampuli lengwa katika utafiti huu, ni magazeti ya Taifa Leo Jumamosi na Taifa Jumapili

na kinacholengwa ni fani na maudhui. Kwa hivyo magazeti na masuala hayo

yameteuliwa kimakusudi. Uteuzi wa kimakusudi ni mbinu ya kutoa sampuli wakilishi

kutokana na idadi kubwa ya watu, au vitu ambavyo haviwezi kuchunguzika vyote kwa

pamoja. Mbinu hii humwezesha mtafiti kuchagua sampuli inayowakilisha kila aina ya

tabia inayopatikana kundini. Utafiti wetu umeazimia kuzingatia magazeti ya Taifa Leo

Jumamosi na Taifa Jumapili kuanzia mwaka wa 2010 hadi 2012. Kwa ambavyo gazeti

hizi ni nyingi hatungeweza kuzichunguza zote kutokana na ukosefu wa muda. Kwa hivyo

mbinu hii ya uteuzi kimaksudi itakuwa ya manufaa kwa vile ilituwezesha kuchagua na

kuchunguza tu yale mashairi ambayo yatakuwa na masuala ya kiuchumi, kijamii na

kisiasa.

1.9.0 Ukusanyaji wa data

Data itaainishwa kulingana na masualaibuka pamoja na malengo ya utafiti. Data

imekusanywa kupitia kusoma kwa kina na kuchagua masuala-ibuka ya kisiasa, kiuchumi

na kijamii. Mtafiti amesoma kwa kuzingatia namna masuala hayo yanavyoshughulikiwa.

1.9.1 Upangaji wa Data

Tumepanga data yetu kulingana na :

(25)

15

ii. Malengo yetu kwa mfano lengo la kwanza limetuwezesha kuona masuala-ibuka,

la pili limetuelekeza katika kuangalia namna masuala hayo yameshughulikiwa

ilhali lengo la tatu limetuwezesha kudhihirisha dhima ya gazeti la Taifa Leo

katika maendeleo ya jamii nchini Kenya.

1.9.2 Uchanganuzi wa Data

Tumechanganua data kwa kuzingatia: malengo, maswali ya utafiti na mihimili ya

nadharia ambayo imeongoza utafiti wetu.

1.9.3 Uwasilishaji wa data

Matokeo ya utafiti yamewasilishwa kupitia kwa njia ya maelezo.

1.9.4 Hitimisho

Sura hii imeshughulikia mambo ya kimsingi kuhusiana na utafiti huu. Haya ni pamoja na

maelezo ya masuala muhimu kama vile: usuli, swala la utafiti, malengo ya utafiti na

maswali ya utafiti. Zaidi ya hayo, sababu za kuchagua mada na upeo wa utafiti ni

vipengele ambavyo vimeelezwa kwa kina. Pia, uhakiki wa yaliyoandikwa kuhusu mada,

misingi ya nadharia, mbinu za kukusanya; kuchanganua na kuwasilisha data

zimeshughulikiwa katika sehemu hii. Katika sura inayofuata tumechunguza fani na

(26)

16

SURA YA PILI

FANI NA MAUDHUI KATIKA USHAIRI WA KISWAHILI 2.0 Utangulizi

Katika sura hii tumechunguza fani na maudhui katika ushairi wa Kiswahili. Sura hii ni

muhimu kwa ambavyo ndiyo imetuwekea msingi thabiti wa kuegemea tunapochambua

fani na maudhui ya kisiasa, kiuchumi na kijamii kama yanavyowasilishwa katika

mashairi yanayochapishwa katika magazeti ya Taifa Leo Jumamosi na Taifa Jumapili.

Kupitia sura hii mtafiti amepata fursa ya kufafanua maana ya fani na kueleza kwa kina

mbinu mbalimbali za fani pamoja na tamathali za usemi zinazotumiwa na wasanii katika

kazi zao. Aidha maelezo kabambe yametolewa kuhusu maudhui yanayoendelezwa katika

utanzu wa ushairi wa Kiswahili. Jambo hili pia ni muhimu kwa vile linajenga msingi

imara katika kutathmini maudhui ya kisiasa, kiuchumi na kijamii kama

yanavyowasilishwa katika mashairi yanayochapishwa katika gazeti la Taifa Leo.

2.1.0 Fani Katika Utunzi Na Uwasilishaji Wa Ushairi

Ushairi ni chombo mwafaka kinachowezesha mwandishi kuufumbata upana na urefu wa

maisha katika maneno teule machache yaliyofinyangwa kisanaa. Uteuzi huo wa maneno

hupangiliwa kama vito kwenye kazi ya sonara anayefua chombo cha dhahabu hukuza

heba ya mkufu huo kwenye jicho la mvaaji na mtazamaji. Mpangilio wa maneno mateule

katika ushairi hujenga picha na tashbihi inayojenga maana na mantiki inayochorwa na

mshairi, lakini heba yake imo katika kukamilisha hisi kwa msomaji au msikilizaji; kama

hisi za mapenzi au chuki, dhiki na faraja, ari au mapuuza, ujinga au werevu, sifa au

(27)

17

vilivyorejelewa hapo juu kama mtindo, mkufu kama maudhui na mvaaji na mtazamaji

kama hadhira. Kwa mujibu wa King‟ei na Amata (2001) ingawa ushairi ni pambo la

lugha na usanifu, mashairi hayawezi kuwa yenye mvuto na mnato iwapo hayatahusu hisi

na mambo yanayofahamika na wote wanaoishi katika jamii husika.

Sehemu kubwa ya sifa na msisimuo wa shairi ni kwa msikilizaji wake kuweza kulielewa

kimaudhui na pia katika kitengo cha lugha. Ushairi ni utanzu wa fasihi ambao

hutofautiana na riwaya na tamthilia hasa katika umbo na matumizi maalum ya lugha.

Wakati ambapo fasihi ya kinathari kama vile tamthilia na riwaya hutumia lugha ya mjazo

au mtiririko, ushairi hutumia zaidi lugha ya mkato kama nyenzo muhimu ya kuwasilisha

maudhui kitaswira, kimafumbo na kimuhtasari (Gibbe 1990 na Senkoro 1988). Hali hiyo

imetokana na hoja kwamba, mshairi huwa hana wakati mwingi wa kujieleza au kufafanua

zaidi maelezo na mifano iliyotolewa. Kadhalika ushairi wa Kiswahili una matumizi ya

upeo wa juu wa lugha hasa ukilinganishwa na aina zingine za fasihi andishi.

Kwa hivyo, kila kipengele cha lugha kilichoteuliwa na kutumiwa katika utungo huo,

hushikilia nafasi muhimu katika uwasilishaji wake. Kwa sababu utamu wa lugha haupo

tu katika maudhui au ujumbe bali pia katika ujumi wa lugha unaotokana na umbuji au

ustadi uliotumiwa katika uwasilishaji wa ujumbe (Kunemah 2008 na Khatib 1999).

Wataalam mbalimbali wanatumia msamiati tofauti tofauti katika kurejelea mtindo.

King‟ei (2005:40) anauita mbinu za usanifu. Nao Ndung‟o na Wafula (1993:44)

wameuita fani. Mogambi (2005:19) naye anauita mtindo. Ndung‟o na Wafula (1993)

wakimnukuu Senkoro (1982:8) wanasema kuwa:

(28)

18

Kutokana na maelezo haya tunaweza kusema kuwa huu ni ustadi au ubingwa ama mbinu

ambazo msanii wa kazi ya fasihi hutumia katika kuwasilisha ujumbe wake kwa hadhira

lengwa. King‟ei (2005) anasema kuwa mbinu za usanifu ni maarifa au ufundi wa kisanaa

kwa jumla anayoshirikisha mtunzi ili kufanya kazi yake ya kifasihi kuwa na mvuto kwa

msomaji wake.

Mogambi (2005) anasema kwamba mtindo ni ufundi wa kuwasilisha mawazo yaliyomo

katika kazi ya msanii. Ndung‟o na Wafula (1993:45) wakimnukuu Mulokozi na Kahigi

(1979:53) katika kuchangia mjadala huu wa maana ya fani wanasema:

Fani ni sanaa, ni jumla ya vipengele vya lugha vilivyowekwa katika mpangilio mahsusi ili kutoa kwetu maana fulani.

Wanaendelea kusema kuwa mtindo ni jumla ya vipengele vya lugha msanii hutumia

katika kutoa maana fulani kwa hadhira. Maelezo haya yana utata kwa vile yatubidi

kuelewa maana ya lugha na zaidi ya hayo vipengele vyake.

Wakiendelea, wananukuu Taasisi ya ukuzaji mitaala (1988:168) ambayo nayo imeeleza

kuwa:

Fani ni umbo lililofasiriwa ili kuelezea hisia za fanani.

Maelezo haya yanatuelekeza kwa dhana kuwa mtindo ni jinsi msanii anavyofinyanga

kazi yake ya sanaa ili kuelezea mawazo na hisia zake kwa lugha ya ufasaha. Kutokana na

maelezo ya wataalamu tuliorejelea tunaona kuwa mtindo ni ujumla wa vipengele vyote

vya fasihi ambavyo msanii hutumia katika juhudi zake za kuelezea mawazo, maoni au

(29)

19

Miundo na vipengele mahsusi vya lugha ambavyo hutumiwa katika ushairi sharti kuweza

kusaidia katika uwasilishaji wa ujumbe uliokusudiwa. Ujumbe unapomfikia msomaji

ndipo hueleweka kwa yakini kwamba, mtunzi ameweza kufanikiwa katika kuwasiliana

na hadhira yake (Maitaria 2012). Aidha, mshairi wa Kiswahili ambaye hupuuza uteuzi

mwafaka wa miundo ya lugha huenda shairi lake likawa chapwa, chakavu na la

kuchosha. Matokeo ni kwamba, shairi linalowasilishwa huenda lisiwe lenye kugusa hisia.

Hadhira isipopata kishawishi cha kuupenda ushairi kwa kuuga zilizotumiwa, ujumbe

kusudiwa hautakuwa umewasilishwa ipasavyo (Darvin na Wamuhu 1994 na Mulokozi na

Kahigi 1982).

Kulingana na nadharia ya Semiotiki ni kuwa, miundo mwafaka ya lugha ni ile husheheni

sitiari, ishara na tamathali za semi zinazochochea usaili na tafakuri ya hadhira. Kwa

hivyo ni muhimu hadhira kuweza kupata kichocheo cha kujiuliza maswali ya kiutafakuri

kila wakati inaposema kazi hiyo ya kisanaa. Katika utunzi, miundo mahususi ya kauli

zilizotumiwa huwa ni ile ambayo husaidia katika ufasiri wa ujumbe kwa kuzingatia

miktadha mbalimbali ipatikanayo ndani ya ushairi na ile iliyopo katika uhalisi wa maisha

ya jamii.

Kwa kutumia kauli mahsusi hususan methali, hadhira huweza kufunuliwa kwa ubanifu

ukweli wa maisha ambao huafiki miktadha ya uhalisi wa maisha na utamaduni wa jamii

(Wamitila 2008 na Lo Liyong 1972). Lugha ya Kiswahili kama zilivyo lugha zingine

ulimwenguni, ina ukwasi mkubwa wa semi kama vile; methali, nahau, misemo, misimu

na kadhalika. Semi zitumiwazo katika uwasilishaji, huufanya utungo kutajirika zaidi

kiuchambuzi (Mosha 2002 na Senkoro 1988). Kwa hivyo msomaji anapoichambua

(30)

20

Ifahamike kuwa mfano kwamba mshairi anapotumia semi kama vile methali kama

chombo chake cha utunzi na uwasilishaji isichukuliwe kuwa ni hali ya kubainisha tu

weledi au ukwasi wake wa lugha, bali pia ni msingi wa kufaulisha upokezi wa ujumbe

(Hawkes 1977, Oslen 1973 na Nowottny 1968).

Kutokana na matumizi ya semi, ushairi wa Kiswahili huweza kuwa ni utanzu wenye

dhima maalum ya kuelimisha, kutafakarisha, kuonya, kuliwaza, kuzindua na kuhifadhi

amali adimu za utamaduni wa jamii. Iwapo uhalisi wa maisha na utamaduni wa jamii

umeathirika au umebadilika kwa namna fulani, semi hizi pia hushabihi mabadiliko hayo.

Kwa mtazamo huo basi ushairi wa Kiswahili ni utanzu ulio hai. Kwa mantiki hiyo, kunga

au fani zitumikazo huweza kubadilika kutegemea mabadiliko yanavyojiri katika jamii.

Kwa hivyo, semi hutumiwa mno katika miktadha ya kitamaduni, kijamii na kihistoria.

Endapo pana mabadiliko ya kitamaduni na kijamii watunzi hutumia semi ambazo

huchukuana vyema ma miktadha ya mabadiliko hayo. (Jalala 2008 na Kitogo 2002).

Mtindo katika kazi ya fasihi ni ile namna ambayo msanii hutunga kazi hiyo na kuipa sura

ambayo kimaudhui huainisha kanuni na kaida zilizofuatwa kama ni zilizopo (za

kimapokeo) au ni za kipekee. Kwa mujibu wa maelezo haya tunaweza kusema kuwa

mtindo ni upangaji wa maudhui katika kazi ya fasihi kwa njia ambayo hatimaye

hubainisha au kuonyesha nafsi na labda upekee wa mtunzi wa kazi hiyo. Kutokana na

mtindo wa kazi ya fasihi inakuwa vigumu kubadili sentensi au hata kidahizo katika kazi

hiyo bila kubadili mtindo wenyewe. Kwa hivyo tunaweza kusema kuwa mtindo ni ile

namna ambayo mtunzi huipa kazi yake ya kifasihi sura kimaudhui kwa njia ambayo

(31)

21

Kinachosisitizwa hapa ni kuwa hata kama watunzi wawili watashughulikia mada moja au

maudhui sawa ni sharti mitindo yao iwe tofauti. Mtindo ndio unaowawezesha

watazamaji, wasikilizaji na hata wasomaji kung‟amua mtunzi wa kazi bila kumwona au

kumtambulisha kwa jina.

Ndung‟o na Wafula (1993) wanasema kuwa pengine lugha ndicho kipengele muhimu

zaidi katika fani ya fasihi. Wanamnukuu Khatib (1981:16) anayedokeza kuhusu lugha

katika fasihi iwe simulizi au andishi:

Lazima iwe na utanashati na ulimbwende wa kipekee wenye mvuto na mnato na kuteka na kusisimua hisi za wasikilizaji, wasomaji au watazamaji.

Lugha ndiyo malighafi ya fasihi. Lugha inayotumika katika fasihi ni lugha ya kisanaa

inayopamba na inayokusudia kuibua hisia fulani kwa hadhira kulingana na jinsi

inavyotumiwa kwa lengo na kuchekesha, kukejeli, kusuta, kuchokoza, kutia hamasa au

kushawishi. King‟ei (2000: xii) anasema kuwa lugha ya kishairi ni ya mkato au

muhtasari. Mshairi hujaribu kuelezea fikira zake katika lugha iliyofinyangika, yenye

uchache wa maneno kama iwezekanavyo. Isitoshe, lugha ya ushairi ni lugha iliyo teule,

ni maneno yaliyochaguliwa kiufundi, kwa makini, ili kuleta athari, hisia na matokeo

maalum yaliyokusudiwa.

Tamathali za usemi za aina tofauti tofauti hutumika kujenga picha. Mifano ya tamathali

hizi ni kama; sitiari, tashhisi, takriri, misemo, methali, kejeli, ishara, tauria, simo,

ndimi-mseto, mbinu rejeshi/kisengere-nyuma, utohozi na kadhalika. Mbinu hizi tumezifafanua

(32)

22 2.1.1 Taswira.

Taswira ni mkusanyiko wa picha mbalimbali ambazo huundwa kwa njia ya maelezo na

wasanii katika kazi ya fasihi. Katika taswira twaweza kubainisha matumizi ya ishara

mbalimbali zinazowakilisha mawazo, dhana, vitu au watu (Ndung‟o na Wafula 1993:51).

Taswira huwa ni lugha ambayo inachora picha ya watu, vitu, wanyama au mahali kwa

kutumia ishara.

Katika taswira twaweza kubainisha maelezo ambayo jinsi yanavyopangwa na msanii

huweza kufanya hadhira zipate aina mbalimbali za hisi za kunusa, kusikia, kuona, kuonja

na kugusa.

Mbinu hii ya fani hutumiwa na washairi ili kunasa na kuteka hisia za hadhira zao.

Wasanii hutumia maneno ambayo huumba picha kamili ya mtu, kitu, hali, wazo, dhana

au uzoefu fulani wa jamii husika. Matumizi ya picha aghalabu huenda sambamba na yale

ya ishara. Tunatumia ishara hapa kwa maana ya dhana au mawazo mbalimbali

yanayotumiwa na wasanii katika kazi zao za fasihi kuwasilisha vitu, dhana au mawazo

mengine.

Matumizi mema ya taswira na ishara hutegemea ubingwa wa msanii wa kuchota mambo

mbalimbali katika mazingira ya jamii anayohusisha katika sanaa yake. Lengo kuu la

kutumia taswira ni kusisitiza maudhui yanayojadiliwa. Hiyo ina maana kuwa kufaulu au

kutofaulu kwa matumizi ya taswira kutatathminiwa kwa mizani ya jinsi taswira hizo

husaidia kuwasilisha au kuzuia maudhui yaliyokudiwa.

Kwa mfano katika gazeti la Taifa Jumapili 18-07-2010 kuna shairi lililo na anwani ya

(33)

23

mshororo wa tatu kuna taswira ya ukunguni kubishana kufanya ukata kutotoka. Taswira

ilidhamiriwa kumwezesha msomaji kupata kuelewa kwa undani namna uzembe

ulivyojongea na kufanya umaskini kupiga kambi kwa mtu anayependa kulaza damu.

Katika ubeti wa pili, mshororo wa pili kuna taswira ya hilako na aibu kumwandama

mzembe. Ubeti wa nne mshororo wa kwanza kuna taswira ya mtu aliye na bidii

anavyozidiwa na miliki na ile ya adui kutishwa na mafanikio ya mwenye bidii.

Katika ubeti wa mwisho mshororo wa tatu kuna taswira ya kuaga dhiki na kudidimisha

umaskini. Kwa jumla mtunzi Kimani Wa Mbogo amefanikiwa kuwasilisha maudhui yake

ya faida za bidii kupitia usawiri wa picha zinazoonyesha namna ambavyo mtu mkunguni

anavyoteseka maishani ilhali mwenye bidii anayafurahia maisha.

Aidha katika gazeti la Taifa Leo Jumamosi tarehe Saba Mei, mwaka wa elfu mbili na

kumi na moja kuna shairi lenye kichwa “Ogopa pia ni Ngao” ambamo malenga Rono

Leonard amewachorea taswira mbalimbali. Katika ubeti wa kwanza mshororo wa nne

kuna taswira ya ogopa kuwa ngao ya kujiepusha na majanga. Mshairi alidhamiria

kuonyesha namna mwoga anavyojiepusha na matatizo mengi. Katika ubeti wa pili

mshororo wa tatu kuna taswira ya mapenzi kumkaba mtu na daima kuwa msiba. Hadhira

imewezeshwa kuona nguvu za mapenzi na athari zake. Katika ubeti wa tatu mshororo wa

kwanza kuna taswira ya mtu aliyejiingiza utandoni. Mtunzi alidhamiria kuonyesha namna

mtu anayejiingiza katika mapenzi ni sawa na aliyejiingiza mtegoni. Vilevile katika ubeti

huo mshororo wa tatu mshairi anasawiri picha ya mtu anayebeba mambo mazito kwa

(34)

24

Katika ubeti wa sita mshororo wa tatu mshairi anasawiri taswira ya nyoyo

zilizokirihishwa kutokana na kuchushwa kwa dawa. Malenga alitumia mbinu hii ili

kuwaelimisha hadhira dhidi ya ubaya wa dawa za kulevya.

2.1.2 Jazanda

Hii ni hali ya kulinganisha uhalisi na hali fulani kwa kutumia maelezo (King‟ei 2005:41).

Kwa mfano katika gazeti la Taifa Leo Jumamosi, 23-10-2010 kuna shairi lililo na anwani

ya “Jongoo na Jogoo” ambamo mna matumizi ya jazanda. Malenga Hamisi Babusa

amelipa shairi lake anwani kwa kuzingatia mbinu ya jazanda. Katika shairi lake neno

jogoo ni jazanda. Neno hilo limetumika katika kuwarejelea watu wenye nguvu au walio

na ushawishi mkubwa. Vilevile katika shairi hilo neno jongoo limetumika kijazanda

kuwarejelea watu wanyonge.

Aidha katika shairi lenye anwani ya “Tafakari Ewe Msichana” lililochapishwa katika

gazeti la Taifa Leo Jumamosi, 05-03-2011 mna matumizi ya jazanda. Katika ubeti wa

tatu mshororo wa pili, nyota yako ni muma, malenga Muge Kipkemboi ametumia mbinu

ya jazanda iliyo na maana ya mafanikio ya anayerejelewa katika elimu. Pia katika ubeti

huohuo kipande cha utao kuna kauli, inayo mwangaza bora iliyo na maana ya matokeo

mazuri.

2.1.3 Chuku

Ni matumizi ya lugha kutoa maelezo yaliyotiwa chumvi ili kuyafanya mambo yaonekane

ni ya ajabu kupita kiasi. Msanii anatumia chuku ili kuongeza ladha katika kazi yake. Vile

vile anaweza kutumia mbinu hii ya fani ili kuchekesha au kusisitiza. Lengo kuu huwa ni

(35)

25 2.1.4 Balagha

Ni matumizi ya maswali ambayo hayahitaji au hayana majibu. Lengo kuu la kutumia

balagha au mbalagha ni kuwazindua wasomaji ili wazingatie na kuyafikiria

yanayorejelewa. Maswali ya balagha hukusudia kuleta uchochezi akilini mwa msomaji

(Mogambi 2005:22).

Kwa mfano katika shairi la “Maskini Wateseka” lililochapishwa katika gazeti la Taifa

Leo Jumamosi, 07-05-2011 mshairi Edison Wanga ametumia mbinu ya balagha kwa

ufanisi mkubwa ili kuwachochea hadhira kutafakari kuhusu maudhui ya hali ya kiuchumi

nchini. Katika ubeti wa kwanza kuna mshororo wa pili, “bei mepanda ki shari, mafukara

tule nini”. Hapa mshairi alifanikiwa kuichochea hadhira kuona taswira halisi ya namna

maskini wanavyoteseka. Pia katika ubeti wa tatu mshororo wa tatu, “Lini itaja nafuu, tena

bila pingamizi”. Hapa mshairi amefanikiwa kuzua taharuki kwa hadhira ili kujaribu

kutofakari ni lini hali itabadilika na kuwa nzuri. Vile vile katika ubeti wa tano mshororo

wa kwanza, “Kodi za nyumba zapanda, fukara tulale wapi”. Hapa mshairi alikuwa na nia

ya kuonyesha malazi ambalo ni hitaji la kimsingi. Pia katika mshororo wa pili, “Wanalia

kina dada, wana wanywe maji yapi”. Mshairi anazidi kuchochea hadhira kutafakari kwa

undani mateso yanayokumba maskini. Pia katika mshororo wa tatu, “Zaingia zino shida,

serikali iko wapi”. Mtunzi amefanikiwa katika matumizi ya balagha ili kuonyesha namna

serikali inakosa kuwajibika raia waliowachagua.

Vilevile katika gazeti la Taifa Jumapili la 29-04- 2012 kuna shairi lenye anwani Mvua ni

heri au balaa? Ustadh Nuhu Zubeir Bakari amefanikisha ujumbe wake kupitia mbinu ya

balagha au mbalagha. Ametumia mbinu hii ili kuifanya hadhira kupiga darubini kuhusu

(36)

26

“Mvua ni heri au balaa?” Kupitia kwa mbinu hii ya balagha hadhira inapata kutafakari

kupitia kwa taharuki ni kwa vipi mvua ni heri au balaa. Vilevile mshairi ametumia mbinu

hii katika kuunda kibwagizo chake, “Mvua kuanza kunyesha, ni heri au balaa?” Mbinu

hii ni ya manufaa kwa vile imemwezesha mshairi kutilia uzito dhamira yake. Pia katika

ubeti wan ne mshororo wa tatu, “Sasa wapi pana heri, ni mvua ama ni jua?” Mshairi

amefanikiwa kuwatafakarisha hadhira na kutathmini ni wapi penye heri iwapo ni kwa

mvua ama kwa jua. Vile vile katika ubeti wa saba mshororo wa tatu, “Wako wapi

manyapara, wakenya tuna huzuni” Mshairi ameweza kuwafanya hadhira wake kupiga

darubini viongozi na kuonyesha naman wanavyokosa kuwajibikia raia na matokeo yake

ni kuwa raia wanazama katika mateso.

2.1.5 Takriri

Ni marudiorudio ya sauti, silabi, neno, sentensi, wazo au ridhimu; ili kuleta athari kwa

msomaji wa shairi linalohusika (Mbunda 1993:6). Marudio haya hufanywa ili kutilia

mkazo jambo ama wazo.

Kwa mfano katika gazeti la Taifa Jumapili, 05-06-2010 malenga Kimanga Bismark

amefanikisha ujumbe wake katika shairi lenye anwani ya “Tupate Fahamu” kupitia

matumizi ya mbinu ya takriri. Mshairi anafanikisha dhamira yake kupitia mbinu ya

takriri. Kila mshororo umeanza kwa maneno mwalimu funza. Takriri hii ililenga

kusisitiza dhamira ya shairi.

Pia, mfano mwingine u katika gazeti la Taifa Leo Jumamosi, 13-02- 2010 ambamo mna

shairi lenye anwani “Ukosefu wa Ajira”. Ustadh Omar Bonge ametumia mbinu ya takriri

katika shairi hili ili kusisitiza dhamira yake kwa hadhira. Mifano ya matumizi ya mbinu

(37)

27

kazi hayawani” na katika ubeti wa pili mshororo wa kwanza,”Hayawani mso kazi, japo

awe sultani.” Katika mishororo hii miwili maneno mso kazi yamerudiwa. Pia katika ubeti

wa pili mshororo wa tatu, “Aamuru uvamizi, kuhatarisha amani” na katika ubeti wa tatu

mshororo wa kwanza, “Amani huhatarisha, watu wakiwa magadeni.” Katika mishororo

hii miwili maneno kuhatarisha amani yamekaririrwa. Vile vile katika ubeti wa tatu

mshororo wa tatu, “Mwishowe hujifundisha, kukaba watu gizani” na katika ubeti wa nne

mshororo wa kwanza, “Hukabwa gizani watu” katika mishororo hii miwili mbinu hii ya

takriri inabainika.

Katika ubeti wa nne mshororo wa tatu,”Haibadiliki katu, hali hii duniani” na katika ubeti

wa tano mshororo wa kwanza “Duniani hii hali, iko tele mitaani” katika mishororo hii

miwili maneno duniani hali hii yamekaririwa.

Katika ubeti wa tano mshororo wa tatu,”Ndipo huja wafadhili, kuwasajili vitani” na

katika ubeti wa sita mshororo wa kwanza,”Vitani kisajiliwa na kuingia kambini”. Katika

mishororo hii miwili maneno kuwasili vitani yamekaririwa.

Hatimaye malenga kupitia matumizi ya takriri amepata kusawiri kibwagizo

chake,”Ukosefu wa ajira, huchangia uhalifu” jambo linalomwezesha kufanikisha dhamira

yake kwa hadhira.

2.1.6 Tashhisi

Huu ni mtindo ambapo vitu ambavyo havina uhai au pia mawazo hupewa sifa au tabia za

binadamu. Mbinu hii hutumika kwa nia ya kuleta mawazo hayo na vitu hivyo karibu na

maisha ya binadamu kwani katika hali kama hiyo, msomaji atavielewa au atapata ujumbe

(38)

28

Kwa mfano katika shairi lenye kichwa “Jongoo na Jogoo” lililochapishwa katika gazeti la

Taifa Leo Jumamosi, 23-10-2010 mshairi Hamisi Babusa ametumia mbinu ya tashhisi

kwa nia ya kumwezesha hadhira kupata ujumbe wake kwa urahisi. Katika ubeti wa

kwanza mshororo wa kwanza, “Nasema nawe jongoo, ulojaa fondogoo”. Hapa neno

jongoo limepewa sifa za ubinadamu kwani ingawa hasemi katika muktadha huu ni kama

anashirikishwa katika mazungumzo kama binadamu.

Katika ubeti wa pili mshororo wa pili, “Acha wako uchokoo, hutamudu mtondoo” Hapa

mshairi anaonya jongoo kuacha uchokozi.

Katika ubeti wa tano mshororo wa kwanza, “Kwa jogoo udondoo, hatakuamba haloo”

Hapa bado mshairi anazidi kudhihirisha mbinu hii ya tashhisi anapowapa jogoo na

jongoo tabia za kusema kama binadamu. Katika ubeti wa mwisho mshororo wa pili,

“Jitizame kwa kioo, jione vyema jongoo” hapa jongoo anapewa sifa ya ubinadamu ya

kujitazama katika kioo.

Mfano mwingine u katika shairi lenye kichwa “Nikawalisha” lililochapishwa katika

gazeti la Taifa Jumapili, Julai 18, 2010. Malenga Kimani Wa Mbogo ametumia tashhisi

ili kumwezesha hadhira kupata taswira kamili ya maudhui ya uzembe na faida za bidii.

Kwa mfano katika ubeti wa kwanza mshororo wa tatu, “Ukata haukutoki, ukunguni

ukibisha” hapa neno ukunguni limepewa uwezo wa kubisha kama binadamu. Katika ubeti

wa nne mshororo wa pili, “Adui awe chuki, jasho langu kumtisha” hapa neno jasho

limepewa sifa za binadamu. Vilevile katika ubeti wa mwisho mshororo wa tatu, “Milele

(39)

29 2.1.7 Kuchanganya ndimi

Hali hii hutokea mzungumzaji au mwandishi anapotumia lugha mbili au zaidi

kuwasilisha maoni yake. Katika mashairi teule ya gazeti la Taifa Leo ingawa

yameandikwa katika lugha ya Kiswahili pana matumizi ya maneno kutoka lugha zingine.

Lengo kuu huwa ni kuonyesha kiwango cha elimu cha mtunzi au hadhira yake.

2.1.8 Inkisari

Hii ni mbinu ya kishairi ambapo mtunzi wa shairi anafupisha baadhi ya maneno. Lengo

kuu la matumizi ya inkisari ni ili kuafikia urari wa mizani katika shairi. Mbinu hii

hujitokezea aghalabu katika mashairi mengi.

Kwa mfano katika gazeti la Taifa Leo Jumamosi, 31-07-2010 mshairi Kevin Wamalwa

ameandika shairi lililo na kichwa “Nchi iko Kilindini” na katika shairi hili maneno

mbalimbali yamefupishwa kama vile:

(i) Kisikia badala ya ukisikia.

(ii)Miye badala ya mimi yeye.

(iii)Likuwa badala ya ilikuwa

(iv)Waso badala ya wasio

(v) Metupa badala ya wametupa

(vi)Litujia badala ya walitujia

(vii) Kajitia badala ya wakajitia

(viii) Nyusao badala ya nyuso zao

(ix)Sa‟ badala ya sasa

(x) Metuachia badala ya wamtuachia

(40)

30

Vilevile katika shairi la “Sherehe au Twapora?” Lililochapishwa katika gazeti la Taifa

Jumapili, 5-09-2010 malenga Wa Nyika Aggrey Juma ametumia vifupisho kama vile:

(i) Yalonichoma badala ya yaliyonichoma

(ii)Waloachwa badala ya walioachwa

(iii) Umbole badala ya umbo lake

(iv) Ndo badala ya ndio

2.1.9 Mazida

Hii ni mbinu ya kurefusha baadhi ya maneno kwa lengo la kupata urari wa mizani.

Vilevile sababu kubwa ya kurefusha huku ni kuwezesha kudhibiti uwiano wa mdundo

katika ushairi (Mazrui na Syambo 1992:37).

Kwa mfano katika gazeti la Taifa Leo Jumamosi, Julai 31, 2010 kuna shairi lenye anwani

“Nchi iko Kilindini” ambamo mshairi Wamalwa Kevin ametumia mbinu hii ya mazida ili

kuafikia urari wa mizani. Mifano ya mazida katika shairi hilo ni kama vile:

(i) Hawanayo badala ya hawana

(ii)Tukazamilie badala ya tukazame

Kwa mfano katika gazeti la Taifa Leo Jumamosi, 31-07- 2010 kuna shairi la Nchi iko

Kilindini ambamo mshairi Wamalwa Kevin amedhihiri matumizi ya mbinu hii ya

mazida. Kwa mfano katika ubeti wa tatu mshororo wa tatu, “Ndio zinayo mambo,

mashimo kila mwahali” hapa neno mwahali limetumiwa badala ya mahali. Pia katika

ubeti wa tano mshororo wa kwanza, “Waja wala makombo, hawanayo hata hali”. Hapa

neno hawanayo limerefushwa. Vilevile katika ubeti wa sita mshororo wa tatu, “Sa‟

(41)

31 2.1.10 Tabdila

Ni mbinu ya kubadilisha mpangilio wa sauti katika neno. Lengo kuu la kutumia tabdila ni

ili msanii aweze kuafikia urari wa vina.

Kwa mfano katika gazeti la Taifa Jumapili, 29-04-2012 kuna shairi lenye anwani “Mvua

ni heri au balaa?” Mbinu hii inadhihirika. Maneno yaliyobadilishwa mpangilio ni kama

vile:

(i) Tuyapigilie badala ya tuyapige.

(ii)Wafile badala ya wafa

Pia katika shairi “Tupate Fahamu” lililochapishwa katika gazeti la Taifa Jumapili, 5-06-

2010 kunadhihirika matumizi ya mbinu ya tabdila kwa lengo la kupata urari wa vina.

Neno lililobadilishwa utaratibu wake ni karimu badala ya karima.

2.1.11 Kuboronga Sarufi

Ni mbinu ya kubadilisha miundo ya sentensi katika shairi. Wasanii hutumia mbinu hii ili

kulipa shairi ridhimu au keleta uwiano wa mpigo.

Kwa mfano katika shairi lenye anwani ya “Ogopa pia ni Ngao” lililochapishwa katika

gazeti la Taifa leo Jumamosi, 7-05- 2011 pana matumizi ya kuboronga sarufi kwa lengo

la kulipa shairi ridhimu.

Mifano.

(i) Ubeti wa kwanza mshororo wa kwanza, “Ninalo jambo moyoni, nikilificha ni

deni” badala ya moyoni ninalo jambo, ni deni nikilificha.

(ii)Ubeti wa kwanza mshororo wa pili “Napanga yangu mizani, nikujuze kwa yakini”

(42)

32

(iii)Ubeti wa pili mshororo wa tatu, “Mapenzi yakikukaba, daima kwako msiba”

badala ya mapenzi yakikukaba, msiba kwako daima .

(iv)Kibwagizo,”Ogopa ni ngao pia, hukuepusha majanga” badala ya ogopa pia ni

ngao, majanga hukuepusha.

(v) Ubeti wa tatu mshororo wa kwanza,”Kujitosa mahabani, mejitosa utandoni”

badala ya mahabani kujitosa, utandoni mejitosa.

(vi)Ubeti wa tatu mshororo wa pili, “Tasabilia kanuni, sirini na hadharani” badala ya

kanuni tasabilia, hadharani na sirini.

(vii) Ubeti wa tatu mshororo wa tatu,”Mazito yaso kifani, tayabeba kwa imani”

badala ya mazito yaso kifani kwa imani tayabeba.

(viii) Ubeti wa nne mshororo wa kwanza, “Naogopa kuwa jizi, kuiba katu

siwezi” badala ya naogopa kuwa jizi, katu siwezi kuiba.

(ix)Ubeti wa tano mshororo wa pili, “Kuitimiza ahadi, kwangu sawa na marudi”

badala ya ahadi kuitimiza, kwangu sawa na marudi.

(x) Ubeti wa sita mshororo wa pili, “Siogopi kukanusha, lolote linalochusha” badala

ya kukanusha siogopi, linalochusha lolote.

(xi)Ubeti wa saba mshororo wa pili, “Hikiki change kifurushi, napulizia marashi”

badala ya kifurushi hiki changu, marashi napulizia

Pia katika shairi la “Kuruhusu Ukahaba” lililochapishwa katika gazeti la Taifa Leo

Jumamosi, 11-02- 2012 malenga Nuhu Zubeir Bakari amesheheni matumizi ya

(43)

33 Mifano.

(i) Ubeti wa nne mshororo wa kwanza, “Tuyalinde maadili, ili tuhepuke dhambi”

badala ya maadili tuyalinde ili dhambi tuhepuke.

(ii)Ubeti wa nne mshororo wa tatu, “Amekataza Jalali, nakufahamisha „jombi‟

badala ya Jalali amekataza „jombi‟ nakufahamisha.

(iii)Ubeti wa tano mshororo wa kwanza, “Msitangulize pesa, dhidi ya utu na dhima”

badala ya pesa msitangulize dhidi ya utu na dhima.

(iv)Ubeti wa tano mshororo wa pili,”Wengine kuwanyanyasa, kwa tabia za kinyama”

badala ya kuwanyanyasa wengine, kwa tabia za kinyama.

(v) Ubeti wa sita mshororo wa pili, “Umeijosea njia, kufanya ubarakala” badala ya

njia umeikosea, ubarakala kufanya.

(vi)Ubeti wa sita mshororo wa tatu, “Itakumeza dunia, utupwe kwenye jalala” badala

ya dunia itakumeza, utupwe kwenye jalala.

(vii) Ubeti wa saba mshororo wa kwanza, “Tunajua „Koinange”, wanapoliwaza

moyo” badala ya „Koinange” tunajua, moyo wanapoliwaza.

(viii)Ubeti wa nane mshororo wa kwanza “Twajua mwatka kodi, kuwatoze

makahaba” badala ya kodi mwataka tajua makahaba kuwatoza.

(ix)Ubeti wa nane mshororo wa pili, “Lakini kwa “saa-Godi”, hamtaipata toba”

badala ya kwa “saa-Godi” lakini, toba hamtaipata.

(x) Ubeti wa tisa mshororo wa kwanza,”Nakomelea komeo, hapa nafunga kiriba”

(44)

34 2.1.12 Methali

Ni usemi wa kisanii wa kimapokeo unaofikiriwa na jamii kuwa kweli na unaotumiwa

kufumbia au kupigia mfano na huwa umebeba maana pana kuliko maneno yenyewe

yanayotumiwa (TUKI, 2004). Methali katika ushairi wa Kiswahili hutumiwa kwa

malengo mbalimbali kama vile: kichepuo cha kufafanulia maelezo ya msingi, kulenga

mapigo ya ridhimu na udhibiti wa mwendo, chombo cha kufumbia fumbo, kuwezesha

hadhira kukumbuka kwa urahisi maudhui ama dhamira ya shairi, kudhibiti kaida za

kisarufi, kujenga taharuki, chombo cha kuwasilishia hisi na kubainisha itikadi ya mtunzi,

kuelekeza na kuiadilisha jamii na kadhalika.

Kwa mfano katika gazeti la Taifa leo Jumamosi, 2-06- 2012 kuna shairi la “Pengine

CCTV” ambamo mshairi Faith Suzen katika ubeti wa tatu mshororo wa kwanza,

ametumia methali sio ndwele yalopita, tuyagange yausoni. Pia katika ubeti wa tano

mshororo wa kwanza, ametumia methali anyolewapo mwenzio, maji ukitie chako.

Aidha katika gazeti la Taifa Leo Jumamosi, 9-07-2011 kuna shairi la “Waukwepaje

Ushuru” ambamo mshairi Salim Kalime Salim katika ubeti wa sita mshororo wa kwanza,

ametumia methali kwa binadamu mchungu, ni wa nguruwe mkuki. Pia katika ubeti wa

saba mshororo wa kwanza, ametumia methali haba na haba huleta, tukajikaza kibaba.

2.1.13 Utohozi.

Ni mbinu ya kuunda msamiati kutokana na msamiati wa lugha nyingine kwa kuzingatia

kanuni za kisarufi za lugha pongezi. Kwa mfano lugha ya Kiswahili imezua msamiati

mpya kutokana na maneno ya Kiingereza kama vile:

(i) Kompyuta kutokana na computer

(45)

35 (iii) Ofisi kutokana na office na kadhalika.

Lengo kuu la kutohoa maneno ni kuonyesha namna utanzu wa ushairi kama sanaa

unavyobadilika kiwakati na kuathiriwa na mifumo mipya katika jamii.

Kwa mfano katika gazeti la Taifa Leo Jumamosi, 11-02-2012 kuna shairi la “Kuruhusu

Ukahaba” ambamo Ustadh Nuhu Zubeir Bakari katika ubeti wa tatu mshororo wa tatu,

“Linapoanguka giza, waigawe „gudi-gudi‟. Hapa neno gudi-gudi limetoholewa kutokana

na lile la Kiingereza good-good. Pia katika ubeti wa nane mshororo wa pili,”Lakini kwa

„saa-Godi‟,hamtaipata toba” hapa neno Godi limetoholewa kutokana na lile la Kiingereza

God.

Aidha katika gazeti la Taifa Leo Jumamosi, 18-08-2012 kuna shairi la “Wanjiku sasa

Nafurahi” ambamo mshairi Elvis Ondieki katika ubeti wa pili mshororo wa

pili,”Wanangu walo sikuli, watezaanza kushaini”. Hapa maneno sikuli na kushaini

yemetoholewa. Neno skuli limetoholewa kutokana na lile la Kiingereza school ilhali

kushaini limetoholewa kutokana na yale ya Kiingereza to shine. Pia katika ubeti huohuo

mshororo wa tatu, “Na upishi wa makuli,‟tarejesha sitovuni” hapa neno stovu

limetoholewa kutokana na lile la Kiingereza stove. Vilevile katiba ubeti wa tatu mshororo

wa kwanza, “Nimeipata sababu, kumugombeza kondakta” hapa neno kondakta

limetoholewa kutokana na lile la Kiingereza conductor. Pia, katika ubeti wa nne

mshororo wa kwanza,”Kesho nikienda pampu, nitazidisha madaha” hapa neno pampu

(46)

36 2.1.14 Tashbihi

Hii ni tamathali ya ufananisho au mlinganisho wa vitu viwili au zaidi. Ni mtindo wa

kifani ambao kwao kitu kimoja au zaidi hulinganishwa au hufananishwa. Tamathali hii

hutumika ili kuwezesha hadhira kupata kwa urahisi dhamira ya mtunzi.

Kwa mfano katika gazeti la Taifa Leo Jumamosi, 11-06-2011 kuna shairi la “Mayatima

Tumekosani?” Ambamo mshairi Clare na Wanalela katika ubeti wa pili mshororo wa

pili,”Wanajamii wanatugemea, mfanowe ibilisi” hapa mtunzi aeleza kuwa wanajamii

wanalinganisha mayatima na shetani.

Vilevile katika gazeti la Taifa leo Jumamosi, 23-10- 2010 kuna shairi la “Jongoo na

Jogoo” ambamo malenga Hamisi babusa katika ubeti wa kwanza mshororo wa tatu,

“Wewe ni kama mnyoo ni dhaifu yako moo” hapa mshairi analinganisha jongoo na

mnyoo. Vilevile katika ubeti wan ne mshororo wa pili, “Akule ja poopoo, pamwe na

wako ukoo” hapa mshairi analinganisha jinsi jogoo anavyoweza kumla jongoo kama

poopoo.

2.1.15 Tanakali za sauti /onomatopoeia

Ni matumizi ya neno ambalo kwalo likitamkwa huelekea kutoa maana. Ni neno ambalo

kimsingi huiga sauti ya kitu (Msokile 1993: 38).

Kwa mfano katika gazeti la Taifa Leo Jumamosi, 23-10-2010 kuna shairi lenye anwani

“Jongoo na Jogoo” ambamo mshairi Hamisi Babusa anadhihirisha matumizi ya taharuki.

Kwa mfano, katika ubeti wa pili mshororo wa tatu, “Ikikohoa kohoo, utabaki uko foo”.

(47)

37 2.1.16 Misimu

Ni maneno au misemo inayozuka ghafla katika jamii kufuatana na matukio maalum

katika jamii hiyo (Msokile 1993).

Kwa mfano katika gazeti la Taifa Leo Jumamosi, 11-02-2012 kuna shairi lenye kichwa

“Kuruhusu Ukahaba” ambamo mna matumizi ya misimu. Kwa mfano katika ubeti wa

pili, “Uzinsi sio halali, hata ungepiga chambi” hapa neno chambi limetumika kwa maana

ya kukita mizizi au kukithiri. Pia, katika ubeti huohuo mshororo wa tatu, “Amekataza

Jalali, nakufahamisha „jombi‟”. Hapa neno jombi limetumika kwa maana ya adinasi.

Vilevile katika ubeti wa tano mshororo wa tatu, “Mnadunga mkinusa, kitawafika

kiyama”.hapa neno mnadunga ni la kimsimu lenye maana ya mnapachika.

2.1.17 Nidaa/Siyahi

Hii ina maana ya mwito fulani. Mwito wa sauti atoayo mtu kama ishara ya furaha,

masikitiko, chuki au hasira. Aidha huonyesha hali ya kushangaa au kukataa kitu (Kalome

na Maria 2001).

Kwa mfano katika gazeti la Taifa Jumapili, 12-02-2012 katika shairi lenye anwani “Bei

kuumiza watu Maskini!” Mshairi Swaleh Suheil Abeid amedhihiri matumizi ya nidaa.

Kwa mfano katika anwani “Bei kuumiza watu maskini! mbinu hii inadhihirika. Pia katika

kibwagizo, “Twaumia maskini, bei za vitu kupanda!” pia nidaa inadhihirika vilevile

katika ubeti wa pili, msohororo wa tatu, “Tungaupika mchuzi, kitoweo kina zani!” Pia

kunadhihirika matumizi ya siyahi. Pia katika ubeti wa tatu, mshororo wa kwanza,

“Kukicha bei za vitu, zapandishwa madukani!” Hapa pia mbinu hii imetumika kuonyesha

(48)

38 2.1.18 Nahau

Ni msemo uliojengwa kwa kutumia maneno ya kawaida, aidha aghalabu, huwa umesitiri

maana tofauti na ile iliyobebwa na maneno ya nahau yenyewe (Msokile 1993).

Kwa mfano katika gazeti la Taifa Leo Jumamosi, 9-10-2011 kuna shairi lililo na anwani

“Waukwepa je Ushuru” ambamo mshairi Kalim Kasim amedhihiri matumizi ya nahau

kama vile katika ubeti wa kwanza mshoro wa kwanza, “Swala lanikereketa, moyo lanipa

udhia” hapa msemo swala lanikereta kwa maana ya suala linalonisumbua. Pia katika

ubeti huohuo mshororo wa tatu, “Ulimi sitaufyata, nanyi nawaulizia” hapa msemo ulimi

sitaufyata umetumika kwa maana ya kuwa sitaacha kusema. Pia katika ubeti wa pili

mshororo wa kwanza, “Ni jambo lilokuwepo, toka enzi za azali”. Hapa msemo enzi za

azali umetumika kwa maana ya wakati wa zamani. Katika ubeti huohuo mshororo wa

tatu, “Jambo hili likiwepo, tukaona ni aali.” Hapa msemo jambo la aali umetumika kwa

maana ya jambo bora. Pia katika ubeti wa nne mshororo wa kwanza, “Migongo

tunaipinda, mashambani tukifika” Hapa nahau migongo tunaipinda imetumika kwa

maana ya kujikaza kazini. Katika ubeti wa tano mshororo wa tatu,”Wakenya ndio ni taka,

waso na wakuwakimu”. Hapa msemo waso na kuwakimu umetumika kwa maana ya

kukosa wa kuwatimizia mahitaji yao. Vilevile katika ubeti wa sita mshororo wa pili,

“Wakenya twala machungu, wao na pesa lukuki”. Hapa msemo wakenya twala

machungu umetumika kwa maana ya wakenya kuteseka sana na pia pesa lukuki kwa

maana ya pesa nyingi. Hatimaye katika ubeti wa saba mshororo wa tatu, “Sa tujazeni

kibaba, sikatae katakata” hapa msemo sikatae katakata kwa maana ya kutokataa kamwe.

2.1.19 Isitiari.

Tamathali ya usemi ya aina hii hulinganisha vitu vya aina mbili au zaidi vyenye sifa

References

Related documents

The most common neural system diffusion model is the Ornstein-Uhlenbeck process (Lansky et al., 1989). This equation is derived in terms of the RC circuit model. Assuming the

The fuzzy based expert system applied to the battery scheduling based on the measured real time data or forecasted data as follows: Time(T), The Battery State of

“Initial” model prediction for the work by Lee and Choi [2] of the change in (a) incident UV light intensity passing through the soot layer as a function of time, and (b)

The literature on informal caregiving needs more elucidation on how women assume the transition to careproviders within the family structure and how women see and feel about the

was  utilized  to  evaluate  professional  development  manuscripts,  collected  based  on  their   focus  of  professional  development  for  community

Our results show that, although tetrasomic inheritance creates additional con fi gurations of lineages that have unique probabilities of coalescence compared to those for

2) Despite the design principles and standards contained in both codes IS and Euro standards codes are same, but they vary in configuration, design criteria, detailing and

In our examination, we have tried different inside and outside releases like void, surface and crown utilizing factual parameters, for example, skewness and